< 1 Samweli 25 >

1 Basi Samweli akafariki. Waisraeli wote wakakusanyika pamoja na kumwomboleza, na wakamzika nyumbani kwake huko Rama. Kisha Daudi akainuka na akashuka hadi jangwa la Parani.
Or, Samuel mourut; et tout Israël s'assembla et le pleura; et on l'ensevelit dans sa maison à Rama. Et David se leva, et descendit au désert de Paran.
2 Kulikuwa na mtu mmoja huko Maoni, na mali zake zilikuwa huko Karmali. Mtu huyo alikuwa tajiri sana. Alikuwa na kondoo elfu tatu na mbuzi elfu moja. Naye alikuwa akiwakata manyoya kondoo wake huko Karmeli.
Or, il y avait à Maon un homme qui avait ses biens à Carmel, et cet homme était fort riche; il avait trois mille brebis et mille chèvres; et il était à Carmel quand on tondait ses brebis.
3 Na mtu huyo aliitwa Nabali, na jina la mke wake aliitwa Abigaili. Mwanamke huyo alikuwa mwenye busara na mzuri kwa sura. Lakini mwanaume alikwa mkaidi na mwovu katika mambo yake. Alikuwa wa uzao wa nyumba ya Kalebu.
Cet homme s'appelait Nabal, et sa femme s'appelait Abigaïl; c'était une femme de bon sens, et belle de visage, mais l'homme était dur, et méchant dans ses actions. Et il était de la race de Caleb.
4 Daudi akasikia akiwa jangwani kwamba Nabali alikuwa akiwakata manyoya kondoo wake.
Or, David apprit au désert que Nabal tondait ses brebis.
5 Hivyo Daudi aliwatuma kwake vijana kumi. Akawaambia wale vijana, “Pandeni kwanda Karmeli, mwendeeni Nabali, na mkamsalimie kwa jina langu.
Il envoya donc dix de ses gens, et leur dit: Montez à Carmel, et allez vers Nabal, et saluez-le de ma part,
6 Mtamwambia, 'Uishi katika baraka, Uwe na amani na nyumba yako iwe na amani, na wote ulionao wawe na amani.
Et dites-lui: Paix à toi pour la vie! Paix à ta maison et à tout ce qui t'appartient!
7 Nasikia kwamba unao wakata manyoya. Wachungaji wako walikuwa pamoja nasi, na hatukuwafanyia ubaya, na muda wote wakiwa Karmeli hawakupotelewa kitu chochote.
Et maintenant, j'ai appris que tu as les tondeurs. Or, tes bergers ont été avec nous, et nous ne leur avons fait aucun outrage, et il ne leur a rien manqué, tout le temps qu'ils ont été à Carmel.
8 Waulize vijana wako, nao watakuambia. Basi vijana wangu wapate kibali machoni pako, maana tumefika siku ya sherehe. Tafadhali utoe cho chote ulicho nacho mkononi kwa watumishi wako na kwa Daudi mwanao.'”
Demande-le à tes gens, et ils te le diront. Que mes gens trouvent donc grâce à tes yeux, puisque nous sommes venus en un bon jour; donne, je te prie, à tes serviteurs et à ton fils David, ce qui se trouvera sous ta main.
9 Vijana wa Daudi walipofika, walimwambia Nabali yote haya kwa niaba ya Daudi na kisha wakasubiri.
Les gens de David vinrent donc, et dirent à Nabal toutes ces paroles, au nom de David; puis ils se turent.
10 Nabali akawajibu watumishi wa Daudi, “Daudi ni nani? Na ni nani mwana wa Yese? Siku hizi wapo watumishi wengi wanaotoroka bwana zao.
Et Nabal répondit aux serviteurs de David et dit: Qui est David, et qui est le fils d'Isaï? Ils sont nombreux aujourd'hui les serviteurs qui abandonnent leurs maîtres!
11 Je, nichukue mkate wangu na maji yangu na nyama yangu ambayo nimewachinjia wakata manyoya wangu, na niwape watu wanaotoka nisikokujua?”
Et je prendrais mon pain, et mon eau, et ma viande que j'ai apprêtée pour mes tondeurs, et je les donnerais à des gens qui viennent je ne sais d'où?
12 Hivyo vijana wa Daudi waligeuka na kurudi, nakumwambia kila kitu kilichosemwa.
Alors les gens de David s'en retournèrent par leur chemin. Ils revinrent donc, et, à leur arrivée, lui rapportèrent toutes ces paroles.
