< 1 Samweli 28 >

1 Ikawa katika siku hizo Wafilisti walikusanya majeshi yao pamoja kwa ajili ya vita, wapigane na Israeli. Akishi akamwambia Daudi, “Ujue kwa hakika kwamba utakwenda nami ndani ya jeshi, wewe na watu wako.”
Now it happened that, in those days, the Philistines gathered together their troops, so that they might be prepared for war against Israel. And Achish said to David, “I know now, certainly, that you will go out with me to war, you and your men.”
2 Naye Daudi akamwambia Akishi, “Sasa utajua kile ambacho mtumishi wako anaweza kufanya.” Akishi akamwambia Daudi, “Basi sasa, nitakufanya uwe mlinzi wangu binafsi daima.”
And David said to Achish, “You know now what your servant will do.” And Achish said to David, “And so, I will appoint you to guard my head for all days.”
3 Samweli alikuwa amefariki; Waisraeli wote walimwomboleza na kumzika huko Rama, katika mji wake mwenyewe. Wakati huo Sauli alikuwa amewafukuza kutoka nchini wote walioongea na wafu au pepo.
Now Samuel was dead, and all of Israel mourned for him, and they buried him in Ramah, his city. And Saul took away the magi and soothsayers from the land.
4 Wafilisti walijikusanya wao wenyewe wakaja na kuweka kambi huko Shunemu; na Sauli akawakusanya Israeli wote pamoja, na wakaweka kambi yao huko Gilboa.
And the Philistines gathered together, and they arrived and made camp at Shunem. Then Saul also gathered all of Israel, and he arrived at Gilboa.
5 Sauli alipoona jeshi la Wafilisti, aliogopa na moyo wake ukatetemeka sana.
And Saul saw the camp of the Philistines, and he was afraid, and his heart was exceedingly terrified.
6 Sauli alipomuomba BWANA kwa ajili ya msaada, BWANA hakumjibu - si kwa ndoto wala kwa Urimu, wala kwa manabii.
And he consulted the Lord. But he did not respond to him, neither by dreams, nor by priests, nor by prophets.
7 Ndipo Sauli akawaambia watumishi wake, “Mnitafutie mwanamke ambaye anaweza kuongea na wafu, ili ni mwendee na kutafuta msaada wake.” Watumishi wake wakamwambia, “Tazama, yupo mwanamke huko Endori awezaye kuongea na wafu.”
And Saul said to his servants, “Seek for me a woman having a divining spirit, and I will go to her, and consult through her.” And his servants said to him, “There is a woman having a divining spirit at Endor.”
8 Basi Sauli akajigeuza, akavaa nguo nyingine tofauti, akaondoka yeye pamoja na watu wawili; wakamwendea yule mwanamke wakati wa usiku. Akasema, “Nitabirie, nakuomba, kwa kuongea na wafu, na uniinulie yule nitakayekutajia.”
Therefore, he changed his usual appearance, and he put on other clothes. And he went, and two men with him, and they came to the woman by night. And he said to her, “Divine for me, by your divining spirit, and raise up for me whomever I will tell you.”
9 Yule mwanamke akamwambia, “Tazama, unajua alichofanya Sauli, jinsi alivyowafukuza kutoka katika nchi wanaoongea na wafu au mizimu. Basi kwa nini mnatega mtego kwa ajili ya uhai wangu, ili kuniua?”
And the woman said to him: “Behold, you know how much Saul has done, and how he has wiped away the magi and soothsayers from the land. Why then do you set a trap for my life, so that it will be put to death?”
10 Sauli akamwapia kwa BWANA na kusema, “Kama BWANA aishivyo, hakuna adhabu utakayopata kutokana na jambo hili.”
And Saul swore to her by the Lord, saying, “As the Lord lives, nothing evil will befall you because of this matter.”
11 Kisha yule mwanamke akasema, “Je, nikuinulie nani?” Sauli akasema, “Niinulie Samweli.”
And the woman said to him, “Whom shall I raise up for you?” And he said, “Raise up for me Samuel.”
12 Yule mwanamke alipomwona Samweli, akalia kwa sauti kuu na kusema na Sauli, akisema, “Kwa nini umenidanganya? Maana wewe ni Sauli.”
And when the woman had seen Samuel, she cried out with a loud voice, and she said to Saul: “Why have you afflicted me? For you are Saul!”
13 Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona kitu gani?” Yule mwanamke akamwambia Sauli, “Naona mungu akitoka katika nchi.” Akamuuliza mwanamke,
And the king said to her: “Do not be afraid. What have you seen?” And the woman said to Saul, “I saw gods ascending from the earth.”
