< 2 Wafalme 23 >

1 Hivyo mfalme akawatuma wajumbe waliokuwa wamemzunguka wazee wote wa Yuda na wa Yerusalemu.
Then the king sent, —and there were gathered unto him, all the elders of Judah, and Jerusalem;
2 Kisha mfalme akapanda hadi kwenye nyumba ya Yahwe, na watu wote wa Yuda na wenyeji wote wa Yerusalemu pamoja naye, na makuhani, manabii, na watu wote, kuanzia mdogo hadi mkubwa. Kisha akasoma katika masikioni kwao maneno yote ya kitabu cha agano ambalo lililokuwa limepatikana kwenye nyumba ya Yahwe.
and the king went up to the house of Yahweh, and all the men of Judah and all the inhabitants of Jerusalem with him, and the priests, and the prophets, and all the people, both small and great, —and he read in their ears, all the words of the book of the covenant, which had been found in the house of Yahweh.
3 Mfalme akasimama karibu na nguzo na kufanya agano mbele ya Yahwe, kutembea pamoja na Yahwe na kukumbuka maagizo yake, kanuni zake, na sheria zake, kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, kuthibitisha maneno ya hili agano ambalo lililokuwa limeandikwa kwenye hiki kitabu. Hivyo watu wote wakakubaliana kusimama kwenye agano
And the king took his stand by the pillar, and solemnised a covenant before Yahweh—to follow Yahweh, and to keep his commandments and his testimonies and his statutes, with all [their] heart and with all [their] soul, to confirm the words of this covenant, written in this book. And all the people took their stand in the covenant.
4 Mfalme akamwamuru Hilkia yule kuhani mkuu, makuhani chini yake, na walinzi wa lango watoe kwenye hekalu vyombo vilivyokuwa vimetengenezwa kwa ajili ya Baali na Ashera, na kwa ajili ya nyota zote za mbinguni. Akivichoma moto Yerusalimu kwenye mashamba ya bonde la Kidroni na kubeba majivu yake kwenda Betheli.
Then the king commanded Hilkiah the high priest, and the priests of the second order, and the keepers of the entrance-hall, to bring forth, out of the temple of Yahweh, all the vessels that had been made for Baal and for the Sacred Stem, and for all the army of the heavens, —and he burned them up outside Jerusalem, in the fields of Kidron, and carried the ashes of them to Bethel;
5 Akawaondoa makuhani waliokuwa wanaabudu miungu ambao wafalme wa Yuda waliwachagua ili kwa ajili ya kufukiza ubani katika mahali pa juu kwenye miji ya Yuda na sehemu zinazoizunguka Yerusalemu-wale waliokuwa wanchoma ubani kwa Baali, kwa juana kwa mwezi, kwa sayari, na kwa nyota zote za mbinguni.
and he put down the idol-priests, whom the kings of Judah had appointed, so that incense might be burned in the high places, in the cities of Judah, and round about Jerusalem, —them also that burned incense to Baal, to the sun, and to the moon, and to the constellations, and to all the army of the heavens;
6 Akaiondoa Ashera kutoka kwenye hekalu la Yahwe, nje ya Yerusalemu hata bonde la Kidroni na kuichoma hapo. Akaipiga kwenye mavumbi na kuiyatupa yale mavumbi kwenye makaburi ya watu wa kawaida.
and he brought forth the Sacred Stem out of the house of Yahweh, outside Jerusalem, into the Kidron ravine, and burned it in the Kidron ravine, and crushed it to powder, —and cast the powder upon the graves of the sons of the people;
7 Akavisafisha vyumba vya makahaba ambao walikuwa kwenye hekalu la Yahwe, ambako wanawake waliposhonea nguo kwa ajili ya Ashera
and he brake down the houses of the male devotees, which were in the house of Yahweh, —where the women did weave houses to the Sacred Stem;
8 Yosia akawaleta makuhani wote nje ya miji ya Yuda na kupanajisi mahali pa juu ambako makuhani walipokuwa wakichomea ubani, kutoka Geba hata Bersheba. Akapaharibu mahala pa juu kwenye malango ambayo yaliyokuwa ya kuingilia kwenda kwenye lango la Yoshua (liwali wa mji), upande wa kushoto wa lango la mji.
