< 1 Wafalme 15 >

1 Katika mwaka wa kumi na tano wa mfame Yeroboamu mwana wa Nebati, Abiya alianza kutawala juu yaYuda.
و در سال هجدهم پادشاهی یربعام بن نباط، ابیام، بر یهودا پادشاه شد.۱
2 Alitawala kwa miaka mitata kule Yerusalemu. Jina la mama yake allikuwa Maaka. Alikuwa binti wa Absalomu.
سه سال در اورشلیم سلطنت نمود و اسم مادرش معکه دختر ابشالوم بود.۲
3 Naye alitembea katika dhambi zote ambazo baba yake alizifanya kabla yake; moyo wake haukuwa mkalifu kwa BWANA, Mungu wake kama moyo wa Daudi, babu yake ulivyokuwa.
و در تمامی گناهانی که پدرش قبل از او کرده بود، سلوک می‌نمود، ودلش با یهوه، خدایش مثل دل پدرش داود کامل نبود.۳
4 Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi, BWANA, Mungu wake alimpa taa Yerusalemu kwa kumwinua mwanae baada yake ili kuiimarisha Yerusalemu.
اما یهوه، خدایش به‌خاطر داود وی رانوری در اورشلیم داد تا پسرش را بعد از اوبرقرار گرداند، و اورشلیم را استوار نماید.۴
5 Mungu alifanya haya kwa sababu Daudi alifanya yaliyo mema machoni pake; wakati wote wa uhai wake, hakugeuka wala hakukosa katika yote aliyomwamuru, isipokuwa tu swala la Uria Mhiti.
چونکه داود آنچه در نظر خداوند راست بود، بجا می‌آورد و از هرچه او را امر فرموده، تمام روزهای عمرش تجاوز ننموده بود، مگر در امراوریای حتی.۵
6 Sasa kulikuwa na vita kati ya Rehoboamu na Jeroboamu katika siku zote za maisha ya Abiya.
و در میان رحبعام و یربعام تمام روزهای عمرش جنگ بود.۶
7 Kwa mambo mengine ya Abiya, yote aliyofanya, je, hayajaandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda? Sasa kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu.
و بقیه وقایع ابیام وهرچه کرد، آیا در کتاب تواریخ ایام پادشاهان یهودا مکتوب نیست؟ و در میان ابیام و یربعام جنگ بود.۷
8 Abiya akalala na mababu zake, nao wakamzika katika mji wa Daudi. Asa mwanae akawa mfalme mahali pake.
و ابیام با پدران خویش خوابید و او رادر شهر دفن کردند و پسرش آسا در جایش سلطنت نمود.۸
9 Katika mwaka wa ishirini wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Asa akaanza kutawala Yuda.
و در سال بیستم یربعام پادشاه اسرائیل، آسابر یهودا پادشاه شد.۹
10 Alitawala kwa miaka arobaini na moja kule Yerusalemu. Bibi yake alikuwa Maaka, binti wa Absalomu.
و در اورشلیم چهل و یک سال پادشاهی کرد و اسم مادرش معکه دخترابشالوم بود.۱۰
11 Asa akafanya yaliyo mema machono mwa BWANA, kama alivyofanya Daudi, babu yake.
و آسا آنچه در نظر خداوند راست بود، مثل پدرش، داود عمل نمود.۱۱
12 Yeye aliwafukuza kutoka katika nchi wale makahaba wa kipagani na akaziondoa sanamu zote ambazo babu zake walikuwa wametengeneza.
و الواط را ازولایت بیرون کرد و بت هایی را که پدرانش ساخته بودند، دور نمود.۱۲
13 Pia alimwondoa bibi yake asiwe Malkia, kwa sababu alikuwa amefanya sanamu ya kuchukiza kwa Ashera. Asa aliikata sanamu ya kuchukiza na kuiteketeza katika Bonde la Kidroni.
و مادر خود، معکه را نیز ازملکه بودن معزول کرد، زیرا که او تمثالی به جهت اشیره ساخته بود. و آسا تمثال او را قطع نموده، آن را در وادی قدرون سوزانید.۱۳
14 Lakini pale mahali pa juu hapakuchukuliwa. Hata hivyo. Moyo wa Asa ulikuwa mkamilifu mbele ya BWANA katika siku zake zote.
