< Torati 17 >

1 Haupaswi kumtolea dhabihu Yahwe Mungu wako ng'ombe au kondoo aliye na kasoro au kitu chochote kibaya, kwa kuwa hiyo itakuwa chukizo kwa Yahwe Mungu wako.
“You shall not immolate to the Lord your God a sheep or an ox, in which there is a blemish or any defect at all; for this is an abomination to the Lord your God.
2 Kama kunapatikana miongoni mwenu, ndani ya malango ya mji wowote ambao Yahwe Mungu wenu anawapatia, mwanaume yoyote au mwanamke ambaye anafanya uovu mbele ya Yahwe Mungu wenu kuiharibu agano lake -
When there will have been found among you, within one of your gates which the Lord your God will give to you, a man or a woman who is doing evil in the sight of the Lord your God, and who is transgressing his covenant,
3 yoyote ambaye ameenda na kuabudu miungu mingine na kuisujudia, wala jua, mwezi, au kati ya jeshi la mbinguni- hakuna chochote nimekuamuru,
so as to go and serve foreign gods and adore them, such as the sun and the moon, or any of the host of heaven, which I have not instructed,
4 na kama ungeambiwa kuhusu hiki, au kama una mifugo- basi unapaswa kufanya uchunguzi wa makini. Kama ni kweli na hakika kwamba chukizo kama hilo limefanyika Israeli-
and when this will have been reported to you, and, upon hearing it, if you have inquired diligently and have found it to be true, that the abomination is being done in Israel:
5 -basi utamleta huyo mwanaume au mwanamke, aliyefanya uovu huu, katika malango ya mji, kwamba mwanaume kabisa au mwanamke, na umponde huyo mtu mpaka kufa.
you shall lead forward the man or the woman who has perpetrated this most wicked thing to the gates of your city, and they shall be stoned to death.
6 Kwa kinywa cha mashahidi wawili, au mashahidi watatu, itakuwa yeye anayepaswa kuuwawa; lakini kwa kinywa cha shahidi mmoja peke hatauwawa.
By the mouth of two or three witnesses, he who is to be put to death shall perish. Let no one be killed with only one person speaking testimony against him.
7 Mkono wa mashahidi unapaswa kuwa wa kwanza kumuuwa, na badae mkono wa watu wote; na mtamuondoa muovu miongoni mwenu.
First, the hands of the witnesses shall be upon him who will be put to death, and lastly, the hands of the remainder of the people shall be sent forth. So may you take away the evil from your midst.
8 Kama jambo linatokea ambalo ni gumu kwenu kufanya maamuzi- pengine swali la mauaji au kifo cha ajali, haki ya mtu mmoja na haki ya mtu mwingine, au swali moja la aina ya kuzulu kufanyika, au aina nyingine ya jambo-mambo ya utata ndani ya malango yenu, basi utapaswa kwenda kwenye eneo ambalo Yahwe Mungu wako atachagua kama patakatifu pake.
If you have perceived that there is among you a difficult and doubtful matter of judgment, between blood and blood, cause and cause, leprosy and leprosy, and if you will have seen that the words of the judges within your gates vary: rise up and ascend to the place which the Lord your God will choose.
9 Utapaswa kwenda kwa makuhani, wazao wa Lawi, na kwa mwamuzi atakayetumika kwa wakati huo; mtatafuta ushauri wao, na watawapa ninyi maamuzi.
And you shall approach the priests of the Levitical stock, and the judge, who shall be among them at that time, and you shall inquire of them, and they will reveal to you the truth of the judgment.
10 Mnapaswa kufuata sheria mliyopewa, katika eneo Yahwe atachagua kama patakatifu pake. Mtakuwa makini kufanya kila kitu ambacho wanawaelekeza kufanya.