and be brought in all the priests out of the cities of Judah, and defiled the high places where, the priests, had burned incense, from Geba unto Beer-sheba, —and brake down the high places of the gates, that were at the entrance of the gate of Joshua, the governor of the city, which were on one’s left hand, in the gate of the city;
9 Ingawa makuhani wa mahali pa juu hawakuruhusiwa kuhudumu kwenye madhabahu ya Yahwe katika Yerusalemu, wakala mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
howbeit, the priests of the high places came not up unto the altar of Yahweh, in Jerusalem, save only that they did eat unleavened bread in the midst of their brethren;
10 Yosia akainajisi Tofethi, ambayo ipo kwenye bonde la Ben Hinomu, ili kwamba mtu yeyote asimuweke mtoto wake wa kiume au binti yake kwenye moto kama sadaka kwa Molaki.
and he defiled Topheth, which was in the valley of the son of Hinnom, —so that no man might cause his son or his daughter to pass through the fire unto Molech;
11 Akawachukua farasi ambao wafalme wa Yuda waliokuwa wametolewa kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye eneo la lango la uingilia kwenye hekalu la Yahwe, karibu na chumba cha Nathani Meleki, msimamizi mkuu wa nyumba ya mfalme. Yosia akayachoma yale magari ya farasi ya jua
and he did away with the horses, which the kings of Judah had devoted to the sun, at the entrance of the house of Yahweh, near the chamber of Nathan-melech the courtier, which was in the suburbs, also, the chariots of the sun, burned he with fire;
12 Yosia mfalme akayaharibu madhabahu yaliyokuwa kwenye dari ya juu ya chumba cha Ahazi, ambacho wafalme wa Yuda walikitengeneza, na madhabahu ambayo Manase aliyatengeneza kwenye behewa mbili za nyumba ya Yahwe. Yosia akazivunga vipande vipande na kuvitupa kwenye bonde la Kidroni.
and, the altars which were on the roof of the upper chamber of Ahaz, which the kings of Judah had made, also the altars which Manasseh had made, in the two courts of the house of Yahweh, did the king break down, —and hurried away from thence, and cast out the powder of them into the Kidron ravine;
13 Mfalme akapaangamiza mahali pa juu magharibi mwa Yerusalemu, kusini mwa mlima wa uharibifu ambapo Sulemani mfalme wa Israeli alipajenga kwa ajili ya Ashtorithi, chukizo la Wamoabu; sanamu za karaha za Wasidoni; kwa Kemoshi, sanamu za karaha wa Moabu; na kwa Moleki, sanamu wa karaha wa watu wa Amoni.
and, the high places that were before Jerusalem, which were on the right hand of the mount of destruction, which Solomon king of Israel had built unto Ashtoreth—the abomination of the Zidonians, and unto Chemosh—the abomination of the Moabites, and unto Milcom—the disgusting thing of the sons of Ammon, did the king defile;
14 Akazivunja nguzo za jiwe kuwa vipande vipande na kuziangusha chini nguzo za Ashera na kuzijaza zile sehemu kwa mifupa ya watu.
and he brake in pieces the pillars, and cut down the Sacred Stems, —and filled their place with human bones:
15 Yosia pia akaiteketeza kabisa madhabahu iliyokuwa Betheli na mahali pa juu ambako Yeroboamu mwana wa Nebati (ambaye aliwafanya Waisraeli kuasi) aliijenga. Pia aliichoma moto ile madhabahu na mahali pa juu na kupapiga hadi pakawa vumbi. Pia akaichoma moto nguzo ya Ashera.
moreover also, the altar that was in Bethel, the high place which Jeroboam son of Nebat made, wherewith he caused, Israel, to sin, —even that altar, and the high place, brake he down, —and burned the high place, crushing it to powder, and burned a Sacred Stem.
16 Yosia alipotazama kwenye lile eneo, akagundua kwamba yale makaburi yalikuwa juu ya mlima. Akawatuma watu kuichukua mifupa kutoka kwenye yale makaburi; kisha akaichoma kwenye madhabahu, akainajisi. Hii ilitokana na neno la Yahwe ambalo mtu wa Mungu aliliongea, yule mtu aliyekuwa ameongea haya mambo kabla.
And, when Josiah turned, and saw the graves which were there, in the mount, he sent and took the bones out of the graves, and burned upon the altar, and defiled it, —according to the word of Yahweh, which the man of God proclaimed, who proclaimed these things.