13 Daudi akawaambia watu wake, “Kila mtu ajifunge upanga wake.” Kila mtu akajifunga upanga wake. Daudi naye pia akajifunga upanga wake. Yapata kama watu mia nne wakafuatana na Daudi, na wengine mia mbili walibaki kulinda mizigo yao.
Et David dit à ses gens: Que chacun de vous ceigne son épée; et ils ceignirent chacun leur épée. David aussi ceignit son épée; et il monta après David environ quatre cents hommes; mais deux cents demeurèrent auprès du bagage.
14 Lakini kijana mmojawapo alimwambia Abigaili, mke wa Nabali akasema, “Daudi aliwatuma wajumbe kutoka jangwani waje wamsalimu bwana wetu, na yeye akawatukana.
Or, un des serviteurs fit ce rapport à Abigaïl, femme de Nabal, et lui dit: Voici, David a envoyé du désert des messagers pour saluer notre maître; mais il s'est emporté contre eux.
15 Bado watu hawa walitutendea mema. Hatukudhurika na hatukupoteza chochote wakati wote tulipotembea nao tulipokuwa mbugani.
Et cependant ces gens ont été très bons envers nous, et nous n'en avons reçu aucun outrage; et rien de ce qui est à nous ne s'est perdu, tout le temps que nous avons été avec eux, lorsque nous étions aux champs;
16 Walikuwa ukuta wetu usiku na mchana, wakati wote tulikuwa pamoja nao tukichunga kondoo.
Ils nous ont servi de muraille, et la nuit et le jour, tout le temps que nous avons été avec eux, paissant les troupeaux.
17 Kwa hiyo tambua hili na zingatia utafanya nini, maana ubaya unamvizia bwana wetu, na utakuwa juu ya nyumba yake yote. Yeye ni mtu asiyefaa na hakuna awezaye kushauriana naye.”
Maintenant donc réfléchis, et vois ce que tu as à faire; car la ruine est résolue contre notre maître, et contre toute sa maison. Mais il est si méchant, qu'on n'ose lui parler.
18 Ndipo Abigaili akaharakisha na akachukuwa mikate mia mbili, chupa mbili za divai, kondoo watano waliokwisha andaliwa, vipimo vitano vya bisi, vishada mia moja vya zabibu, na mikate mia mbili ya tini na akavipakia juu ya punda.
Alors Abigaïl se hâta, et prit deux cents pains, deux outres de vin, cinq moutons tout apprêtés, cinq mesures de grain rôti, cent paquets de raisins secs, et deux cents cabas de figues sèches; et elle les mit sur des ânes.
19 Akamwambia kijana wake, “Tangulia mbele yangu, nami nitakuja nyuma yako.” Lakini hakumwambia mmewe Nabali.
Puis elle dit à ses gens: Passez devant moi; voici, je viens après vous. Mais elle n'en dit rien à Nabal, son mari.
20 Alipokuwa akienda juu ya punda wake na kutelemka penye kificho cha mlima, Daudi na watu wake walishuka chini wakimwelekea Abigaili, naye akakutana nao.
Et, montée sur un âne, elle descendait par un chemin couvert de la montagne; et voici, David et ses gens descendaient en face d'elle, et elle les rencontra.
21 Basi Daudi alikuwa amesema, “Hakika nimelinda bure vyote alivyonavyo mtu huyu huko nyikani, na vyote alivyonavyo hakuna kilichopotea, pamoja na hayo amenilipa mabaya badala ya mema.
Or, David avait dit: C'est bien en vain que j'ai gardé tout ce que cet homme avait dans le désert, de sorte qu'il ne s'est rien perdu de tout ce qui était à lui; il m'a rendu le mal pour le bien.
22 Mungu na anitendee hivyo mimi, Daudi, pia iwe zaidi, iwapo nitamwacha hata mtu mmoja wa kwake akiwa hai ifikapo kesho asubuhi.
Que Dieu fasse ainsi aux ennemis de David, et qu'il y ajoute, si d'ici à demain matin, je laisse subsister de tout ce qu'il a, même un seul homme.
23 Abigaili alipomwona Daudi, aliharakisha na kushuka chini ya punda wake, akalala kifudifudi na kujiinamisha hadi chini.
Quand donc Abigaïl aperçut David, elle se hâta de descendre de son âne, se jeta sur son visage devant David, et se prosterna en terre.
