< 2 Wafalme 20 >

1 Katika siku hizo Hezekia aliugua akawa kwenye hatari ya kufa. Hivyo Isaya mwana wa Amozi, akaja, na kumwambia, “Yahwe asema, 'Weka nyumba yako kwenye mpangilio; kwa kuwa utakufa, na hutapona.'”
In those days was Hezekiah sick unto death. And Isaiah the prophet the son of Amoz came to him, and said unto him: 'Thus saith the LORD: Set thy house in order; for thou shalt die, and not live.'
2 Kisha Ahazi akageuza uso wake kwenye ukuta na kumuomba Yahwe, akisema,
Then he turned his face to the wall, and prayed unto the LORD, saying:
3 “Tafadhali, Yahwe, ukumbuke jinsi nilivyo mwaminifu kutembea mbele yako kwa moyo wangu wote, na jinsi nilivyofanya yaliyo mazuri usoni kwako.” Kisha Hezekia akalia kwa sauti.
'Remember now, O LORD, I beseech Thee, how I have walked before Thee in truth and with a whole heart, and have done that which is good in Thy sight.' And Hezekiah wept sore.
4 Kabla ya Isaya hajatoka nje kwenye mji wa kati, neno la Yahwe likamjia, kusema,
And it came to pass, before Isaiah was gone out of the inner court of the city, that the word of the LORD came to him, saying:
5 '“Rudi, na umwambie Hezekia, kiongozi wa watu wangu, 'Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Daudi babu yako, asemavyo: “Nimesikia maombi yako, na nimeyaona machozi yako. Nitakuponya katika siku ya tatu, na utapanda juu kwenye nyumba ya Yahwe.
'Return, and say to Hezekiah the prince of My people: Thus saith the LORD, the God of David thy father: I have heard thy prayer, I have seen thy tears; behold, I will heal thee; on the third day thou shalt go up unto the house of the LORD.
6 Nitakuongeza miaka kumi na tano ya maisha yako, na nitakulinda na huu mji kwa ajili yangu na kwa ajili ya mtumishi wangu."”'
And I will add unto thy days fifteen years; and I will deliver thee and this city out of the hand of the king of Assyria; and I will defend this city for Mine own sake, and for My servant David's sake.'
7 Hivyo Isaya akasema, “Chukueni mkate wa tini.” Walifanya hivyo na kuweka kwenye jipu lake, na akapona.
And Isaiah said: 'Take a cake of figs.' And they took and laid it on the boil, and he recovered.
8 Hezekia akamwambia Isaya, “Je kutakuwa na alama gani ambayo Yahwe ataniponya, na kwamba nitapanda juu hadi kwenye hekalu la Yahwe katika siku ya tatu?”
And Hezekiah said unto Isaiah: 'What shall be the sign that the LORD will heal me, and that I shall go up unto the house of the LORD the third day?'
9 Isaya akajibu, “Hii ndiyo itakuwa ishara kwako kutoka kwa Yahwe, kwamba Yahwe atafanya kitu amacho alichokisema. Je kivuli kitaenda mbele hatua saba, au kurudi nyuma hatua saba?”
And Isaiah said: 'This shall be the sign unto thee from the LORD, that the LORD will do the thing that He hath spoken: shall the shadow go forward ten degrees, or go back ten degrees?
10 Hezekia akajibu, “Ni kitu chepesi kwa kivuli kwenda mbele hatua kumi. Hapana, hicho kivuli kirudi nyuma hatua kumi.”
And Hezekiah answered: 'It is a light thing for the shadow to decline ten degrees; nay, but let the shadow return backward ten degrees.'
11 Hivyo Isaya nabii akamlilia Yahwe, na akaleta kivuli hatua kumi nyuma, kutoka pale ambapo zilikuwa zimevuka kwenye ngazi za Ahazi.
And Isaiah the prophet cried unto the LORD; and he brought the shadow ten degrees backward, by which it had gone down on the dial of Ahaz.