17 Kisha akasema, “Ni ukumbusho wa nani ule ninao uona?” Mtu wa ule mji akamwambia, “Lile ni kaburi la mtu wa Mungu ambaye alikuja kutoka Yuda na kuongea kuhusu haya mambo ambayo ameyafanya dhidi ya madhabahu ya Betheli.”
Then said he—What is yonder erection, which I do see? And the men of the city said unto him—The grave of the man of God, who came in out of Judah, and proclaimed these things, which thou hast done, concerning the altar of Bethel.
18 Hivyo Yosia akasema, “Mwacheni. Mtu asihamishe mifupa yake.” Hivyo wakaacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya nabii ambaye alikuja kutoka Samaria.
And he said—Let him rest, let, no man, disturb his bones. So they let his bones rest, with the bones of the prophet who came in out of Samaria.
19 Kisha Yosia akahamisha nyumba zote za mahali pa juu ambazo zilikuwa katika mji wa Samaria, ambazo wafalme wa Israeli walizokuwa wamezitengeneza, na ambazo zilizokuwa zimemgadhabisha Yahwe kwa hasira.
Moreover also, all the houses of the high places which were in the cities of Samaria, which the kings of Israel had made, so as to provoke Yahweh to anger, did Josiah remove, —and he did to them according to all the doings which he had done in Bethel;
20 Aliwafanyia kile ambacho kilikuwa kimefanyika katika Betheli. Aliwachinja makuhani wote wa mahali pa juu ya madhabahu na aliichoma mifupa ya watu juu yao. Kisha akarudi Yerusalemu.
and he sacrificed all the priests of the high places, who were there, by the altars, and burned human bones thereupon, —and returned to Jerusalem.
21 Kisha mfalme akawaamuru watu wote, akisema, “Itunzeni Pasaka ya Yahwe Mungu wenu, kama ilivyoandikwa kwenye hiki kitabu cha agano.”
Then did the king command all the people, saying, Keep ye a passover unto Yahweh, your God, —such as is written in this book of the covenant.
22 Hiyo Pasaka haijawahi kufanyika tangu siku za waamuzi ambao waliiongoza Israeli, wala katika siku zote za wafalme wa Israeli au Yuda.
Surely there had not been held such a passover as this, from the days of the Judges who judged Israel, —nor all the days of the kings of Israel, and the kings of Judah;
23 Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa Mfalme Yosia hii Pasaka ya Yahwe ilisheherekewa katika Yerusalemu.
save only, in the eighteenth year of King Josiah, when this passover was held unto Yahweh, in Jerusalem.
24 Yosia pia akawafukuza wale ambao waliokuwa wameongea na wafu au na roho. Pia aliifukuza miungu ya sananmu, sanamu, na vitu vyote ambavyo ni chukizo vilivyokuwa vinaonekana katika nchi ya Yuda na katika Yerusalemu, hivyo kwa kuthibitisha yale maneno ya sheria ambayo iliyokuwa imeandikwa kwenye kitabu cha Hilkia yule kuhani aliyekuwa amepatikana kwenye nyumba ya Yahwe.
Moreover also, them who had familiar spirits, and the wizards, and the household gods, and the manufactured gods, and the abominations which were to be seen in the land of Judah, and in Jerusalem, did Josiah consume, —that he might confirm the words of the law which were written in the book that Hilkiah the priest had found in the house of Yahweh.
25 Kabla ya Yosia, hapakuwa na mfalme kama yeye, aliyekuwa amemwelekea yahwe kwa moyo wake wote, roho yake yote, na nguvu zake zote, ambaye alifuata sheria zote za Musa. Hapakuwa na mfalme kama Yosia aliyeinuka baada ya yeye.
And, like him, was no king, before him, who turned unto Yahweh with all his heart, and with all his soul, and with all his might, according to all the law of Moses, —neither, after him, arose one, like him.
26 Walakini, Yahwe hakugeuka kutoka kwenye ukali wa hasira yake, ambayo ilikuwa dhidi ya Yuda kwa waabudu wapagani wote pamoja ambao Manase aliokuwa amemgadhibisha.
Howbeit, Yahweh turned not away from the glow of his great anger, wherewith his anger glowed against Judah—because of all the provocations wherewith, Manasseh, had provoked him.
