< Mhubiri 10 >

1 Kama nzi walio kufa husababisha manukato kutoa harufu ya uozo, hivyo hivyo upumbavu kidogo hushinda hekima na heshima.
Dead flies cause the ointment of the apothecary to send forth a stinking smell: so does a little folly him that is in reputation for wisdom and honor.
2 Moyo wa mtu mwenye hekima huelekea kulia, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.
A wise man’s heart is at his right hand; but a fool’s heart at his left.
3 Wakati mpumbavu anapotembea barabarani, fikira zake zina upungufu, ikithibitisha kwa kila mtu kwamba ni mpumbavu.
Yes also, when he that is a fool walks by the way, his wisdom fails him, and he says to every one that he is a fool.
4 Kama jaziba za mtawala zikiinuka kinyume na wewe, usiache kazi yako. Utulivu unaweza kutuliza ukatili mkubwa.
If the spirit of the ruler rise up against you, leave not your place; for yielding pacifies great offenses.
5 Kuna uovu niliouona chini ya jua, aina ya kosa ambalo huja kutoka kwa mtawala:
There is an evil which I have seen under the sun, as an error which proceeds from the ruler:
6 Wapumbavu wanapewa nafasi za uongozi, wakati watu walio faulu wanapewa nafasi za chini.
Folly is set in great dignity, and the rich sit in low place.
7 Nimewaona watumwa wakipanda farasi, na watu walio faulu wakitembea kama watumwa juu ya ardhi.
I have seen servants on horses, and princes walking as servants on the earth.
8 Yeyote anayechimba shimo anaweza kutumbukia yake, na popote mtu anayevunja ukuja, nyoka anaweza kumuuma.
He that digs a pit shall fall into it; and whoever breaks an hedge, a serpent shall bite him.
9 Yeyote achongaye mwawe, anaweza kuumizwa nayo. Na mtu achongaye mbao, anaweza kujihatarisha kwa hiyo.
Whoever removes stones shall be hurt therewith; and he that splits wood shall be endangered thereby.
10 Kama chuma bapa kisicho na makali, na mtu hainoi, kisha ni lazima atumie nguvu nyingi, lakini hekima hutoa faida kwa ufaulu.
If the iron be blunt, and he do not whet the edge, then must he put to more strength: but wisdom is profitable to direct.
11 Kama nyoka akiuma kabla hajafurahi, hivyo hakuna faida kwa mfurahishaji.
Surely the serpent will bite without enchantment; and a babbler is no better.
12 Maneno ya kinywa cha mtu mwenye hekima yana huruma. Lakini midomo ya mpumbavu humumeza mwenyewe.
The words of a wise man’s mouth are gracious; but the lips of a fool will swallow up himself.
13 Kama maneno yanavyo anza kutiririka mdomoni mwa mpumbavu, ujinga hutoka, na mwisho mdomo wake hutiririka wazimu mbaya.
The beginning of the words of his mouth is foolishness: and the end of his talk is mischievous madness.
14 Mpumbavu huongeza maneno, lakini hakuna ajuaye kinachokuja. Ni nani ajuaye baada yake?
A fool also is full of words: a man cannot tell what shall be; and what shall be after him, who can tell him?
15 Jasho la wapumbavu huwavaa wao, hivyo hawajui hata barabara ya kwenda mjini.
The labor of the foolish wearies every one of them, because he knows not how to go to the city.
16 Ole wako ardhi kama mfalme wako ni kijana mdogo, na kama viongozi wako huanza karamu ahsubuhi!
Woe to you, O land, when your king is a child, and your princes eat in the morning!
17 Lakini umebarikiwa ardhi kama mfalme wako ni mwana wa waungwana, na kama vingozi wako hula wakati muafaka, kwa nguvu, na sio kwa ulevi.
Blessed are you, O land, when your king is the son of nobles, and your princes eat in due season, for strength, and not for drunkenness!
18 Kwa sababu ya uvivu paa huanguka. Na kwa sababu isiyo fanya kazi nyumba hupata ufa.
By much slothfulness the building decays; and through idleness of the hands the house drops through.
19 Watu huandaa chakula kwa kicheko, divai huleta furaha maishani, na fedha hutimiza hitaji kwa kila kitu.
A feast is made for laughter, and wine makes merry: but money answers all things.
20 Usimlaani mfalme, hata katika akili, na usiwalaani wenye mali katika chumba chako cha kulala. Kwa kuwa ndege wa angani inaweza kuchukua maneno yako. Chochote kilicho na mabawa kinaweza kusambaza jambo.
Curse not the king, no not in your thought; and curse not the rich in your bedchamber: for a bird of the air shall carry the voice, and that which has wings shall tell the matter.

< Mhubiri 10 >