اما مکان های بلند برداشته نشد لیکن دل آسا در تمام ایامش باخداوند کامل می‌بود.۱۴
15 Alivirerjesha katika nyumba ya BWANA vitu vile vilivyokuwa vimetengwa kwa ajili ya BWANA, na vile vitu vyake vilivyokuwa vimetengezwa kwa fedha, na dhahabu na vyombo.
و چیزهایی را که پدرش وقف کرده و آنچه خودش وقف نموده بود، از نقره و طلا و ظروف، در خانه خداونددرآورد.۱۵
16 Basi kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli, kwa miaka yao yote.
و در میان آسا و بعشا، پادشاه اسرائیل، تمام روزهای ایشان جنگ می‌بود.۱۶
17 Baasha mfalme wa Israeli, akaivamia na kuijenga Rama, kiasi kwamba hakumruhusu yeyote kuondoka au kuingia katika nchi ya Asa mfalme wa Yuda.
و بعشاپادشاه اسرائیل بر یهودا برآمده، رامه را بنا کرد تانگذارد که کسی نزد آسا، پادشاه یهودا رفت و آمدنماید.۱۷
18 Kisha Asa akazichukua zile fedha na dhahabu zilizokuwa zimebaki kwenye hazina kwenye nyumba ya BWANA, na katika hazina ya ikulu ya mfalme. Akaziweka katika mikono ya watumishi wake na kuzituma kwa Beni Hadadi mwana wa Tabrimoni mwana wa Hezioni, mfalme wa Shamu ambaye alikuwa akishi Dameski. Akamwambia,
آنگاه آسا تمام نقره و طلا را که درخزانه های خانه خداوند و خزانه های خانه پادشاه باقی‌مانده بود گرفته، آن را به‌دست بندگان خودسپرد و آسا پادشاه ایشان را نزد بنهدد بن طبرمون بن حزیون، پادشاه ارام که در دمشق ساکن بودفرستاده، گفت:۱۸
19 “Naomba tufanye patano kati yangu na wewe, kama ilivyokuwa kati ya baba yangu na baba yako. Tazama, Nimekutumia zawadi ya fedha na dhahabu. Ili uvunje agano lako na Baasha mfalme wa Israeli, ili kwamba aniache.”
«در میان من و تو و در میان پدرمن و پدر تو عهد بوده است، اینک هدیه‌ای از نقره و طلا نزد تو فرستادم، پس بیا و عهد خود را بابعشا، پادشاه اسرائیل بشکن تا او از نزد من برود.»۱۹
20 Beni Hadadi akamsikiliza mfalme Asa na kutuma wakuu wa majeshi yake, nao wakaishambulia miji ya Israeli. Wakaishambulia Ijoni, Dani, Abeliya Bethi Maaka, na Kinerothi yote, pamoja na nchi yote ya Naftali.
و بنهدد، آسا پادشاه را اجابت نموده، سرداران افواج خود را بر شهرهای اسرائیل فرستاد و عیون ودان و آبل بیت معکه و تمامی کنروت را با تمامی زمین نفتالی مغلوب ساخت.۲۰
21 Ikawa Baasha aliposikia haya, akaacha kuijenga Rama akarudi Tirza.
و چون بعشا این را شنید بنا نمودن رامه را ترک کرده، در ترصه اقامت نمود.۲۱
22 Kisha mfalme Asa akaitangazia Yuda yote. Hakuna aliyeachwa. Wakayabeba mawe na miti ya Rama ambayo Baasha alikuwa akijengea mji. Kisha mfalme Asa akavitumia hivyo vitu kuijenga Geba ya Benjamini na Mispa.
و آسا پادشاه در تمام یهودا ندادرداد که احدی از آن مستثنی نبود تا ایشان سنگهای رامه و چوب آن را که بعشا بنا می‌کردبرداشتند، و آسا پادشاه جبع بنیامین و مصفه را باآنها بنا نمود.۲۲
23 Mambo mengine yanyohusu utawala wa Asa, uwezo wake wote, yote aliyofanya, na miji aliyoijenga, je, hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda? Lakini wakati wa uzee wake alipata ugonjwa wa miguu.
و بقیه تمامی وقایع آسا و تهور اوو هرچه کرد و شهرهایی که بنا نمود، آیا در کتاب تواریخ ایام پادشاهان یهودا مذکور نیست؟ اما درزمان پیریش درد پا داشت.۲۳
24 Kisha Asa akalala na mababu zake na akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Yehoshafati mwanae akawa mfalme mahali pake.