27 Hivyo Yahwe akasema, “Pia nitaiondoa Yuda usoni kwangu, kama nilivyoiondoa Israeli, na nitautupilia mbali huu mji ambao nilio uchagua, Yerusalemu, na ile nyumba ambayo niliyokuwa nimesema, 'Jina langu litakuwa humo.”'
So Yahweh said: Even Judah, will I remove from my presence, as I have removed Israel, —and will reject this city, which I had chosen, even Jerusalem, and the house as to which I had said, My Name, shall be, there.
28 Kama kwa mambo mengine yanayo muhusu Yosia, kila kitu alichofanya, je vimeandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
Now, the rest of the story of Josiah, and all that he did, are, they, not written in the book of the Chronicles of the Kings of Judah?
29 Katika siku zake, Farao Neko, mfalme wa Misri, alienda kupigana dhidi ya mfalme wa Ashuru huko mto Frati. Mfalme Yosia akaenda kuonana na Neco katika mapigano, na Neko akamuua huko Megido.
In his days, came up Pharaoh-necoh king of Egypt, against the king of Assyria, unto the river Euphrates, —and, when King Josiah went against him, he slew him at Megiddo, as soon as he saw him.
30 Watumishi wa Yosia wakambeba kwenye gari la farasi akiwa amekufa kutoka Migido, kumleta Yerusalemu, na kumzika katika kaburi lake mwenyewe. Kisha watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta, na kumfanya kuwa mfalme katika mahali pake.
And his servants conveyed him in a chariot, dead, from Megiddo, and brought him to Jerusalem, and buried him in his own sepulchre, —and the people of the land took Jehoahaz, son of Josiah, and anointed him, and made, him, king, in his father’s stead.
31 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na tatu alipoanza kutawala, na alitawala miezi mitatu katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa akiitwa Hamutali; alikuwa binti wa Yeremia wa Libana.
Twenty-three years old, was Jehoahaz when he began to reign, and, three months, reigned he in Jerusalem, —and, his mother’s name, was Hamutal daughter of Jeremiah, of Libnah.
32 Yehoahazi alifanya yaliyo maovu usoni kwa Yahwe, kama kila kitu ambacho babu zake walichokifanya.
And he did the thing that was wicked in the eyes of Yahweh, according to all that his, fathers, had done.
33 Farao Neko akamfunga gerezani huko Ribla katika nchi ya Hamathi, hivyo asiweze kutawala katika Yerusalemu. Kisha Neko akaitoza Yuda talanta mia moja za fedha na talanta moja ya dhahabu.
And Pharaoh-necoh put him in bonds at Riblah, in the land of Hamath, that he might not reign in Jerusalem, —and he laid a fine upon the land, a hundred talents of silver, and a talent of gold.
34 Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia mfalme katika mahali pa Yosia baba yake, na kubadilisha jina lake kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua mfalme Yehoahazi kwenda Misri, na Yehoahazi akafia huko.
And Pharaoh-necoh made Eliakim son of Josiah king, instead of Josiah his father, and turned his name to Jehoiakim, —and, Jehoahaz, took he away, so he entered Egypt, and died there.
35 Yehoyakimu akalipa fedha na dhahabu kwa Farao. Ili akutane na amri ya Farao, Yehoyakimu akaitoza nchi na kulazimisha kila mtu miongoni mwa watu wa nchi wamlipe fedha na dhahabu kulingana na makadirio yao.
And, the silver and the gold, did Jehoiakim give unto Pharaoh, howbeit he assessed the land, that he might give the silver at the bidding of Pharaoh, —every man, according to his assessment, exacted the silver and the gold of the people of the land, that he might give it to Pharaoh-necoh.
36 Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na tano alipoanza kutawala, na alitawala miaka kumi na moja katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa akiitwa Zebida; alikuwa binti wa Pedaia wa Ruma.
Twenty-five years old, was Jehoiakim when he began to reign, and, eleven years, reigned he in Jerusalem, —and, his mother’s name, was Zebudah daughter of Pedaiah, of Rumah.
37 Yehoyakimu akafanya yale yaliyo maovu usoni kwa Yahwe, kama waliyoyafanya babu zake.
And he did the thing that was wicked in the eyes of Yahweh, —according to all that, his fathers, had done.

< 2 Wafalme 23 >