< Waefeso 2 >

1 Kama vile mlivyo kuwa mmekufa katika makosa na dhambi zenu.
Och eder också, då I döde voren genom öfverträdelser och synder;
2 Ilikuwa katika haya kwamba kwanza mlienenda kulingana na nyakati za ulimwengu huu. Mlikuwa mkienenda kwa kufuata mtawala wa mamlaka ya anga. Hii ndiyo roho yake yule afanyaye kazi katika wana wa kuasi. (aiōn g165)
Der I uti fordom vandraden, efter denna verldenes lopp, efter den Förstan, som magt hafver i vädret, nämliga efter den andan, som nu verkar i otrones barn; (aiōn g165)
3 Sisi wote hapo mwanzo tulikuwa miongoni mwa hawa wasioamini. Tulikuwa tukitenda kwa namna ya tamaa mbaya za miili yetu. Tulikuwa tukifanya mapenzi ya mwili na ufahamu wetu. Tulikuwa kwa asili wana wa ghadhabu kama wengine.
Ibland hvilka vi ock alle fordom vandrat hafve, uti vårt kötts begärelser, och gjordom hvad köttet och sinnet lyste; och vorom af naturen vredsens barn, såsom ock de andre.
4 Lakini Mungu ni mwingi wa rehema kwa sababu ya pendo lake kubwa alilotupenda sisi.
Men Gud, som är rik i barmhertigheten, för sina stora kärleks skull, der han oss med älskat hafver;
5 Wakati tulipokuwa wafu katika makosa yetu, alituleta pamoja katika maisha mapya ndani ya Kristo. Ni kwa neema kwamba mmeokolewa.
Den tid vi ännu döde vorom i synderna, hafver han oss samt med Christo gjort lefvande (genom nådena ären I frälste);
6 Mungu alitufufua pamoja na kutufanya kukaa pamoja katika mahali pa mbingu ndani ya Kristo Yesu.
Och hafver samt med honom uppväckt oss, och samt med honom satt oss i det himmelska väsendet i Christo Jesu;
7 Alifanya hivi ili katika nyakati zijazo aweze kutuonesha utajiri mkuu wa neema yake. Hutuonesha sisi hili kwa njia ya wema wake ndani ya Kristo Yesu. (aiōn g165)
På det han i tillkommande tid bevisa skulle sine nåds öfversvinneliga rikedom, genom sina mildhet öfver oss, i Christo Jesu. (aiōn g165)
8 Kwa neema mmeokolewa kwa njia ya imani. Na hii haikutoka kwetu. Ni zawadi ya Mungu.
Ty af nådene ären I frälste, genom trona; och det icke af eder, Guds gåfva är det;
9 Haitokani na matendo. Matokeo yake, asiwepo mmoja wapo wa kujisifu.
Icke af gerningar, på det ingen skall berömma sig.
10 Kwa sababu sisi tu kazi ya Mungu, tumeumbwa katika Kristo Yesu kutenda matendo mema. Ni matendo haya ambayo Mungu aliyapanga tangu zamani za kale kwa ajili yetu, ili tutembee katika hayo.
Ty vi äre hans verk, skapade i Christo Jesu till goda gerningar, till hvilka Gud oss tillförene beredt hafver, att vi uti dem vandra skole.
11 Kwa hiyo kumbukeni kwamba hapo zamani mlikuwa watu wa Mataifa kwa jinsi ya mwili. Mnaitwa “msio na tohara” kwa kile kinachoitwa tohara ya mwili inayofanywa kwa mikono ya binadamu.
Derföre, tänker derpå, att I som fordom efter köttet hafven varit Hedningar, och vorden kallade förhud af dem som kallas omskärelse efter köttet, den med handene sker;
12 Kwa wakati huo mlikuwa mmetengwa na Kristo. Mlikuwa wageni kwa watu wa Israel. Mlikuwa wageni kwa agano la ahadi. Hamkuwa na uhakika wa wakati ujao. Mlikuwa bila Mungu katika ulimwengiu.
Att I på den tid voren utan Christo, främmande och utan Israels borgareskap, och främmande ifrå löftsens Testament, intet hopp hafvande, och voren utan Gud i verldene.
13 Lakini sasa katika Kristo Yesu ninyi ambao hapo mwanzo mlikuwa mbali na Mungu mmeletwa karibu na Mungu kwa damu ya Kristo.
Men nu, I som i Christo Jesu ären, och fordom fjerran voren, ären nu när vordne, genom Christi blod.
14 Kwa maana yeye ndiye amani yetu. Alifanya wawili kuwa mmoja. Kwa mwili wake aliuharibu ukuta wa utengano ambao ulikuwa umetutenganisha, huo uadui.
Ty han är vår frid, den af bådom hafver gjort ett; och hafver nederbrutit medelbalken, i det att han igenom sitt kött borttog ovänskapen;
15 Kwamba alikomesha sheria ya amri na kanuni ili kwamba aumbe mtu mmoja mpya ndani yake. Akafanya amani.
Nämliga lagen, som i budordom stod; på det han skulle af tvåm skapa ena nya mennisko i sig sjelfvom, och frid göra.
16 Alifanya hivi ili kuwapatanisha makundi mawili ya watu kuwa mwili mmoja kwa Mungu kupitia msalaba. Kwa njia ya msalaba aliufisha uadui.
Och att han skulle försona dem båda med Gudi uti en kropp, genom korset; och hafver dödat ovänskapen genom sig sjelf;
17 Yesu alikuja na kutangaza amani kwenu ninyi mliokuwa mbali na amani kwao wale waliokuwa karibu.
Och är kommen, och hafver igenom Evangelium bådat eder frid, I som fjerran voren; så ock dem som när voro.
18 Kwa maana kwa njia ya Yesu sisi wote wawili tuna nafasi kwa yule Roho mmoja kuingia kwa Baba.
Ty genom honom hafve vi både tillgång uti en Anda till Fadren.
19 Hivyo basi, ninyi watu wa mataifa si wasafiri na wageni tena. Bali ni wenyeji pamoja na wale waliotengwa kwa ajili ya Mungu na wajumbe katika nyumba ya Mungu.
Så ären I icke nu mera gäster och främmande; utan helgamanna medborgare, och Guds husfolk;
20 Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii. Kristo Yesu mwenyewe alikuwa jiwe kuu la pembeni.
Uppbyggde på Apostlarnas och Propheternas grund, der Jesus Christus öfverste hörnestenen är;
21 Katika yeye jengo lote limeungamanishwa pamoja na kukua kama hekalu ndani ya Bwana.
På hvilken hela byggningen tillhopafogad växer till ett heligt tempel i Herranom.
22 Ni ndani yake ninyi nanyi mnajengwa pamoja kama mahali pa kuishi pa Mungu katika Roho.
På hvilken ock I med uppbyggde varden, Gudi till ett hemman, genom Andan.

< Waefeso 2 >