24 Akamwangukia miguuni pake na kusema, “Juu yangu tu, bwana wangu, na uwe uovu. Tafadhali acha mjakazi wako aseme nawe, tena uyasikilize maneno ya mjakazi wako.
Elle tomba donc à ses pieds, et dit: Que la faute soit sur moi, mon seigneur! mais que ta servante parle, je te prie, devant toi, et écoute les paroles de ta servante.
25 Nakusihi bwana wangu usimjali mtu huyu asiyefaa, Nabali, kwa maana kama jina lake lilivyo, ndivyo alivyo. Jina lake ni Nabali, na upumbavu uko pamoja naye. Lakini mimi mjakazi wako sikuwaona vijana wa bwana wangu, uliowatuma.
Que mon seigneur ne prenne pas garde, je te prie, à ce méchant homme, à Nabal; car il est tel que son nom; il s'appelle Nabal (fou), et il y a de la folie en lui. Mais moi, ta servante, je n'ai point vu les gens que mon seigneur a envoyés.
26 Sasa basi, bwana wangu, kama BWANA aishivyo, na kama unavyoishi, kwa kuwa BWANA amekuondoa kutoka kumwaga damu, na kuacha kulipiza kisasi kwa mkono mwenyewe, basi adui zako, na wale ambao wanatafuta kumfanyia uovu bwana wangu, wawe kama Nabali
Et maintenant, mon seigneur, comme l'Éternel est vivant, et comme ton âme vit, c'est l'Éternel qui t'a empêché d'en venir au sang et de te venger de ta propre main. Or, que tes ennemis, et ceux qui cherchent à nuire à mon seigneur, soient comme Nabal.
27 Na sasa zawadi hii ambayo mjakazi wako ameileta kwa bwana wangu, na wapewe vijana ambao wanamfuata bwana wangu.
Et maintenant, voici le présent que ta servante apporte à mon seigneur, afin qu'on le donne aux gens qui marchent à la suite de mon seigneur.
28 Tafadhali ulisamehe kosa la mjakazi wako, maana BWANA hakika atamfanyia bwana wangu nyumba imara, kwa sababu bwana wangu anapigana vita vya BWANA; na uovu hautaonekana ndani yako maadamu unaishi.
Pardonne, je te prie, la faute de ta servante; car l'Éternel ne manquera point d'établir à mon seigneur une maison stable, parce que mon seigneur soutient les guerres de l'Éternel, et qu'il ne s'est trouvé aucun mal en toi, pendant toute ta vie.
29 Na ingawa watu wangeinuka na kukuandama ili wakuue, bado uhai wa bwana wangu utafungwa katika furushi la walio hai na BWANA Mungu wako; na atayatupa maisha ya adui zako mbali, kama vile kutoka katika mfuko wa kombeo.
Et si quelqu'un se lève pour te persécuter, et pour chercher ta vie, l'âme de mon seigneur sera liée dans le faisceau de la vie auprès de l'Éternel ton Dieu; mais il lancera au loin, comme du milieu d'une fronde, l'âme de tes ennemis.
30 Na itakuwa, BWANA atakapokuwa amemtimizia bwana wangu mambo yote mazuri ambayo amekuahidi, na alivyokufanya kiongozi juu ya Israeli,
Et quand l'Éternel fera à mon seigneur tout le bien qu'il t'a dit, et qu'il t'établira conducteur d'Israël,
31 jambo hili halitakuwa huzuni kwako, wala chukizo moyoni kwa bwana wangu, kwa sababu hukumwaga damu bila sababu, na hujajilipizia kisasi. Na BWANA akikuletea mafanikio, umkumbuke mjakazi wako.”
Ceci ne te sera point en achoppement; et le cœur de mon seigneur n'aura point le remords d'avoir, sans cause, répandu le sang, et de s'être vengé soi-même; et quand l'Éternel aura fait du bien à mon seigneur, tu te souviendras de ta servante.
32 Ndipo Daudi akamwambia Abigaili, “BWANA, Mungu wa Israeli, abarikiwe, aliyekutuma uonane na mimi leo.
Alors David dit à Abigaïl: Béni soit l'Éternel, le Dieu d'Israël, qui t'a aujourd'hui envoyée au-devant de moi!
33 Na hekima yako ibarikiwe, nawe umebarikiwa, kwa sababu leo umenizuia nisiwe na hatia ya kumwaga damu, na kutojilipizia kisasi kwa mkono wangu mwenyewe.
Et bénie soit ta prudence, et sois bénie toi-même, toi qui m'as aujourd'hui empêché d'en venir au sang, et de me venger de ma propre main!
