< 2 Samweli 17 >

1 Kisha Ahithofeli akamwambia Absalomu, “Niruhusu sasa nichague watu elfu kumi na mbili nami nitaondoka na kumfuatia Daudi usiku huu.
И рече Ахитофел ко Авессалому: изберу ныне себе дванадесять тысящ мужей и востану, и пожену вслед Давида нощию,
2 Nitampata kwa ghafla wakati amechoka na dhaifu nami nitamstukiza kwa hofu. Watu waliopamoja naye watakimbia nami nitamshambulia mfalme peke yake.
и найду на него, и той утружден и ослаблен руками, и устрашу его, и побежат вси людие иже с ним, и убию царя единаго:
3 Nitawarejesha watu wote kwako kama bibi harusi ajavyo kwa bwana wake, na watu wote watakuwa katika amani chini yako.”
и возвращу вся люди к тебе, имже образом обращается невеста к мужеви своему: ты бо токмо души единаго мужа ищеши, всем же людем будет мир.
4 Alichokisema Ahithofeli kikampendeza mfalme na wazee wote wa Israeli.
И угодно слово бысть пред очима Авессаломлима и пред очима всех старейшин Израилевых.
5 Kisha Absalomu akasema, “Sasa mwiteni pia Hushai Mwarki ili tusikie yeye pia anasemavyo.”
И рече Авессалом: призовите же и Хусиа Арахиина, и услышим что из уст его.
6 Hushai alipofika kwa Absalomu, Absalomu akamweleza kile ambacho Ahithofeli alikuwa amesema na kisha akamwuliza Hushai, “Je tufanye alivyosema Ahithofeli? Ikiwa hapana, tueleze kile unachoshauri.”
И вниде Хусий ко Авессалому, и рече Авессалом к нему, глаголя: по глаголу сему глагола Ахитофел: сотворим ли по словеси его? Аще же ни, ты глаголи.
7 Hivyo Hushai akamwambia Absalomu, “Ushauri aliotoa Ahithofeli siyo mzuri kwa wakati huu.”
И рече Хусий ко Авессалому: не благ совет сей, егоже совеща Ахитофел единою сие.
8 Hushai akaongeza, “Unamjua baba yako na kwamba watu wake ni mashujaa na kwa sasa wanauchungu, ni kama dubu aliyenyang'anywa watoto wake mwituni. Baba yako ni mtu wa vita; hatalala na jeshi usiku huu.
И рече Хусий: ты веси отца твоего и мужей его, яко сильни суть зело, и гневливи душами своими, яко медведица чад лишеная на селе, и аки вепрь свирепый на поли: и отец твой муж борец, и не даст почити людем:
9 Tazama, kwa wakati huu pengine amejificha katika shimo fulani au mahali pengine. Itakuwa kwamba baadhi ya watu wako watakapokuwa wameuawa mwanzoni mwa shambulio hata kila mtu atakayesikia atasema, mauaji yamefanyika kwa askari wanaomfuata Absalomu.'
се бо, той ныне скрыся на некоторем холме или на некоторем месте: и будет внегда напасти на них в начале, и услышит слушаяй, и речет: бысть сокрушение в людех иже за Авессаломом:
10 Kisha hata askari jasiri zaidi ambao moyo wao ni kama moyo wa simba, wataogopa kwa kuwa Israeli yote inajua kwamba baba yako ni mtu mwenye nguvu na kwamba watu alionao ni wenye nguvu sana.
и той сын силы, емуже сердце якоже сердце льву таящо истает: понеже весть весь Израиль, яко силен отец твой, и сынове силы вси иже с ним:
11 Hivyo ninashauri kwamba Israeli wote wakutanike kwako pamoja kutoka Dani hadi Beersheba, wengi kama mchanga ufuoni mwa bahari na kwamba wewe mwenyewe uende vitani.
тако советуя аз усоветовах, и собираяся соберется к тебе весь Израиль от Дана и до Вирсавии, аки песок иже при мори во множестве, и лице твое идущее посреде их:
12 Kisha tutampata popote atakapokuwa nasi tutamfunika kama umande uangukavyo juu ya nchi. Hatutamwachia hata mmoja aliye hai kati ya watu wake wala yeye mwenyewe.
и приидем к нему на едино место, идеже обрящем его тамо, и ополчимся на него, якоже спадает роса на землю, и не оставим в нем и в мужех его иже с ним ни единаго:
13 Ikiwa ataingia ndani ya mji kisha Israeli wote tutaleta kamba juu ya mji huo na kuukokotea mtoni, hata kusionekane hata jiwe moja dogo lililosalia.”
и аще во град соберутся, и возмет весь Израиль ко граду тому ужы, и совлечем его в поток, дондеже не останется тамо ниже камень.
14 Kisha Absalomu na watu wa Israeli wakasema, “Shauri la Hushai Mwarki ni jema kuliko lile la Ahithofeli. Yahwe aliwafanya wakatae shauri jema la Ahithofeli ili kumwangamiza Absalomu.
И рече Авессалом и вси мужие Израилтестии: благ совет Хусиа Арахиина паче совета Ахитофелева. И Господь заповеда разорити совет Ахитофелев благий, яко да наведет Господь на Авессалома злая вся.
15 Kisha Hushai akawambia Sadoki na Abiathari makuhani, “Ahithofeli alimshauri Absalomu na wazee wa Israeli hivi na hivi, lakini mimi nimeshauri vinginevyo.
И рече Хусий арахиин ко Садоку и Авиафару иереем: тако и тако советова Ахитофел Авессалому и старейшинам Израилевым: и аз тако и тако советовах:
16 Sasa basi, nendeni haraka na mmtaarifu Daudi kusema, 'Usipige kambi usiku huu katika vivuko vya Araba, lakini kwa namna yoyote vukeni, tofauti na hapo mfalme atamezwa pamoja na watu wote walio pamoja naye.”
