< Danieli 12 >

1 Katika kipindi hicho, Mikaeli, jemedari mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka. Kutakuwa na wakati wa mateso ambao haujawahi kutokea tangu mwanzo wa taifa lolote mpaka kipindi hicho. Katika muda huo watu wako wataokolewa, yeyote ambaye jina lake litapatikana katika kitabu.
E naquele tempo se levantará Michael, o grande príncipe, que se levanta a favor dos filhos do teu povo, e haverá um tempo de angústia, qual nunca houve, desde que houve nação até àquele tempo; porém naquele tempo livrar-se-á o teu povo, todo aquele que se achar escrito no livro.
2 Na wengi wa wale waliolala katika mavumbi ya dunia watainuka. baadhi kwa uzima wa milele na baadhi kwa ajili ya fedheha na matwezo ya milele.
E muitos dos que dormem no pó da terra ressuscitarão, uns para vida eterna, e outros para vergonha e para nojo eterno.
3 Wale wenye hekima watang'ara kama mng'ao wa anga la juu, na wale wenye kuwaelekeza wengine katika haki, watakuwa kama nyota milele na milele.
Os entendidos pois resplandecerão como o resplandor do firmamento, e os que a muitos ensinam a justiça como as estrelas sempre e eternamente.
4 Lakini wewe, Danieli, yafunge maneno haya; kihifadhi kitabu kikiwa kimetiwa chapa mpaka nyakati za mwisho. Watu wengi watakimbia huku na kule, na maarifa yataongezeka.
E tu, Daniel, fecha estas palavras e sela este livro, até ao fim do tempo: então muitos passarão, lendo-o, e a ciência se multiplicará.
5 Kisha mimi, Danieli, nilitazama, na kulikuwa na malaika wengine wawili wamesimama. Mmoja alisimama katika upande huu wa ukingo wa mto, na mwingine alisimama katika ukingo wa upande mwingine wa mto.
E eu, Daniel, olhei, e eis que estavam em pé outros dois, um desta banda, à beira do rio, e o outro da outra banda, à beira do rio.
6 Mmoja wao alimwambia mtu aliyevaa nguo za kitani, yeye aliyekuwa juu ya mkondo wa mto, “Je itachukua muda gani mpaka mwisho wa matukio haya ya kushangaza?”
E ele disse ao homem vestido de linho, que estava sobre as águas do rio: Até quando será o fim das maravilhas?
7 Nilimsikia mtu yule aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu katika mkondo wa mto, aliinua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni na kuapa kwa yeye aishiye milele kwamba itakuwa kwa wakati, nyakati, na nusu wakati. Na wakati nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimeshaharibiwa, mambo haya yote yatakuwa yamemalizika.
E ouvi o homem vestido de linho, que estava sobre as águas do rio, e levantou a sua mão direita e a sua mão esquerda ao céu, e jurou por aquele que vive eternamente que depois do determinado tempo, determinados tempos e a metade do tempo, e quando acabar de espalhar o poder do povo santo, todas estas coisas serão cumpridas.
8 Nilisikia, lakini sikufahamu. Basi nikamwuliza, “Bwana wangu, mambo haya yote yatakuwa na matokeo gani?”
Eu pois ouvi, mas não entendi; por isso eu disse: Senhor meu, qual será o fim destas coisas?
9 Alisema, “Nenda zako Danieli, kwa kuwa maneno yamefungwa na kutiwa chapa mpaka wakati wa mwisho.
E disse: vai, Daniel, porque estas palavras estão fechadas e seladas até ao tempo do fim.
10 Watu wengi watakuwa wametakaswa, wameoshwa, na kusafishwa, lakini waovu wataenenda katika uovu.
Muitos serão purgados, e embranquecidos, e provados; mas os ímpios obrarão impiamente, e nenhum dos ímpios entenderá, mas os entendidos entenderão.
11 Katika muda ule ambapo sadaka ya kawaida ya kuteketezwa itakapokuwa imeondolewa na chukizo la uharibifu liliosababisha ukiwa limesimamishwa, kutakuwa na siku zipatazo 1, 290.
E desde o tempo em que o contínuo sacrifício for tirado, e posta a abominação assoladora, serão mil, duzentos e noventa dias.
12 Ana heri mtu yule anayengojea mpaka mwisho wa siku 1, 335.
Bem-aventurado o que espera e chega até mil, trezentos e trinta e cinco dias.
13 Unapaswa uondoke uende njia yako hata mwisho, na kisha utapumzika. Utainuka katika sehemu uliyopewa, mwishoni mwa siku.”
Tu, porém, vai até ao fim; porque repousarás, e te levantarás na tua sorte, no fim dos dias.

< Danieli 12 >