< Danieli 10 >

1 Katika mwaka wa tatu wa Koreshi mfalme wa Uajemi, ujumbe ulifunuliwa kwa Danieli, aliyeitwa pia Belteshaza. Ujumbe huu ulikuwa ni wa kwelil. Ulihusu vita kuu. Danieli aliufahamu ujumbe alipopata ufumbuzi kutoka katika maono.
In the third year of Koresh king of Persia a word was revealed to Daniel, whose name was called Belteshazzar; and the word was true: a great war. And he understood the word, and had understanding of the vision.
2 Katika siku hizo, mimi Danieli, nilikuwa katika maombolezo kwa wiki tatu.
In those days I, Daniel, was mourning for three whole weeks.
3 Sikula chakula kizuri, sikula nyama, sikunywa divai, na sikujipaka mafuta mwenyewe mpaka ukamilifu wa wiki tatu nzima.
I had no pleasing food, neither meat nor wine came into my mouth, neither did I anoint myself at all, until three whole weeks were fulfilled.
4 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza, nilipokuwa niko karibu na mto mkubwa (ambao ni Tigrisi),
In the four and twentieth day of the first month, as I was by the side of the great river, which is the Tigris,
5 Nilitazama juu na nikamwona mtu aliyevaa kitani, akiwa na mkanda kiunoni mwake uliotengenezwa kwa dhahabu safi kutoka Ufazi.
I lifted up my eyes and looked, and look, a man clothed in linen, around his waist a belt made of pure gold from Uphaz.
6 Mwili wake ulikuwa kama kito, na sura yake ilikuwa kama radi. Macho yake yalikuwa kama miali ya tochi, na mikono yake na miguu yake ilikuwa kama shaba iliyosafishwa. Sauti ya maneno yake ilikuwa kama sauti ya umati mkubwa wa watu.
His body was like beryl, and his face like the appearance of lightning, and his eyes like flaming torches, and his arms and his feet like burnished bronze, and the sound of his words like the sound of a multitude.
7 Mimi, Danieli peke yangu niliyaona maono, na watu niliokuwa na pamoja hawakuyaona maono. Lakini, jambo kuu la kuogofya liliwaijia juu yao, na walikimbia na kujificha wao wenyewe.
I, Daniel, alone saw the vision; for the men who were with me did not see the vision; but a great trembling fell on them, and they fled to hide themselves.
8 Hivyo niliachwa peke yangu na niliyaona maono haya ajabu. Hakuna nguvu iliyobakia ndani yangu; mwonekano wangu wa kung'aa ulibadilika na kuwa mwonekano wa uharibifu, na hazikubakia nguvu ndani yangu.
So I was left alone, and saw this great vision, and there remained no strength in me; for my natural appearance grew deathly pale, and I retained no strength.
9 Kisha nikasikia maneno yake, na nilipoyasikia, nilianguka kifudifudi na kupata usingizi mzito.
Yet I heard the sound of his words, and when I heard the sound of his words, then I fell into a deep sleep on my face, with my face toward the ground.
10 Mkono ulinigusa, na ilinifanya nitetemeke katika magoti yangu na viganja vya mikono yangu.
Look, a hand touched me, which set me on my knees and on the palms of my hands.
11 Malaika aliniambia, “Danieli, mtu aliyetunzwa sana, yafahamu maneno ninayokwambia wewe. Simama wima, kwa kuwa nimeshakutuma.” Na alipomaliza kuniambia ujumbe huu, nilisimama nikiwa natetemeka.
He said to me, "Daniel, man greatly loved, understand the words that I speak to you, and stand upright; for I have now been sent to you." And when he had spoken this word to me, I stood trembling.
12 Kisha aliniambia, “Usiogope, Danieli. Tangu siku ya kwanza ulipoiweka akili yako kutaka kufahamu na kujinyenyekeza mwenyewe mbele ya Mungu, maneno yako yalisikiwa, na nimekuja kwasababu ya maneno yako.
Then he said to me, "Do not be afraid, Daniel; for from the first day that you did set your heart to understand, and to humble yourself before your God, your words were heard. And I have come because of your words.
13 Mwana wa mfalme wa ufalme wa Uajemi alinizuia, na niliwekwa huko na mfalme wa Uajemi kwa siku ishirini na moja. Lakini Mikaeli, mmoja kati ya wakuu alikuja kunisaidia.
But the prince of the kingdom of Persia withstood me twenty-one days; but, look, Michael, one of the chief princes, came to help me, because I was left there with the kings of Persia.
14 Sasa nimekuja kukusaidia ili ufahamu kile kitakachotokea kwa watu wako katika siku za mwisho. Kwa kuwa maono ni kwa ajili siku ambazo hazijatokea bado.
Now I have come to make you understand what shall happen to your people in the latter days; for the vision refers to future days."
15 Na alipokuwa akali akiniambia maneno haya, niligeuza uso wangu na kuuelekeza chini na sikuwa na uwezo wa kuzungumza.
And when he had spoken to me according to these words, I turned my face toward the ground, and could not speak.
16 Yeye aliyekuwa kama wana wa mtu alinigusa mdomo wangu na nifumbua kinywa changu na nilimwambia huyo aliyekuwa amesimam mbele yangu: “Bwana wangu, niko katika masumbuko makali kwasababu ya maono; sina nguvu ndani yangu iliyosalia.
And look, something like a man's hand touched my lips. Then I opened my mouth and spoke and said to him who stood before me, "My lord, it is because of the vision anguish has come upon me, and I have no strength.
17 Mimi ni mtumishi wako. Je ninawezaje kuongea na Bwana wangu? Kwa kuwa sasa sina nguvu, na hakuna pumzi iliyosalia ndani yangu.”
For how can this servant of my lord talk with my lord? As for me, no strength remains, and I am breathless."
18 Tena yule mwenye mwonekano wa mtu alinigusa na kunitia nguvu.
Then one like the appearance of a man touched me again and strengthened me.
19 Alisema, “Usiogope, mtu ulithaminiwa sana. Amani na iwe kwako! Uwe mwenye nguvu, uwe na nguvu!” Na alipokuwa anaongea na mimi, nilipata nguvu. Nilimwambia, “Bwana wangu na aseme, kwa kuwa umenitia nguvu.”
And he said, "Greatly loved man, do not be afraid, peace be to you; be strong, be strong." When he spoke to me, I was strengthened, and said, "Let my lord speak, for you have strengthened me."
20 Aliniambia, “Je unajua ni kwanini nimekuja kwako? Nitarudi hivi karibuni kupigana na mkuu wa Uajemi. Na nitakapoenda, mkuu wa Ugiriki atakuja.
Then he said, "Do you know why I have come to you? Now I will return to fight with the prince of Persia. When I go forth, look, the prince of Greece shall come.
21 Lakini nitakwambia kile kilichoandikwa katika Kitabu cha Ukweli. Hakuna yeyote anayejionesha kuwa na nguvu pamoja nami dhidi yao, isipokuwa Mikaeli mkuu wenu.”
But I will tell you that which is inscribed in the Book of Truth. And there is no one who contends with me against them except Michael, your prince."

< Danieli 10 >