< 2 Nyakati 1 >

1 Selemani mwana wa Daudi, aliimariswa katika utawala wake, na Yahwe Mungu wake alikuwa pamoja naye na alimpa nguvu nyingi sana.
AND SOLOMON the son of David was strengthened in his kingdom, and the LORD his God was with him, and magnified him exceedingly.
2 Sulemani akasema kwa Israleli wote, na maakida wa maelfu na wa mamia, na kwa waamuzi, na kwa kila mfalme kiongozi katika Israeli yote, wakuu wa kaya.
And Solomon spoke unto all Israel, to the captains of thousands and of hundreds, and to the judges, and to every prince in all Israel, the heads of the fathers' houses.
3 Hivyo Sulemani na kusanyiko lote wakaenda pamoja naye sehemu ya juu iliyokuwa Gibeoni, maana ndipo palikuwepo hema ya kukutania ya Mungu, ambayo Musa mtumishi wa Yahwe, alikuwa ameitengeneza jangwani.
So Solomon, and all the congregation with him, went to the high place that was at Gibeon; for there was the tent of meeting of God, which Moses the servant of the LORD had made in the wilderness.
4 Lakini Daudi alikuwa ameleta pale sanduku la Mungu kutoka Kiriath yeriam hadi sehemu ambayo alikuwa ametayarisha, maana alikuwa ameliandalia hema huko katika Yerusalemu.
But the ark of God had David brought up from Kiriath-jearim to the place that David had prepared for it; for he had pitched a tent for it at Jerusalem.
5 Zaidi ya hayo, madhabahu ya shaba iliyotengenezwa na Bezaleli mwana wa uri mwana wa Huri ilikuwepo huko kabla ya mbele ya madhabahu ya Yahwe; Sulemani na kusanyiko wakaenda ilikokuwa. (Maandiko ya zamani yanasema
Moreover the brazen altar, that Bezalel the son of Uri, the son of Hur, had made, had been put before the tabernacle of the LORD; and Solomon and the congregation sought unto it.
6 Selemani akaenda huko kwenye kwenye madhabahu ya shaba mbele za Yahwe, ambayo ilikuwepo mahali pa hema ya kukutamia, na akatoa sadaka elfu za kuteketezwa juu yake.
And Solomon offered there, upon the brazen altar before the LORD, which was at the tent of meeting, he offered a thousand burnt-offerings upon it.
7 Mungu akamtokea Selemani usiku huo na akasema kwake, “Omba! Nikupe nini?”
In that night did God appear unto Solomon, and said unto him: 'Ask what I shall give thee.'
8 Selemani akasema kwa Mungu, “Umeonesha agano la uaminifu mkuu kwa Daudi baba yangu, na umenifanya mfalme katika nafasi yaye.
And Solomon said unto God: 'Thou hast shown great kindness unto David my father, and hast made me king in his stead.
9 Sasa, Yahwe Mungu, ahadi yako kwa Daudi baba yangu itimie, maana umenifanya mfalme juu ya watu wengi kama mavumbi ya dunia.
Now, O LORD God, let Thy promise unto David my father be established; for Thou hast made me king over a people like the dust of the earth in multitude.
10 Sasa nipe hekima na maarifa, ili niweze kuwaongoza watu hawa, maana ni nani anayeweza kuwaamua watu wako, ambao ni wengi sana kwa idadi?”
Give me now wisdom and knowledge, that I may go out and come in before this people; for who can judge this Thy people, that is so great?'
11 Mungu akasema kwa Selemani, “Kwa kuwa hili lilikuwa kwenye moyo wako, na kwa kuwa hujaomba mali, utajiri, au heshima, wala maisha ya wale wanaokuchukia, wala maish marefu kwa jili yako binafsi, lakini umeomba hekima na maarifa kwa ajili yako, ili uwatawale watu wangu, ambao juu yao nimekufanya mfame, na hivi ndivyo nitafanya.
And God said to Solomon: 'Because this was in thy heart, and thou hast not asked riches, wealth, or honour, nor the life of them that hate thee, neither yet hast asked long life, but hast asked wisdom and knowledge for thyself, that thou mayest judge My people, over whom I have made thee king;
12 Sasa nitakupa hekima na maarifa, pia nitakupa mali na utajiri, na heshima, kuliko wafalme wote waliokuwepo kabla yako walivyokuwa, na baada yako hakuna yeyote atakayekuwa navyo.”
wisdom and knowledge is granted unto thee, and I will give thee riches, and wealth, and honour, such as none of the kings have had that have been before thee, neither shall there any after thee have the like.'
13 Kwa hiyo Selemani akaenda Yerusalemu kutoka sehemu ya juu iliyokuwepo Gibeoni, kutoka mbele ya hema ya kukutania; akatawala juu ya Israeli.
So Solomon came from his journey to the high place that was at Gibeon, from before the tent of meeting, unto Jerusalem; and he reigned over Israel.
14 Selemani akakusanya magari na wanaume waendesha farasi, naye alikuwa na magari 1, 400 na waendesha farasi kumi na mbili elfu ambao aliwaweka katika miji ya magari, pamoja naye, mfalme katika Yerusalemu.
And Solomon gathered chariots and horsemen; and he had a thousand and four hundred chariots, and twelve thousand horsemen, that he placed in the chariot cities, and with the king at Jerusalem.
15 Mfalme akatengeneza fedha na dhahabu kuwa vitu vya kawaida kama mawe katika Yerusalemu, na mbao za mierezi kuwa kama miti ya mikuyu iliyomo katika nyanda za chini.
And the king made silver and gold to be in Jerusalem as stones, and cedars made he to be as the sycamore-trees that are in the Lowland, for abundance.
16 Selemani katika uagizaji wa farasi kutoka Misiri, wafanya biashara wake walinunua farasi kutoka Misiri kwa bei stahiki.
And the horses which Solomon had were brought out of Egypt; also out of Keve, the king's merchants buying them of the men of Keve at a price.
17 Waliagiza gari kutoka Misiri kwa shekeli mia sita za fedha, na farasi mmoja kwa shekeli 150. Pia walinunua kutoka kwa wafalme wa Wahiti na wafalme wa Washamu.
And they fetched up, and brought out of Egypt a chariot for six hundred shekels of silver, and a horse for a hundred and fifty; and so for all the kings of the Hittites, and the kings of Aram, did they bring them out by their means.

< 2 Nyakati 1 >