14 “Je, anafanana na nani?” Mwanamke akajibu, “Mtu mzee anazuka; naye amevaa kanzu.” Sauli akafahamu kuwa huyo ni Samweli, naye Sauli akainamisha uso wake hadi chini akionesha heshima.
And he said to her, “What appearance does he have?” And she said, “An old man ascends, and he is clothed in a cloak.” And Saul understood that it was Samuel. And he bowed himself upon his face on the ground, and he reverenced.
15 Samweli akamwambia Sauli, “Kwa nini umenisumbua na kuniinua juu?” Sauli akajibu, “Nimetaabika sana, maana Wafilisti wamepanga vita dhidi yangu, na Mungu ameniacha na hanipi majibu tena, si kwa manabii, wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita, ili unijulishe kile nitakachofanya.”
Then Samuel said to Saul, “Why have you disquieted me, so that I would be raised up?” And Saul said: “I am greatly distressed. For the Philistines fight against me, and God has withdrawn from me, and he is not willing to heed me, neither by the hand of prophets, nor by dreams. Therefore, I have summoned you, so that you would reveal to me what I should do.”
16 Samweli akasema, “Kwa kuwa BWANA amekuacha, basi unaniuliza nini, naye amekuwa adui yako?
And Samuel said, “Why do you question me, though the Lord has withdrawn from you, and has crossed over to your rival?
17 BWANA amekutendea kile alichosema kuwa angekifanya. BWANA amerarua ufalme kutoka mkononi mwako na amempa ufalme mtu mwingine - amempa Daudi.
For the Lord will do to you just as he spoke by my hand. And he will tear your kingdom from your hand. And he will give it to your neighbor David.
18 Kwa sababu hukuitii sauti ya BWANA na hukutekeleza hasira yake kali juu ya Amaleki, kwa hiyo leo naye amefanya hili kwako.
For you did not obey the voice of the Lord, and you did not carry out the wrath of his fury upon Amalek. For this reason, the Lord has done to you what you are enduring this day.
19 Zaidi ya hayo, BWANA atamweka Israeli pamoja na wewe katika mkono wa Wafilisti. Kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. BWANA pia ataliweka jeshi la Israeli katika mkono wa Wafilisti.”
And the Lord also will give Israel into the hands of the Philistines, along with you. Then tomorrow you and your sons will be with me. But the Lord will also deliver the camp of Israel into the hands of the Philistines.”
20 Ndipo ghafla Sauli alianguka chini kifudifudi na aliogopa kwa sababu ya yale maneno ya Samweli. Aliishiwa nguvu mwilini mwake, kwa kuwa siku hiyo alikuwa hajala chakula, hata kwa usiku huo wote.
And immediately, Saul fell stretched out on the ground. For he was terrified by the words of Samuel. And there was no strength in him. For he had not eaten bread all that day.
21 Ndipo yule mwanamke akaja kwa Sauli na akaona kwamba Sauli amepata shida, naye akamwambia, “Tazama, mjakazi wako ameisikiliza sauti yako; Nimeyaweka maisha yangu mkononi mwangu na nimeyasikiliza maneno uliyoniambia.
And so, the woman entered to Saul, (for he was very troubled) and she said to him: “Behold, your handmaid has obeyed your voice, and I have placed my life in my hand. And I have heeded the words which you spoke to me.
22 Hivyo basi, nakusihi, sikiliza pia sauti ya mjakazi wako, na uniruhusu nilete chakula kidogo mbele yako. Ule ili upate nguvu za kwenda kule uendako.”
And so now, I ask you to heed the voice of your handmaid, and let me place before you a morsel of bread, so that, by eating, you may recover strength, and you may be able to undertake the journey.”
23 Lakini Sauli alikataa na kusema, “Sitakula.” Lakini watumishi wake, pamoja na yule mwanamke, wakamlazimisha hatimaye alisikiliza sauti zao. Hivyo aliinuka kutoka chini na kukaa kitandani.
But he refused, and he said, “I will not eat.” But his servants and the woman urged him, and after some time, heeding their voice, he rose up from the ground, and he sat upon the bed.
24 Yule mwanamke alikuwa na ndama mnono hapo nyumbani; akafanya haraka na kumchinja; akachua unga, akaukanda, na akatengeneza mikate isiyotiwa chachu kwa unga huo.
Now the woman had a fatted calf in the house, and she hurried and killed it. And taking meal, she kneaded it, and she baked unleavened bread.
25 Akaileta mbele ya Sauli na watumishi wake, nao wakala. Baaadaye waliinuka na kuondoka usiku huo.
And she set it before Saul and before his servants. And when they had eaten, they rose up, and they walked all through that night.

< 1 Samweli 28 >