< Torati 29 >

1 Haya ni maneno ambayo Yahwe alimuamuru Musa kuwaambia watu wa Israeli katika nchi ya Moabu, maneno ambayo yaliongezwa katika agano alilolifanya pamoja nao kule Horebu.
These, are the words of the covenant which Yahweh commanded Moses to solemnise with the sons of Israel in the land of Moab, —besides the covenant, which he solemnised with them in Horeb.
2 Musa aliwaita Waisraeli wote na kuwaambia, “Mmeona kila kitu ambacho Yahwe alifanya mbele ya macho yenu katika nchi ya Misri kwa Farao, kwa watumishi wake wote, na kwa nchi yake yote –
And Moses called unto all Israel and said unto them, —Ye yourselves, saw all that Yahweh did before your eyes in the land of Egypt, unto Pharaoh and unto all his servants and unto all his land:
3 mateso makubwa ambayo macho yenu yaliona, ishara, pamoja na ile miujiza mikubwa.
the great provings which thine own eyes saw, —those great signs and wonders:
4 Lakini mpaka leo Yahwe hajawapatia moyo wa kufahamu, macho ya kuona, au masikio ya kusikia.
yet hath Yahweh not given onto you a heart to know, or eyes to see or ears to hear, —until this day.
5 Nimewaongoza kwa miaka arobaini jangwani; mavazi yenu hayakuchakaa juu yenu, na ndala zenu hazikuchakaa miguuni mwenu.
I led you, therefore forty years in the desert, —your mantles fell not with age, from off you, even thy sandal, fell not with age from off thy foot:
6 Hamkula mkate wowote, na wala hamkunywa divai yoyote au kinywaji chochote chenye ulevi, ili kwamba muweze kujua kuwa mimi ni Yahwe Mungu wenu.
Bread, ye did not eat, and wine and strong drink, ye did not drink, —that ye might know that, I, Yahweh, was your God.
7 Mlipokuja mahali hapa, Sihoni, mfalme wa Heshboni, na Ogu, mfalme wa Bashani, walikuja dhidi yetu kutupiga, na tukawapiga.
And when ye entered into this place, then came forth Sihon king of Heshbon and Og king of Bashan to meet us in battle and we smote them;
8 Tulichukua ardhi yao na kuwapa kama urithi Wareubeni, kwa Wagadi, na kwa nusu ya kabila ya Manase.
and we took their land, and gave it for an inheritance unto the Reubenites and unto the Gadites, —and unto the half tribe of Manasseh.
9 Kwa hiyo shikilia maneno ya agano hili na kuyatenda, ili ufanikiwe katika kila kitu ufanyacho.
Ye must, therefore, keep the words of this covenant, and do them, —that ye may prosper in all that ye do.
10 Nyie wote, mnasimama leo, mbele ya Yahwe Mungu wenu; machifu wenu, makabila yenu, wazee wenu, na maafisa wenu – wanaume wote wa Israeli,
Ye are stationed, to-day, all of you, before Yahweh your God, —your heads your tribes, and your elders and your officers, every man of Israel;
11 watoto wenu, wake zenu, na wageni ambao wamo miongoni wa kambi yenu, kutoka kwa yule anayekata mbao zenu mpaka kwa yule atekaye maji.
your little ones your wives, and thy sojourner that is in the midst of thy camps, —from him that heweth thy wood unto him that draweth thy water:
12 Mpo hapa ili kwamba muingie katika agano la Yahwe Mungu wenu na katika kiapo ambacho Yahwe Mungu wako anafanya na wewe leo,
that thou mayest pass through into the covenant of Yahweh thy God and into his oath, —which Yahweh thy God is solemnising with thee, to-day:
13 ili kwamba awafanye leo kuwa watu wake, na kwamba aweze kuwa Mungu kwa ajili yako, kama alivyonena kwako, na kama alivyoapa kwa mababu zako, kwa Abrahamu, kwa Isaka na kwa Yakobo.
that he may confirm thee to-day as his own people, while, he, becometh thine own God, as he spake unto thee, —and as he sware unto thy fathers, unto Abraham unto Isaac and unto Jacob.
14 Kwa maana ninafanya agano hili na kiapo hiki sio na wewe tu –
And not with you alone, am I solemnising this covenant and this oath;
15 pamoja kila mtu aliyesimama hapa pamoja nasi leo mbele ya Yahwe Mungu wetu – bali na wale ambao hawapo pamoja nasi leo pia.
but with him who is here with us, standing to-day before Yahweh our God, —and with him who is not here with us to-day.
16 Unajua jinsi tulivyoishi katika nchi ya Misri, na jinsi tulivyopenya miongoni mwa mataifa ambao uliwapita.
(For, ye, know, how we dwelt in the land of Egypt, —and how we passed through the midst of the nations which ye did pass through;
17 Mmeona sanamu zao zinazokera zilizotengenezwa kwa mbao na mawe, fedha na dhahabu, ambazo zilikuwa miongoni mwenu.
and ye saw their disgusting images, and their manufactured gods, —the wood and the stone, the silver and the gold that are with them.)