34 Kwa kweli, kama BWANA, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye amenizuia nisikuumize, kama usinge harakisha kuja ukutane nami, kwa hakika kesho asubuhi asinge salia hata mtoto mmoja wa kiume kwa Nabali.”
Mais certainement, comme l'Éternel, le Dieu d'Israël, qui m'a empêché de te faire du mal, est vivant, si tu ne te fusses hâtée de venir au-devant de moi, il ne serait pas demeuré de reste à Nabal, d'ici à demain matin, même un seul homme.
35 Kwa hiyo Daudi akavipokea kutoka mkononi mwake vile alivyokuwa amemletea; akamwambia, “Nenda kwa amani hadi nyumbani kwako; tazama, nimeisikiliza sauti yako na nimekubali.”
David prit donc de sa main ce qu'elle lui avait apporté, et lui dit: Remonte en paix à ta maison; regarde, j'ai écouté ta voix, et je t'ai accordé ta demande.
36 Abigaili akarudi kwa Nabali; tazama, alikuwa akifanya sherehe katika mji wake, kama sherehe ya mfalme; na moyo wa Nabali ulifurahi ndani yake, kwa sababu alikwa amelewa sana. Kwa hiyo hakumwambia chochote kabisa hadi kulipopambazuka
Alors Abigaïl revint vers Nabal, et voici, il faisait un festin dans sa maison, comme un festin de roi; et Nabal avait le cœur joyeux, et était entièrement ivre; et elle ne lui dit pas la moindre chose jusqu'au lendemain matin.
37 Ikawa asubuhi, divai ilipokuwa imemtoka Nabali, basi mkewe akamwambia mambo hayo; moyo wake ukafa ndani yake, na akawa kama jiwe.
Mais, le matin, quand Nabal fut revenu de son ivresse, sa femme lui dit ces choses; et son cœur en reçut un coup mortel, et il devint comme une pierre.
38 Ikawa baada ya siku kumi BWANA alimpiga Nabali naye akafa.
Et environ dix jours après, l'Éternel frappa Nabal, et il mourut.
39 Naye Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, akasema, “BWANA abarikiwe, aliyenichukulia hatua ya shutuma yangu kutoka mkono wa Nabali, na kumzuia mtumishi wake asifanye maovu. Na amemrudishia Nabali tendo la uovu juu ya kichwa chake mwenyewe.” Ndipo Daudi akawatuma watu wakaongee na Abigaili, ili amchukue awe mke wake.
Et quand David apprit que Nabal était mort, il dit: Béni soit l'Éternel qui m'a fait droit de l'outrage que j'avais reçu de la main de Nabal, et qui a préservé son serviteur de faire du mal! Mais l'Éternel a fait retomber la malice de Nabal sur sa tête! Puis David envoya des gens à Abigaïl, et lui fit parler, afin de la prendre pour sa femme.
40 Watumishi wake Daudi walipofika kwa Abigaili huko Karmeli, wakaongea naye na kusema, “Daudi ametutuma kwako tukuchukue hadi kwake uwe mke wake.”
Les serviteurs de David vinrent donc vers Abigaïl, à Carmel, lui parlèrent, en disant: David nous a envoyés vers toi, afin de te prendre pour sa femme.
41 Abigaili aliinuka, akainamisha uso chini, na akasema, “Tazama, mjakazi wako ni mtumwa aoshaye miguu ya watumishi wa bwana wangu.”
Alors elle se leva, se prosterna le visage contre terre, et dit: Voici, ta servante sera à ton service pour laver les pieds des serviteurs de mon seigneur!
42 Akaharakisha na kuamka, akapanda punda akiwa na vijakazi wake watano waliofuatana naye; akawafuata wajumbe wa Daudi, na akawa mke wake.
Puis Abigaïl se leva promptement et monta sur son âne, et cinq servantes la suivaient; et elle suivit les messagers de David, et elle fut sa femme.
43 Daudi pia alimchukua Ahinoamu wa Yezreeli akamwoa; wote wawili wakawa wake zake.
David avait aussi épousé Achinoam de Jizréel, et toutes deux furent ses femmes.
44 Wakati huo Sauli alikuwa amempa Palti, mwana wa Laishi mtu wa Galimu, Mikali, binti yake, aliyekuwa mke wa Daudi.
Mais Saül avait donné Mical sa fille, femme de David, à Palti, fils de Laïsh, qui était de Gallim.

< 1 Samweli 25 >