< 2 Nyakati 9 >

1 Malikia wa Sheba aliposikia kuhusu umaarufu wa Selemani, akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Akaja pamoja na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliosheheni manukato, dhahabu nyingi, na vito vingi vya thamani. Alipofika kwa
Царица же Савска услыша имя Соломоново и прииде искусити его гаданьми во Иерусалиме с силою тяжкою зело: и велблюды носящии ароматы и злата множество и камения драгаго: и прииде к Соломону и глагола ему вся, елика беша в сердцы ея.
2 Selemani, akamwambia yaliyokuwa moyoni mwake. Selemani akamjibu maswaali yake yote; hakuna kitu kilichokuwa kigumu sana kwa Selemani; hakuna swali ambalo hakulijibu.
И возвести ей Соломон вся словеса ея, и не прейде слово, егоже бы не возвестил ей.
3 Malikia wa Sheba alipoiona hekima ya Selemani na ikulu aliyokuwa amejenga,
И виде царица Савска премудрость Соломоню, и дом егоже созда,
4 chakula mezani kwake, mahali pa kukaa watumishi wake, kazi ya watumisshi wake na mavazi yao, pia wabebakikombe na mavazi yao, na namna alivyotoa sadaka za kuteketezwa katika nyumba ya Yahwe, hapakuwa na roho zaidi ndani yake.
и яди столов его, и седалища рабов его, и состояние служебников его и ризы их, и виночерпчия его и украшение их, и всесожжения, яже жряше в дому Господни, и вне себе бысть.
5 Akasema kwa mfalme, “Ni kweli, taarifa ninioisikia katika nchi yangu kuhusu maneno yako na hekima yako.
Рече же ко царю: истинно есть слово, еже слышах в земли моей о словесех твоих и о премудрости твоей:
6 Sikuamini nilichokisika mpaka nilipokuja hapa, na sasa macho yangu yamekiona. Sikuambiwa nusu kuhusu hekima yako na utajiri wako! Umeuzidi umaarufu niliokuwa nimesikia kuhusu wewe.
и не веровах словесем их, дондеже приидох, и видеста очи мои, и се, не возвестиша мне половины множества премудрости твоея: приложил еси ко слышанию яже слышах:
7 Wamebarikiwa watu wako, na watumishi wako ambao husimama mbele yako, kwa sababu wanaisikia hekima yako. (Baadhi ya maandiko yanasema, “Wambarikiwa wake zako”, ikidhaniwa kwamba kifungu hicho kinapaswa kusomeka kama ilivyo katika Wafalme 10: 8).
блажени мужие твои и блажени раби твои сии, иже предстоят пред тобою на всяко время и слышат премудрость твою:
8 Amebarikiwa Yahwe Mungu wako, ambaye amepata raha ndani yako, aliyekuweka juu ya kiti chake cha enzi, ili uwe mfalme kwa ajili ya Yahwe Mungu wako. Kwa sababu Mungu wako inaipenda Israeli, ili kuwathibisha milele, amekufanya kuwa mfalme juu yao, ili ufanye hukumu na haki.
да будет Господь Бог твой благословен, иже благоволи в тебе, еже дати тя на престол Свой царя Господу Богу твоему: зане возлюби Господь Бог твой Израиля, еже утвердити его во век, и постави тя над ними царя, да сотвориши суд и правду.
9 Akampa mfalme talanta 120 za dhahabu na kiasi kikubwa manukato na vit vya thamani. Selemani hakupewa tena kiasi kikubwa cha manukato kama hiki amabacho alipewa na malakia wa Sheba.
Даде же царю сто двадесять талант злата и ароматы многи зело и камение драгое, и не быша ароматы таковы яко сия, яже даде царица Савска царю Соломону.
10 Watumishi wa Hiramau na wa mfalme Selemani, ambaye alileta dhahabu kutoka Ofiri, miti ya msandali, na vito vya thamani.
Но и раби Хирамовы с рабы Соломоними приношаху злато Соломону драгое.
11 Kwa miti hiyo ya msandali, mfalme Selemani akatengeneza madari ya nyumba ya Yahwe na nyumba yake, na vinubi na vinanda kwa ajili ya wanamziki. Hapajaonekana tena mbao kama hiyo katika nchi ya Yuda.
И сотвори Соломон царь от древ певговых степени в дом Господень и в дом царев, и гусли и псалтири песней, и никогдаже видена быша в земли Иудине прежде такоая.
12 Mfalme Selemani akampa malkia wa Sheba kila kitu alichotaka, chochote alichoomba, zaidi ya vile alivyoleta kwa mfalme Selemani. Kwa hiyo akaondoka na kurudi kwenye nchi yake, yeye na wataumishsi wake.
Царь же Соломон даде царице Савстей вся по желанию ея, ихже просила, кроме всех яже принесе царю Соломону, и возвратися в землю свою.
13 Sasa uzito wa dhahabu ambayo ililetwa kwa Selemani ndani ya mwaka mmoja ulikuwa talanta 666 za dhahabu,
Бе же вес злата приносимаго к Соломону на всяко лето шесть сот шестьдесят шесть талант злата,
14 nje na dhahabu ambayo waliileta wachukuzi na wafanya biashara. Walme wote wa Arabuni na maliwali katika nchi pia wakamletea Selemanai dhahabu na fedha.
кроме мужей подданных и купцов, иже приношаху, и всех царей Аравских и властелей земли, иже вси приношаху злато и сребро царю Соломону.