18 Hakikisha hakuna kati yenu mwanamume, mwanamke, ukoo, au kabila ambaye moyo wake unamuacha Yahwe Mungu wetu leo, ili kwenda na kuabudu miungu ya mataifa hayo. Hakikisha hakuna kati yenu mzizi utakaozaa nyongo na pakanga.
Lest there be among you—a man or a woman or a family or a tribe, whose heart is turning to-day, from Yahweh our God, to go and serve the gods of those nations, —lest there be among you a root fruitful of poison and wormwood;
19 Wakati mtu huyo anaposikia maneno ya laana hii, atajifariji moyoni mwake na kusema, “Nitakuwa na amani, ingawa natembea katika ukaidi wa moyo wangu”. Hii itaangamiza ubichi pamoja na ukavu.
and so it come to pass while he is hearing the words of this oath, that he will bless himself in his heart—saying, Prosperity, shall I have, although in the stubbornness of my heart, I go on, —so that the drunkenness addeth to the thirst:
20 Yahwe hatamsamehe, lakini badala yake, hasira ya Yahwe na wivu wake utambanika mtu huyo, na laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki vitakuwa juu yake, na Yahwe ataliondoa jina lake kutoka mbinguni.
Yahweh will not be willing to forgive him, but, then, will the anger of Yahweh and his jealousy smoke against that man, and all the oath that is written in this scroll, shall settle down upon him, —and Yahweh wipe out his name from under the heavens;
21 Yahwe atamuweka kando kwa ajili ya maafa kutoka katika makabila yote ya Israeli, kwa kuzingatia laana zote za agano ambazo zimeandikwa katika kitabu hiki cha sheria.
and Yahweh single him out for calamity, out of all the tribes of Israel, —according to all the oaths of the covenant that is written in this scroll of the law.
22 Kizazi kifuatacho, watoto wako watakaoinuka baada yako, na mgeni atakayekuja kutoka nchi ya mbali, watazungumza watakapoona mapigo juu ya nchi hii na magonjwa ambayo Yahwe ameyafanya yawe –
So that the generation coming after—your sons who shall rise up after you, and the foreigner who shall come in from a far-off land, will say—when they see the plagues of that land and the sicknesses thereof wherewith Yahweh hath made it sick:
23 na watakapoona kuwa nchi yote imekuwa salfa na chumvi ichomayo, ambapo hakuna kitu kipandwacho au kuzaa matunda, ambapo hapaoti mmea wowote, kama anguko la Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, ambayo Yahwe aliangamiza katika ghadhabu na hasira yake –
brimstone and salt burning up all the land thereof, it shall not be sown neither shall it shoot forth neither shall there come up thereon any herbage, —like the overthrow of Sodom and Gomorrah, Admah and Zeboiim, which Yahweh overthrow in his anger and in his wrath:
24 watasema kwa pamoja na mataifa mengine, “Kwa nini Yahwe amefanya hili katika nchi hii? Joto ya hasira hii kali inamaanisha nini?”
yea all the nations will say, For what cause, hath Yahweh done, thus, unto this land? what meaneth this great heat of anger?
25 Kisha watu watasema, “Ni kwa sababu walitelekeza agano la Yahwe, Mungu wa mababu zao, alilofanya nao alipowatoa kutoka Misri,
Then will men say, Because they forsook the covenant of Yahweh the God of their fathers, —which he solemnised with them, when he brought them forth out of the land of Egypt;
26 na kwa sababu waliondoka na kutumikia miungu mingine na kuzisujudu, miungu ambayo hawakujiua na ambayo hakuwapatia.
and went and served other gods, and bowed down to them, —gods which they had not known, and in which he had given them no share:
27 Kwa hiyo hasira ya Yahwe imewaka dhidi ya nchi hii, ili kuleta juu yake laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki.
therefore did the anger of Yahweh kindle upon that land, —to bring in upon it all the curse that is written in this scroll;
28 Yahwe amewang’oa kutoka nchini kwao kwa hasira, kwa ghadhanu, na kwa ghadhabu kali, na kuwatupa katika nchi nyingine, leo.
and therefore hath Yahweh rooted them out, from off their own soil, in anger and in wrath and in great indignation, —and cast them into another land as at this day.
29 Mambo ya siri ni ya Yahwe Mungu wetu pekee; lakini mambo yaliyofichuliwa ni ya kwetu milele pamoja na wazawa wetu, ili tufanye maneno yote ya sheria hii.
The secret things, [belong unto Yahweh our God] and, the things that are revealed, belong to us and to our children unto times age-abiding, that we may do all the words of this law.

< Torati 29 >