< Torati 6 >

1 Sasa haya ni maagizo, amri, na sheria ambazo Yahwe Mungu wetu ameniamuru mimi kuwafundisha ninyi, ili kwamba muweze kuzishika katika nchi ambayo mnaenda ng'ambo ya pili ya Yordani kumiliki,
Und dies ist das Gebot, die Satzungen und die Rechte, so Jehovah, euer Gott, geboten hat euch zu lehren, auf daß ihr sie tut in dem Lande, in das ihr hinüberziehet, um es einzunehmen.
2 ili kwamba mpate kumheshimu Yahwe wenu, ili muzishike amri zake zote na maagizo ninayowaamuru-ninyi, wana wenu na wana wa wana wenu, siku zenu zote za maisha, ili kwamba siku zenu ziongezeke.
Damit du fürchtest Jehovah, deinen Gott, und haltest alle Seine Satzungen und Seine Gebote, die ich dir gebiete, du und dein Sohn und deines Sohnes Sohn, alle Tage deines Lebens, und auf daß deine Tage verlängert werden.
3 Kwa hiyo wasikilizeni, Israeli, na kuzishika ili kwamba iweze kuwa vizuri kwenu, ili kusudi muweze kuzidi mno kwenye nchi itiririkayo maziwa na asali, kama Yahwe Mungu wa Baba zenu, amewaahidi atafanya.
Und höre, Israel, und hüte dich, daß du es tust, auf daß es dir gut gehe und ihr euch sehr mehret, wie Jehovah, der Gott deiner Väter, zu dir geredet hat, in dem Lande, das von Milch und Honig fließt.
4 Sikiliza, Israel: Yahwe Mungu wetu ni mmoja.
Höre, Israel, Jehovah, unser Gott, ist ein Jehovah.
5 Mtampenda Yahwe Mungu wenu kwa moyo wenu wote, kwa roho zenu zote, na kwa akili zenu zote.
Und du sollst lieben Jehovah, deinen Gott, von deinem ganzen Herzen und von deiner ganzen Seele und mit deiner ganzen Kraft.
6 Maneno ninayowaamuru ninyi leo yatakuwa katika moyo wenu;
Und diese Worte, die ich dir heute gebiete, seien in deinem Herzen.
7 na mtayafundisha kwa bidii kwa watoto wenu, mtayazungumza wakati mkaapo katika nyumba zenu, wakati mlalapo, na wakati mwinukapo.
Und sollst sie deinen Söhnen einschärfen, und sollst davon reden wenn du sitzest in deinem Hause oder auf dem Wege gehst, und wenn du dich niederlegst und wenn du aufsteht;
8 Utazifunga kama ishara juu ya mkono wako, nayo yatakuwa utepe kati ya macho yako.
Und sollst sie als Zeichen auf deine Hand binden und sie seien als Stirnband zwischen deinen Augen.
9 Utaziandika kwenye miimo ya mlango ya nyumba yako na kwenye malango.
Und sollst sie auf die Türpfosten deines Hauses und an deine Tore schreiben.
10 Wakati Yahwe Mungu wako akuleta kwenye nchi ambayo aliaapa kwa baba zako, Ibrahimu, Isaka, na Yakobo, kwamba angekupa, pamoja na miji mikubwa na mizuri ambayo hamkuijenga,
Und es soll geschehen, wenn dich Jehovah, dein Gott, in das Land hineingebracht, daß Er deinen Vätern, dem Abraham, dem Isaak und dem Jakob geschworen hat, dir zu geben, große und gute Städte, die du nicht bautest.
11 na nyumba zilizojaa kila aina ya vitu vizuri ambavyo hamkuzifanya, visima ambavyo hamkuvichimba, mashamba na miti ya mizeituni ambayo hamkuipanda, mtakula na kutosheka-
Und Häuser, alles Guten voll, die du nicht gefüllt, und ausgehauene Brunnen, die du nicht ausgehauen, Weinberge und Ölgärten, die du nicht gepflanzt hast, und davon issest und satt wirst;
12 basi iweni makini ili kwamba msije kumsahau Yahwe, aliyewaleta toka nchi ya Misri, toka nyumba ya utumwa.
