< 1 Samweli 29 >

1 Basi Wafilisti walikusanya pamoja majeshi yao yote huko Afeki; Waisraeli wakapiga kambi karibu na chemchemi iliyoko Yezreeli.
Now the Philistines gathered together all their hosts, towards Aphek, —and, the Israelites, were encamping by the fountain, that is in Jezreel.
2 Nao wakuu wa Wafilisti wakapitwa na mamia kwa maelfu; Daudi na watu wake wakapita wakiwa wa mwisho pamoja na Akishi.
And, the lords of the Philistines, were passing on by hundreds, and by thousands, —but, David and his men, were passing on in the rear, with Achish.
3 Kisha wakuu wa Wafilisti wakasema, “Hawa Waebrania wanafanya nini hapa?” Akishi akawaambia wakuu wengine wa Wafilisti, “Huyu si Daudi, mtumishi wa Sauli, mfalme wa Israeli, ambaye amekaa nami kwa siku hizi, au kwa miaka hii, nami nimeona hana kosa tangu aje kwangu hadi leo?”
Then said the princes of the Philistines, What are these Hebrews [doing]? And Achish said unto the princes of the Philistines—Is not this David, servant of Saul king of Israel, who hath been with me this year, or two, and I have found in him nothing, from the day of his coming over unto me unto this day?
4 Lakini wale wakuu wa Wafilisti walimkasirikia Akishi; wakamwabia, Mfukuze mtu huyo, aende kwake kule ulikompatia; usimruhusu aende nasi vitani, ili asiwe adui yetu katika vita. Kwa jinsi gani mtu huyu angeweza kufanya amani na bwana wake? Siyo kwa gharama ya vichwa vya watu wetu?
But the princes of the Philistines raged against him, and the princes of the Philistines said unto him—Let the man go back, that he may return unto the place which thou didst appoint him, and let him not go down with us, into battle, so shall he not become to us a traitor, in the battle, —for, wherewith, should this fellow gain favour with his lord? Would it not be with the heads of those men?
5 Je, huyu siye Daudi ambaye walimuimba kwa kupokezana na kucheza, wakisema: 'Sauli ameua maelfu yake, Na Daudi makumi elfu yake?”'
Is not this David, of whom they made responses in the dances, saying, —Saul, hath smitten, his thousands, But, David, his, tens of thousands?
6 Ndipo Akishi alimwita Daudi na kumwambia, “Kama BWANA aishivyo, umekuwa mwema, na kutoka kwako na kuingia kwako pamoja nami katika jeshi ni kwema kama nionavyo mimi; maana sijaona kosa kwako tangu siku unakuja kwangu hadi siku hii ya leo. Hata hivyo, wakuu hawakupendi.
So Achish called for David, and said unto him—By the life of Yahweh, surely, upright, thou art, and, pleasing in mine eyes, have been thy going out and thy coming in with me, in the host, for I have found in thee no wrong, from the day of thy coming in unto me, until this day, —but, in the eyes of the lords, displeasing, thou art.
7 Basi sasa rudi na uende kwa amani, ili usiwakwaze wakuu wa Wafilisti.”
Now, therefore, return, and go in peace, —so shalt thou not do wrong in the eyes of the lords of the Philistines.
8 Daudi akamwambia Akishi, “Lakini nimefanya nini? Kitu gani umekiona kwa mtumishi wako kwa muda ambao nimekuwa mbele yako hadi leo, kiasi kwamba nisiende kupigana na adui za bwana wangu mfalme?”
Then said David unto Achish—But what have I done? and what hast thou found in thy servant, from the day that I came before thee, unto this day, —that I may not go in and fight, with the enemies of my lord the king.
9 Akishi akajibu na kumwambia Daudi, “Najua kwamba hauna lawama mbele zangu kama alivyo malaika wa Mungu; hata hivyo, wale wakuu wa Wafilisti wamesema, Kamwe hatapanda pamoja nasi hadi vitani.'
Then answered Achish, and said unto David, I acknowledge that, pleasing, thou art in mine eyes, as a messenger of God, —notwithstanding, the princes of the Philistines, have said, He shall not go up with us, into the battle.
10 Basi sasa amka asubuhi na mapema na watumishi wa bwana wako waliokuja pamoja nawe; mara tu muamkapo asubuhi na mapema na kupata mwanga, ondokeni.”
Now, therefore, rise up early in the morning, thou and the servants of thy lord who have come with thee, —yea, as soon as ye have risen early in the morning, and have light, then depart.
11 Hivyo Daudi aliamka mapema, yeye pamoja na watu wake, waondoke asubuhi, warudi kule katika nchi ya Wafilisti. Lakini Wafilisti walipanda kwenda Yezreeli.
So David rose up early, he and his men, to depart in the morning, to return into the land of the Philistines, —but, the Philistines, went up to Jezreel.

< 1 Samweli 29 >