15 Mfalme Selemani akatengeneza ngao kubwa mia mbili za dhahabu iliyofuliwa. Shekeli mia sita za dhahabu zikatumika kwa kila ngao.
Сотвори убо царь Соломон двести щитов златых тягненых, шесть сот златник чистых бяху во единем щите:
16 Pia akatengeneza ngao mia tatu za shahabu iliyopigwa. Minas tatu za dhahabu zikaenda kwa kila ngao; mfalme akaziweka kwenye ikulu ya Msitu wa Lebanoni.
и триста щитов златых тягненых, по триста златник бяше во единем коемждо щите, и положи я царь в дому древа Ливанова.
17 Kisha mfalme atengeneza kiti cha enzi kikubwa cha pembe na kufunika kwa dhahabu safi.
Сотвори же царь престол от слоновых зубов велик, и позлати его златом чистым,
18 Kulikuwa na ngazi sita kwenda kwenye kiti cha enzi, na sehemu ya juu ya kiti cha enzi ilikuwa duara. Kulikuwa na mikono kila upande wa kiti, na simba wawili wamesimama pembeni na hiyo mikono.
и шесть степений у престола позлащени златом, и мышчицы две туду и сюду над престолом седалища, и два льва стояща близ мышчцей,
19 Simba kumi na wawili walisimama juu ya zile ngazi, mmoja kila upande wa ngazi sita.
и дванадесять львов стоящих тамо на шести степенех от обоих стран: и не бысть таков престол во всяцем царстве.
20 Hapakuwa na kiti cha enzi kama hicho katika ufalme wowote mwingine. Vikombe vyote vya kunywea vya Selemani vilikuwa vya dhahabu, na vikombe vyote vya mfalme katika Nyumba ya Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu halisi. Hakuna hata kimoja kilichokuwa cha fedha kwa sababu fedha haikuchuliwa kuwa ya thamani katika siku za Selemani.
Вси же сосуди царя Соломона бяху златы, и вси сосуди дому дубравы Ливанския златом окружены, сребро бо во днех Соломоних ни во что вменяшеся:
21 Mfalme alikuwa na meli zilizosafiri baharini, pamoja na meli za Hiramu. Mara moja kwa mwaka meli zilileta dhahabu, fedha, na pembe, na manukato, na pia nyani na tausi.
зане корабль царев хождаше в Фарсис с рабы Хирамовыми, единицею в лета три прихождаше корабль от Фарсиса ко царю, полн злата и сребра и зубов слоновых и обезян.
22 Kwa hiyo Mfalme Selemani aliawazidi utajiri na hekima wafalme wote wa dunia.
И возвеличися Соломон паче всех царей земных богатством и мудростию.
23 Dunia yote waliutafuta uwepo wa Selemanai ili kusikia hekima yake, ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
Вси же царие земстии желаху видети лице Соломоне и слышати премудрость его, юже даде Бог в сердце его:
24 Waliomtembelea walileta kodi, vyombo vya shaba na dhahabu, nguo, silaha, na manukato, na farasi na anyumbu, mwaka baada ya mwaka.
и приношаху ему кийждо дары своя, сосуды сребряны и златы, и одеяния и стакту, и сладости, кони и мски, на всякое лето.
25 Selemani alikuwa na mazizi elfu nne kwa ajili ya farasi na magari, na wapanda farasi kumi na mbili elfu, ambao waliwaweka katika miji ya magari na pamoja naye katika Yerusalemu.
И бяху царю Соломону четыредесять тысящ кобылиц к колесницы и дванадесять тысящ конник, и постави их во градех колесничных и со царем во Иерусалиме.
26 Akatawala juu ya wafalme wote kutoka mto Efrati hadi nchi ya Wafilisti, na hadi mpaka wa Misiri.
И быть вождь всех царей от реки (Евфрата) даже до земли иноплеменник и даже до предел Египетских.
27 Mfalme alikuwa na fedha katika Yerusalemu, nyingi kama mawe juu ya aridhi. Akazifanya mbao za mierezi kuwa nyingi kama miti ya mikuyu ambayo iko nyanda za chini.
И даде царь злато и сребро во Иерусалиме яко камение, и кедры яко черничие, еже (раждается) в полях множество.
28 Wakaleta farasi kutoka Misri na kutoka nchi zote kwa ajili ya Selemani.
И приводяху кони Соломону от Египта и от всея земли.
29 Kwa mambo mengine kuhusu Selemani, mwanzo na mwisho, hayajandikwa katika Historia ya Nathani Nabii, katika unabii wa Abiya Mshinoni, na katika Maono ya Ido mwonaji wa mambo ya Yeroboamu mwana wa Nabati?
И прочая словеса Соломоня первая и последняя, се, сия писана суть в словесех Нафана пророка и в словесех Ахии Силониты и в видениих Иоиля видящаго, противу Иеровоама сына Наватова.
30 Selemani akatawala katika Yerusalemu juu ya Israeli yote kwa miaka arobaini.
И царствова Соломон во Иерусалиме над всем Израилем четыредесять лет.
31 Akalala na babu zake na watu wakamzika katika mji wa Daudi baba yake. Rehoboamu, mwanaye, akawa mfalme katika sehemu yake.
И успе Соломон со отцы своими, и погребоша его во граде Давида отца его. И воцарися Ровоам сын его вместо его.

< 2 Nyakati 9 >