< Torati 23 >

1 Mwanamume aliyejeruhiwa kwa kupondwa au kukatwa haruhusiwi kuingia katika kusanyiko la Yahwe.
He who is wounded in the testicles, or has his private part cut off, shall not enter into the assembly of Jehovah.
2 Mwana haramu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
A bastard shall not enter into the assembly of Jehovah, even to the tenth generation none of his shall enter into the assembly of Jehovah.
3 Muamori au Mmoabu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
An Ammonite or a Moabite shall not enter into the assembly of Jehovah, even to the tenth generation none belonging to them shall enter into the assembly of Jehovah forever,
4 Hii ni kwa sababu hawakukutana nanyi kwa mkate na maji barabarani mlipokuwa mmetoka nje ya Misri, na kwa sababu walimkodisha Balaamu mwana wa Beoro kutoka Pethoro kule Aramu Naharaimu, awalaani.
because they met you not with bread and with water on the way, when ye came forth out of Egypt, and because they hired against thee Balaam the son of Beor from Pethor of Mesopotamia, to curse thee.
5 Lakini Yahwe Mungu wako hakumsikiliza Balaamu; badala yake, Yahwe Mungu wako aligeuza laana kuwa baraka kwenu, kwa sababu Yahwe Mungu wako aliwapenda.
Nevertheless Jehovah thy God would not hearken to Balaam, but Jehovah thy God turned the curse into a blessing to thee, because Jehovah thy God loved thee.
6 Hamtakiwi kutafuta amani au mafanikio yao, katika siku zenu zote.
Thou shall not seek their peace nor their prosperity all thy days forever.
7 Hutakiwi kumchukia Muedomi, kwa maana ni kaka yako; hutakiwi kumchukia Mmisri, kwa maana ulikuwa mgeni katika nchi yake.
Thou shall not abhor an Edomite, for he is thy brother. Thou shall not abhor an Egyptian, because thou were a sojourner in his land.
8 Wazawa wa kizazi cha tatu wanaozaliwa kwao wanaweza kuwa katika kusanyiko la Yahwe.
The sons of the third generation who are born to them shall enter into the assembly of Jehovah.
9 Utakapotembea kijeshi dhidi ya maadui zako, basi unapaswa kujitenga na kila aina ya uovu.
When the army goes forth against thine enemies, then thou shall keep thee from every evil thing.
10 Iwapo miongoni mwenu kuna mwanamume ambaye sio msafi kwa sababu ya jambo lililofanyika kwake usiku, basi anatakiwa atoke nje ya kambi ya jeshi; hatakiwi kurudi kambini.
If there be among you any man, who is not clean by reason of an accident by night, then he shall go abroad out of the camp. He shall not come inside the camp.
11 Jioni ikifika, anatakiwa ajiogeshe kwa maji; na jua likizama atarudi ndani kambini.
But it shall be, when evening comes on, he shall bathe himself in water, and when the sun is down, he shall come inside the camp.
12 Pia unatakiwa kuwa na eneo nje ya kambi ambayo utakwenda;
Thou shall have a place also outside the camp, where thou shall go forth abroad.
13 na utakuwa na kitu katika zana zako cha kuchimbia; utakapochuchumaa kujisaidia, unapaswa kuchimbia nacho na kisha kurudishia udongo na kufunika kile kilichotoka kwako.
And thou shall have a paddle among thy weapons, and it shall be, when thou sit down abroad, thou shall dig with it, and shall turn back and cover that which comes from thee.
14 Kwa maana Yahwe Mungu wako anatembea miongoni mwa kambi yenu kuwapa ushindi na kuwapa maadui zenu mkononi mwenu. Kwa hiyo kambi yenu lazima iwe takatifu, ili kwamba asione kitu chochote kichafu miongoni mwenu na kuwaacha.
For Jehovah thy God walks in the midst of thy camp, to deliver thee, and to give up thine enemies before thee. Therefore thy camp shall be holy, that he may not see an unclean thing in thee, and turn away from thee.
15 Hutakiwi kumrudishia bwana mtumwa aliyetoroka kwake.
Thou shall not deliver to his master a servant who is escaped from his master to thee.
16 Mruhusu aishi pamoja nawe, katika mji wowote atakaochagua. Usimuonee.
He shall dwell with thee, in the midst of thee, in the place which he shall choose within one of thy gates, where it pleases him best. Thou shall not oppress him.
17 Hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa mabinti wa Israeli, na wala hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa wana wa kiume wa Israeli.
There shall be no prostitute of the daughters of Israel, neither shall there be a sodomite of the sons of Israel.
18 Hautakiwi kuleta mshahara wa kahaba au mshahara wa mbwa katika nyumba ya Yahwe Mungu wako kwa kiapo chochote; kwa maana vyote hivi na machukizo mbele ya Yahwe Mungu wako.
Thou shall not bring the hire of a harlot, or the wages of a dog, into the house of Jehovah thy God for any vow, for even both these are an abomination to Jehovah thy God.
19 Hutakiwi kumkopesha Muisraeli mwenzako kwa riba – riba ya fedha, riba ya chakula, au riba ya kitu chochote kinachokopeshwa kwa riba.
Thou shall not lend upon interest to thy brother: interest of money, interest of food, interest of anything that is lent upon interest.
20 Kwa mgeni unaweza kukopesha kwa riba; lakini kwa Muisraeli mwenzako haupaswi kukopesha kwa riba, ili kwamba Yahwe Mungu wako aweze kukubariki katika kila jambo uwekalo mkono wako, katika nchi ambayo mnaenda kumiliki.
To a foreigner thou may lend upon interest, but to thy brother thou shall not lend upon interest, that Jehovah thy God may bless thee in all that thou put thy hand to, in the land where thou go in to possess it.
21 Unapofanya kiapo kwa Yahwe Mungu wako, haupaswi kukawia kuikamilsha, kwa maana Yahwe Mungu wako hakika atadai kiapo hicho; itakuwa dhambi kako usipokamilisha.
When thou shall vow a vow to Jehovah thy God, thou shall not be slack to pay it. For Jehovah thy God will surely require it of thee, and it would be sin in thee.
22 Lakini iwapo utajizuia kutoa kiapo, haitakuwa dhambi kwako.
But if thou shall forbear to vow, it shall be no sin in thee.
23 Kile ambacho kimetoka kinywani mwako unapaswa kukifuata na kukitekeleza; kulingana na kiapo ulichotamka kwa Yahwe Mungu wako, chochote ulichotamka kwa hiari kwa kinywa chako.
That which has gone out of thy lips thou shall observe and do, according as thou have vowed to Jehovah thy God, a freewill offering, which thou have promised with thy mouth.
24 Utakapokwenda katika shamba la mizabibu la jirani yako, unatakiwa kula mizabibu idadi yoyote unayotaka, lakini hautakiwi kuhifadhi yoyote katika kikapu chako.
When thou come into thy neighbor's vineyard, then thou may eat thy fill of grapes at thine own pleasure, but thou shall not put any in thy vessel.
25 Utakapokwenda katika shamba la zao lililoiva la jirani yako, unaweza kuvuna kichwa cha mavuno kwa mkono wako, lakini haupaswi kutumia mundu kuvuna zao lililoiva la jirani yako.
When thou come into thy neighbor's standing grain, then thou may pluck the ears with thy hand, but thou shall not move a sickle to thy neighbor's standing grain.

< Torati 23 >