So hüte dich, daß du Jehovahs nicht vergessest, Der dich aus Ägyptenland, aus dem Hause der Knechte, ausgeführt hat.
13 Mtamheshimu Yahwe Mungu wenu, yeye mtamwabudu, na mtaapa kwa jina lake.
Jehovah, deinen Gott, sollst du fürchten und Ihm dienen und bei Seinem Namen schwören.
14 Hamtawaendea miungu mingine, miungu ya watu wanaowazunguka wote-
Ihr sollt nicht anderen Göttern nachgehen, von den Göttern der Völker, die rings um euch sind.
15 kwa kuwa Yahwe Mungu wenu katikati yenu ni Mungu wa wivu- kama mtafanya, hasira ya Yahwe Mungu wenu atawasha dhidi yenu na atawaangamiza kutoka kwenye uso wa dunia.
Denn ein eifernder Gott ist Jehovah, dein Gott, in deiner Mitte, auf daß nicht der Zorn Jehovahs, deines Gottes, entbrenne wider dich, und Er dich von den Angesichten des Bodens vernichte.
16 Hamtamjaribu Yahwe Mungu wenu kama mlivyomjaribu huko Massah.
Ihr sollt Jehovah, euren Gott, nicht versuchen, wie ihr Ihn in Massah versucht habt.
17 Kwa bidii mtayashika maagizo ya Yahwe Mungu wenu, maagizo yake makini, na amri ambazo amewaamuru.
Ihr sollt halten die Gebote Jehovahs, eures Gottes, und Seine Zeugnisse und Seine Satzungen, die Er dir geboten hat;
18 Mtafanya kile kilicho sahihi na kizuri katika macho ya Yahwe, kwamba iwe vizuri kwenu, na kwamba muweze kuingia na kumiliki nchi nzuri ambayo Yahwe aliaapa kwa baba zenu,
Und sollst tun, was recht und gut ist in den Augen Jehovahs, auf daß es dir gut gehe und du hineinkommst und das gute Land einnehmest, das Jehovah deinen Vätern geschworen hat;
19 kuwaondoa maadui zenu wote mbele zenu, kama Yahwe alivyosema.
Auf daß Er vertreibe alle deine Feinde vor dir, wie Jehovah geredet hat.
20 Wakati mwana wako auliza kwa wakati unaokuja, kusema,”Ni zipi amri za gano, sheria, na amri zingine ambazo Yahwe Mungu wetu alituamuru?
Wenn dich dein Sohn morgen fragen wird und sagen: Was sollen diese Zeugnisse und die Satzungen und die Rechte, die Jehovah, unser Gott, euch geboten hat?
21 Basi utasema kwa mwana wako, tulikuwa watumwa wa Farao huko Misri, Yahwe alitutoa Misri kwa mkono wa uweza,
So sollst du deinem Sohne sagen: Wir waren Knechte dem Pharao in Ägypten; und Jehovah hat uns mit starker Hand aus Ägypten ausgeführt.
22 na alionesha ishara na maajabu, makuu na makali, Misri kwa Farao, na kwa nyumba yake yote, mbele ya macho yenu,
Und Jehovah tat große und schlimme Zeichen und Wahrzeichen an Ägypten, an Pharao und an seinem ganzen Haus vor unseren Augen.
23 na alitutoa kutoka huko, ili kwamba atulete ndani, kutupa nchi ambayo aliaapa kwa baba zetu.
Und führte uns aus von da, auf daß Er uns heranbrächte und gäbe uns das Land, das Er unseren Vätern geschworen hatte.
24 Yahwe alituamuru daima kuzishika amri hizi, kumuogopa Yahwe Mungu wetu kwa uzuri wetu, ili kwamba atuweke hai, kama tulivyo leo.
Und Jehovah hat uns geboten, all diese Satzungen zu tun, Jehovah, unseren Gott, zu fürchten, auf daß es uns gut gehe alle Tage, daß Er uns am Leben erhalte, wie es heutigentags ist.
25 Kama tutashika maagizo haya yote mbele ya Yahwe Mungu wetu kama alivyotuamuru, hii itakuwa haki yetu.
Und es wird für uns Gerechtigkeit sein, wenn wir daran halten, daß wir all dies Gebot tun vor Jehovah, unserem Gott, wie Er uns geboten hat.

< Torati 6 >