и ныне послите скоро и возвестите Давиду, глаголюще: не пребуди нощь сию во Аравофе пустыни, но пойти потщися, да не како пожерт будет царь и вси людие иже с ним.
17 Yonathani na Ahimaasi walikuwako katika chemichemi za En Rogeli. Hivyo kijakazi mmoja alikuwa akienda na kuwapasha habari waliyopaswa kuifahamu, ili kwamba wasihatarishe maisha yao kwa kuonwa wakiingia mjini. Ujumbe ulipofika ndipo huenda na kumtaarifu mfalme Daudi.
И Ионафан и Ахимаас стояста на студенце Рогили, и иде рабыня и поведа има: и тии идоста и возвестиста Давиду царю, яко не могоста явитися еже внити во град.
18 Lakini kijana mmoja akawaoni mara akamwambia Absalomu. Hivyo Yonathani na Ahimaasi wakaenda kwa haraka na wakaingia katika nyumba ya mtu mmoja huko Bahurimu, aliyekuwa na kisima katika ua wake wakaingia humo.
И виде их отрочищь и поведа Авессалому. И идоста оба скоро и приидоста в дом мужа в Ваурим: и тому ров на дворе, и снидоста тамо.
19 Mke wa mtu huyo akachukua kifuniko na kukikufunika kwenye mlango wa kisima kisha akaanika nafaka juu yake, hivyo hakuna aliyejua kwamba Yonathani na Ahimaasi walikuwa kisimani.
И взя жена, и положи покров на устии рова, и суши на нем арафоф, и не познася глагол.
20 Watu wa Absalomu wakaja kwa mwanamke na kumwuliza, “Ahimaasi na Yonathani wako wapi?” Mwanamke akawaambia, “Wamevuka mto.” Hivyo baada ya kuwatafuta bila kuwaona kurejea Yerusalemu.
И приидоша отроцы Авессаломли к жене в дом и реша: где Ахимаас и Ионафан? И рече им жена: преидоста вмале воду. И искаша, и не обретоша, и возвратишася во Иерусалим.
21 Ikawa baada yao kuondoka Yonathani na Ahimaasi wakatoka ndani ya kisima. Wakaenda kumtaarifu mfalme Daudi; wakamwambia, “Inuka na uvuke maji haraka kwa maana Ahithofeli ametoa mashauri haya na haya juu yako.”
Бысть же по отшествии их, и излезоста из рова, и идоста, и возвестиста Давиду царю и глаголаста ему: востаните, и прейдите скоро воду, яко сице совеща на вы Ахитофел.
22 Kisha Daudi akainuka pamoja na watu wote walikuwa pamoja naye, nao wakauvuka Yordani. Hata ilipofika alfajiri hakuna hata mmoja aliyesalia kwa kutouvuka Yordani.
И воста Давид и вси людие иже с ним и преидоша Иордан до света заутра, и ни един не оста, иже бы не прешел Иордана.
23 Ikawa Ahithofeli alipoona kwamba ushauri wake haukufuatwa, akapanda punda wake na kuondoka. Akaenda nyumbani katika mji wake mwenyewe, akaweka mambo yake katika utaratibu na kisha akajinyonga. Kwa hiyo akafa na kuzikwa katika kaburi la baba yake.
И Ахитофел виде, яко не сбыстся совет его, и оседла осля свое, и воста, и отиде в дом свой, во град свой: и заповеда дому своему, и удавися, и умре, и погребен бысть во гробе отца своего.
24 Ndipo Daudi akaja Mahanaimu. Lakini Absalomu yeye akavuka Yordani yeye pamoja na watu wote wa Israeli waliokuwa pamoja naye.
И Давид прейде в Манаим, Авессалом же прейде Иордан сам и вси мужие Израилтестии с ним.
25 Absalomu alikuwa amemweka Amasa juu ya jeshi badala ya Yoabu. Naye huyo Amasa alikuwa mwana wa Yetheri Mwishmaeli, aliyekuwa amelala na Abigaili, aliyekuwa binti Nahashi na dada wa Seruya, mamaye Yoabu.
И Амессая постави Авессалом вместо Иоава над силою: Амессай же сын мужа, емуже имя Иефер Иезраилитин, сей вниде ко Авигеи дщери Иессеине, сестре Саруии матере Иоавли.
26 Kisha Israeli na Absalomu wakapiga kambi katika nchi ya Gileadi.
И ополчися Авессалом и весь Израиль в земли Галаадстей.
27 Ikawa wakati Daudi alipokuwa amekuja Mahanaimu, huyo Shobi mwana wa Nahashi kutoka Raba ya Waamoni na Makiri mwana wa Amieli wa kutoka Lo Debari, na Berzilai Mgileadi wa Rogelimu,
И бысть егда вниде Давид в Манаим, и Уесвий сын Наасов от Раввафа сынов Аммоних, и Махир сын Амииль иже из Лодавара, и Верзеллий Галаадитин из Рогеллима,
28 wakaleta magodoro na mabulangeti, mabakuri na vyungu, na ngano, unga wa shayiri, nafaka zilizokaangwa, maharage, dengu,
принесоша десять постель устроеных и конобов десять и сосуды скуделны и пшеницу и ячмень и муку и пшено и боб и сочевицу
29 asali, siagi, kondoo na samli, ili kwamba Daudi na watu waliokuwa pamoja naye waweze kula. Kwani walisema, “Watu wana njaa, wamechoka na wana kiu huko nyikani.”
и мед и масло и овцы и сыры кравия, и принесоша Давиду и людем иже с ним ясти: быша бо людие гладни и утруждени и жаждни в пустыни.

< 2 Samweli 17 >