و آسا با پدران خویش خوابید و او را در شهر داود با پدرانش دفن کردند، و پسرش یهوشافاط در جایش سلطنت نمود.۲۴
25 Nadabu mwana wa Yerobiamu alianza kutawala huko Israeli wakati wa mwaka wa pili wa Asa mfalme wa Yuda; Aliitawala Israeli kwa miaka miwili.
و در سال دوم آسا، پادشاه یهودا، ناداب بن یربعام بر اسرائیل پادشاه شد، و دو سال براسرائیل پادشاهی کرد.۲۵
26 Akafanya yaliyo maovu mbele y a macho ya BWANA naye akatembea katika njia ya baba yake, na katika dhambi yake, aliisababisha Israeli kufanya dhambi.
و آنچه در نظر خداوندناپسند بود، بجا می‌آورد. و به راه پدر خود و به گناه او که اسرائیل را به آن مرتکب ساخته بود، سلوک می‌نمود.۲۶
27 Baasha mwana wa Ahiya, wa familia ya Isakari, akafanya hila dhidi ya Nadabu; Baasha akamwua huko Gibethoni, ambao ulikuwa mji wa Wafilisti, kwa kuwa Nadabu na Israeli walikuwa wakiuhusuru Gibethoni.
و بعشا ابن اخیا که از خاندان یساکار بود، بروی فتنه انگیخت و بعشا او را در جبتون که از آن فلسطینیان بود، کشت و ناداب و تمامی اسرائیل، جبتون را محاصره نموده بودند.۲۷
28 Katika mwaka wa tatu wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha alimwua Nadabu naye akawa mfalme mahali pake.
و در سال سوم آسا، پادشاه یهودا، بعشا او را کشت و درجایش سلطنت نمود.۲۸
29 Mara tu baad ya kuwa mfalme, Baasha aliwaua watu wote wa familia ya Yeroboamu. Hakumwacha hata mmoja wa uzao wa Yeroboamu awe hai; Kwa njia hii akawa ameuharibu ukoo wote wa kifalme, kama vile BWANA alivyokuwa amesema kupitia mtumishi wake Ahiya Mshilo,
و چون او پادشاه شد، تمام خاندان یربعام را کشت و کسی را برای یربعام زنده نگذاشت تا همه را هلاک کرد موافق کلام خداوند که به واسطه بنده خود اخیای شیلونی گفته بود.۲۹
30 kwa sababu ya dhambi za Yeroboamu ambazo alifanya na akaisababishia Israeli kufanya dhambi, kwa kuwa alimkasirisha BWANA, Mungu wa Israeli.
و این به‌سبب گناهانی شد که یربعام ورزیده، و اسرائیل را به آنها مرتکب گناه ساخته، و خشم یهوه، خدای اسرائیل را به آنها به هیجان آورده بود.۳۰
31 Mambo mengine yanayomhusu Nadabu, na yote aliyofanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?
و بقیه وقایع ناداب و هرچه کرد، آیا درکتاب تواریخ ایام پادشاهان اسرائیل مکتوب نیست؟۳۱
32 Kisha kulikuwa na vita kati ya Asa na Baasha mfalme wa Israeli katika siku zao zote.
و در میان آسا و بعشا، پادشاه اسرائیل، در تمام روزهای ایشان جنگ می‌بود.۳۲
33 Katika mwaka wa tatu wa Asa mfalme wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya alianza kuitawala Israeli yote huko Tirza naye alitawala kwa miaka ishirini na nne.
در سال سوم آسا، پادشاه یهودا، بعشا ابن اخیا بر تمامی اسرائیل در ترصه پادشاه شد وبیست و چهار سال سلطنت نمود.۳۳
34 Naye akafanya yaliyo mabaya katika macho ya BWANA na akatembea katika njia ya Yeroboamu na katika dhambi yake ambayo kwa hiyo aliifanya Israeli kufanya dhambi.
و آنچه درنظر خداوند ناپسند بود، می‌کرد و به راه یربعام وبه گناهی که اسرائیل را به آن مرتکب گناه ساخته بود، سلوک می‌نمود.۳۴

< 1 Wafalme 15 >