< Torati 23 >

1 Mwanamume aliyejeruhiwa kwa kupondwa au kukatwa haruhusiwi kuingia katika kusanyiko la Yahwe.
“凡外肾受伤的,或被阉割的,不可入耶和华的会。
2 Mwana haramu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
“私生子不可入耶和华的会;他的子孙,直到十代,也不可入耶和华的会。
3 Muamori au Mmoabu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
“亚扪人或是摩押人不可入耶和华的会;他们的子孙,虽过十代,也永不可入耶和华的会。
4 Hii ni kwa sababu hawakukutana nanyi kwa mkate na maji barabarani mlipokuwa mmetoka nje ya Misri, na kwa sababu walimkodisha Balaamu mwana wa Beoro kutoka Pethoro kule Aramu Naharaimu, awalaani.
因为你们出埃及的时候,他们没有拿食物和水在路上迎接你们,又因他们雇了美索不达米亚的毗夺人比珥的儿子巴兰来咒诅你们。
5 Lakini Yahwe Mungu wako hakumsikiliza Balaamu; badala yake, Yahwe Mungu wako aligeuza laana kuwa baraka kwenu, kwa sababu Yahwe Mungu wako aliwapenda.
然而耶和华—你的 神不肯听从巴兰,却使那咒诅的言语变为祝福的话,因为耶和华—你的 神爱你。
6 Hamtakiwi kutafuta amani au mafanikio yao, katika siku zenu zote.
你一生一世永不可求他们的平安和他们的利益。
7 Hutakiwi kumchukia Muedomi, kwa maana ni kaka yako; hutakiwi kumchukia Mmisri, kwa maana ulikuwa mgeni katika nchi yake.
“不可憎恶以东人,因为他是你的弟兄。不可憎恶埃及人,因为你在他的地上作过寄居的。
8 Wazawa wa kizazi cha tatu wanaozaliwa kwao wanaweza kuwa katika kusanyiko la Yahwe.
他们第三代子孙可以入耶和华的会。”
9 Utakapotembea kijeshi dhidi ya maadui zako, basi unapaswa kujitenga na kila aina ya uovu.
“你出兵攻打仇敌,就要远避诸恶。
10 Iwapo miongoni mwenu kuna mwanamume ambaye sio msafi kwa sababu ya jambo lililofanyika kwake usiku, basi anatakiwa atoke nje ya kambi ya jeshi; hatakiwi kurudi kambini.
“你们中间,若有人夜间偶然梦遗,不洁净,就要出到营外,不可入营;
11 Jioni ikifika, anatakiwa ajiogeshe kwa maji; na jua likizama atarudi ndani kambini.
到傍晚的时候,他要用水洗澡,及至日落了才可以入营。
12 Pia unatakiwa kuwa na eneo nje ya kambi ambayo utakwenda;
“你在营外也该定出一个地方作为便所。
13 na utakuwa na kitu katika zana zako cha kuchimbia; utakapochuchumaa kujisaidia, unapaswa kuchimbia nacho na kisha kurudishia udongo na kufunika kile kilichotoka kwako.
在你器械之中当预备一把锹,你出营外便溺以后,用以铲土,转身掩盖。
14 Kwa maana Yahwe Mungu wako anatembea miongoni mwa kambi yenu kuwapa ushindi na kuwapa maadui zenu mkononi mwenu. Kwa hiyo kambi yenu lazima iwe takatifu, ili kwamba asione kitu chochote kichafu miongoni mwenu na kuwaacha.
因为耶和华—你的 神常在你营中行走,要救护你,将仇敌交给你,所以你的营理当圣洁,免得他见你那里有污秽,就离开你。”
15 Hutakiwi kumrudishia bwana mtumwa aliyetoroka kwake.
“若有奴仆脱了主人的手,逃到你那里,你不可将他交付他的主人。
16 Mruhusu aishi pamoja nawe, katika mji wowote atakaochagua. Usimuonee.
他必在你那里与你同住,在你的城邑中,要由他选择一个所喜悦的地方居住;你不可欺负他。
17 Hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa mabinti wa Israeli, na wala hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa wana wa kiume wa Israeli.
“以色列的女子中不可有妓女;以色列的男子中不可有娈童。
18 Hautakiwi kuleta mshahara wa kahaba au mshahara wa mbwa katika nyumba ya Yahwe Mungu wako kwa kiapo chochote; kwa maana vyote hivi na machukizo mbele ya Yahwe Mungu wako.
娼妓所得的钱,或娈童所得的价,你不可带入耶和华—你 神的殿还愿,因为这两样都是耶和华—你 神所憎恶的。
19 Hutakiwi kumkopesha Muisraeli mwenzako kwa riba – riba ya fedha, riba ya chakula, au riba ya kitu chochote kinachokopeshwa kwa riba.
“你借给你弟兄的,或是钱财或是粮食,无论什么可生利的物,都不可取利。
20 Kwa mgeni unaweza kukopesha kwa riba; lakini kwa Muisraeli mwenzako haupaswi kukopesha kwa riba, ili kwamba Yahwe Mungu wako aweze kukubariki katika kila jambo uwekalo mkono wako, katika nchi ambayo mnaenda kumiliki.
借给外邦人可以取利,只是借给你弟兄不可取利。这样,耶和华—你 神必在你所去得为业的地上和你手里所办的一切事上赐福与你。
21 Unapofanya kiapo kwa Yahwe Mungu wako, haupaswi kukawia kuikamilsha, kwa maana Yahwe Mungu wako hakika atadai kiapo hicho; itakuwa dhambi kako usipokamilisha.
“你向耶和华—你的 神许愿,偿还不可迟延;因为耶和华—你的 神必定向你追讨,你不偿还就有罪。
22 Lakini iwapo utajizuia kutoa kiapo, haitakuwa dhambi kwako.
你若不许愿,倒无罪。
23 Kile ambacho kimetoka kinywani mwako unapaswa kukifuata na kukitekeleza; kulingana na kiapo ulichotamka kwa Yahwe Mungu wako, chochote ulichotamka kwa hiari kwa kinywa chako.
你嘴里所出的,就是你口中应许甘心所献的,要照你向耶和华—你 神所许的愿谨守遵行。
24 Utakapokwenda katika shamba la mizabibu la jirani yako, unatakiwa kula mizabibu idadi yoyote unayotaka, lakini hautakiwi kuhifadhi yoyote katika kikapu chako.
“你进了邻舍的葡萄园,可以随意吃饱了葡萄,只是不可装在器皿中。
25 Utakapokwenda katika shamba la zao lililoiva la jirani yako, unaweza kuvuna kichwa cha mavuno kwa mkono wako, lakini haupaswi kutumia mundu kuvuna zao lililoiva la jirani yako.
你进了邻舍站着的禾稼,可以用手摘穗子,只是不可用镰刀割取禾稼。”

< Torati 23 >