And you shall accept whatever they will say, those who preside in the place which the Lord will choose, and whatever they will teach you,
11 Fuata sheria wanayowafundisha, na kufanya kulingana na maamuzi wanawapa. Msigeuke kutoka kwa kile wanawambia, kwa kulia au kushoto.
in accord with his law, and you shall follow their sentence. Neither shall you turn aside to the right or to the left.
12 Yeyote anayefanya kwa kiburi, kwa kutomsikiliza kuhani anayesimama kutumika mbele ya Yahwe Mungu wako, au kwa kutomsikiliza mwamuzi- huyu mtu atakufa; mtaweka mbali uovu kutoka Israeli.
But whoever will be arrogant, unwilling to obey the order of the priest who ministers at that time to the Lord your God, and the decree of the judge, that man shall die. And so shall you take away the evil from Israel.
13 Watu wote wanapaswa kusikia na kuogopa, na kutofanya kwa kiburi tena.
And when the people hear about this, they shall be afraid, so that no one, from that time on, will swell with pride.
14 Wakati mlipokuja kwenye nchi ambayo Yahwe Mungu anawapa, na wakati mnamiliki na kuanza kuishi ndani yake, na halafu unasema, 'Nitajiwekea mfalme juu yangu, kama mataifa yote yanayonizunguka mimi,'
When you will have entered into the land which the Lord your God will give to you, and you possess it, and you live in it, and you say, ‘I will appoint a king over me, just as all the surrounding nations have done,’
15 basi unapaswa kwa hakika kujiwekea mfalme juu yako mtu yeyote ambaye Yahwe atachagua. Unapaswa kujiweka kama mfalme juu yako mtu yeyote kutoka miongoni mwa ndugu zenu. Haupaswi kuweka mgeni, ambaye si ndugu yenu, juu yenu.
you shall appoint him whom the Lord your God will choose from among the number of your brothers. You cannot make a man of another people king, one who is not your brother.
16 Lakini hapaswi kuzidisha farasi kwa ajili yake, wala kusababisha watu kurudi Misri ili kwamba aweze kuzidisha farasi, kwa kuwa Yahwe alikwisha sema kwako, 'Unapaswa kuanzia sasa usirudi njia hiyo tena.'
And when he will have been appointed king, he shall not multiply horses for himself, nor lead the people back into Egypt, having been exalted by the number of his horsemen, especially since the Lord has instructed you never to return along the same way.
17 Na hapaswi kuzidisha wake kwa ajili yake, ili kwamba moyo wake usigeuke kotoka kwa Yahwe; wala hapaswi sana kuzidisha kwa ajili yake fedha au dhahabu.
He shall not have many wives, who might allure his mind, and he shall not have immense weights of silver and gold.
18 Wakati aketipo kwenye kiti cha enzi cha ufalme wake, anapaswa kuandika kwenye kitabu kwa ajili yake nakala ya sheria hii, kutoka kwenye sheria ambayo iko mbele ya makuhani, ambao ni Walawi.
Then, after he has been seated upon the throne of his kingdom, he shall write for himself the Deuteronomy of this law in a volume, using a copy from the priests of the Levitical tribe.
19 Kitabu kinapaswa kuwa na yeye, na anapaswa kusoma ndani yake kwa siku zake zote, ili kwamba aweze kujifunza kumheshimu Yahwe Mungu wako, ili kwamba ashike maneno yote ya sheria hii na amri hizi, kuzishika.
And he shall have it with him, and he shall read it all the days of his life, so that he may learn to fear the Lord his God, and to keep his words and ceremonies, which are instructed in the law.
20 Anapaswa kufanya hivi ili kwamba moyo wake usiinuliwe zaidi ya ndugu zake, na ili kwamba asigeuke mbali na amri, kwa kulia au kwa kushoto' kwa kusudi kwamba aweze kuzidisha siku zake katika ufalme wake, yeye na watoto wake, miongoni mwa Israel.
And so may his heart not become exalted with arrogance over his brothers, nor turn aside to the right or to the left, so that he and his sons may reign for a long time over Israel.”

< Torati 17 >