12 Katika kipindi hicho Merodak Baladani mfalme wa Babeli alituma barua na zawadi kwa Hezekia, kwa kuwa alisikia kwamba Hezekia alikuwa anaumwa.
At that time Berodach-baladan the son of Baladan, king of Babylon, sent a letter and a present unto Hezekiah; for he had heard that Hezekiah had been sick.
13 Hezekia akasikiliza hizo barua, na kisha kuwaonyesha wajumbe sehemu zote na sehemu zake za thamani, fedha, dhahabu, manukato na marhamu na nyumba yenye ghala la silaha zake, na yote yaliyokutwa kwenye ghala za nyumba zake. Hapakuwa na kitu kwenye nyumba, wala kwenye ufalme wake wote, ambao Hezekia hakuwaonyesha.
And Hezekiah hearkened unto them, and showed them all his treasure-house, the silver, and the gold, and the spices, and the precious oil, and the house of his armour, and all that was found in his treasures; there was nothing in his house, nor in all his dominion, that Hezekiah showed them not.
14 Kisha Isaya akaja kwa Hezekia na kumuuliza, “Hawa watu walikuwa wanakwambiaje? Wanatokea wapi?” Hezekia aksema, “Wamekuja kutoka nchi ya mbali ya Babeli.
Then came Isaiah the prophet unto king Hezekiah, and said unto him: 'What said these men? and from whence came they unto thee?' And Hezekiah said: 'They are come from a far country, even from Babylon.'
15 Isaya akauliza, “Wameona nini kwenye nyumba yako?” Hezekia akajibu, “Wameona kila kitu kwenye nyumba yangu. Hakuna kitu miongoni mwa vitu vyangu vya thamani ambavyo sijawaonyesha.”
And he said: 'What have they seen in thy house?' And Hezekiah answered: 'All that is in my house have they seen; there is nothing among my treasures that I have not shown them.'
16 Basi Isaya akamwambia Hezekia, “Sikiliza neno la Yahwe:
And Isaiah said unto Hezekiah: 'Hear the word of the LORD.
17 'Tazama siku zinakuja wakati kila kitu kwenye kwenye nyumba yako ya kifalme, vitu ambavyo babu zako walivitunza huko hadi leo, vitabebwa kwenda Babeli. Hakuna kitakachobakia, Yahwe asema.
Behold, the days come, that all that is in thy house, and that which thy fathers have laid up in store unto this day, shall be carried to Babylon; nothing shall be left, saith the LORD.
18 Watoto waliozaliwa na wewe, ambao umewazaa wewe mwenyewe-watawachukua mbali, na watakuwa matowashi kwenye nyumba ya kifalme ya mfalme wa Babeli.'”
And of thy sons that shall issue from thee, whom thou shalt beget, shall they take away; and they shall be officers in the palace of the king of Babylon.'
19 Hezekia akamwambia Isaya, “neno la Yahwe uliloliongea ni jema.” Kwa kuwa alifikiri, Je sivyo ikiwapo amani na kweli katika siku zangu?”
Then said Hezekiah unto Isaiah: 'Good is the word of the LORD which thou hast spoken.' He said moreover: 'Is it not so, if peace and truth shall be in my days?'
20 Kama kwa mambo mengine yanamuhusu Hezekia, na ushujaa wake wote, na jinsi alivyotengeza bwawa la maji na mfereji, na kuleta maji kwenye mji-hayakuandikwa kwenye kitabu cha ya matukio ya wafalme wa Yuda?
Now the rest of the acts of Hezekiah, and all his might, and how he made the pool, and the conduit, and brought water into the city, are they not written in the book of the chronicles of the kings of Judah?
21 Hezekia akalala na babu zake, na Manase mwanae akawa mfalme katika sehemu yake.
And Hezekiah slept with his fathers; and Manasseh his son reigned in his stead.

< 2 Wafalme 20 >