< 1 Nyakati 27 >

1 Hii ni orodha ya familia za viongozi wa Israeli, wakuu wa maelfu na mamia, pamoja na maafisa wa jeshi walio mtumikia mfalme kwa namna tofauti. Kila kikosi cha jeshi kilitumika mwenzi hadi mwezi kwa mwaka mzima. Kila kikosi kilikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
This is a list of the Israeli men who served the king in the army. Some were leaders of families, some were commanders of 100 men, some were commanders of 1,000 men, and some were their officers. There were 24,000 men [DOU] in each group. Each group served one month of each year.
2 Kwa mwezi wa kwanza wa kikosi alikuwa Yashobeamu mwana wa Zabdieli. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
Jashobeam, the son of Zabdiel, was in charge of the group that served during the first month [of each year].
3 Alikuwa miongoni mwa uzao wa Perezi na mhusika wa maafisa wa jeshi kwa mwezi wa kwanza.
He was a descendant of Perez, and he was the commander of all the army officers during the first month of each year.
4 Juu ya kikosi kwa mwezi wa pili alikuwa Dodai, wa ukoo wa uliotoka kwa Ahoa. Mikilothi alikuwa wa pili kwa cheo. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
Dodai, from the clan of Ahohi, was the commander of the group that served during the following/second month of each year. Mikloth was his (assistant/chief officer).
5 Mkuu wa jeshi wa mwezi wa tatu alikuwa Benaia mwana wa Yehoiada, kuhani na kiongozi. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
Benaiah, the son of Jehoiada the Supreme Priest, was the commander of the group that served during the following/third month.
6 Huyu ni Benaia aliye kuwa kiongozi wa wale thelathini na juu ya wale thelathini. Amizabadi mwanae alikuwa katika kikosi chake.
He was the one who was a mighty warrior among David’s thirty greatest soldiers, and he was their leader. His son Ammizabad was his assistant.
7 Mkuu kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli kaka wa Yoabu. Zebadia mwanae akawa mkuu baada yake. Katika kikosi chake kulikuwa na wanaume elfu ishirini na nne.
Asahel, Joab’s [younger] brother, was [the commander of the group that served] during the following/fourth month. Asahel’s son Zebadiah became the commander after Asahel [was killed].
8 Mkuu kwa mwezi wa tano alikuwa Shamihuthi, mzao wa Izra. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The commander for the following/fifth month was Shamhuth, a descendant of Izrah.
9 Mkuu kwa mwezi wa sita alikuwa Ira mwana wa Ikeshi, kutoka Tekoa. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The commander for the following/sixth month was Ira the son of Ikkesh from Tekoa [town].
10 Mkuu kwa mwezi wa saba alikuwa Helezi Mpeloni, kutoka watu wa Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The commander for the following/seventh month was Helez, a member of the Pelon [clan] from the tribe of Ephraim.
11 Mkuu kwa mwezi wa nane alikuwa Sibekai Mhushathi, kutoka ukoo ulitoka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The commander for the following/eighth month was Sibbecai, a descendant of Zerah from Hushah [town].
12 Mkuu kwa mwezi wa tisa alikuwa Abi Ezeri Manathothi, kutoka kwa kabila la Benjamini. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The commander for the following/ninth month was Abiezer from Anathoth [city] in the tribe of Benjamin.
13 Mkuu kwa mwezi wa kumi alikuwa Maharai kutoka mji wa Netofa, kutoka ukoo ulio toka kwa Zera. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The commander for the following/tenth month was Maharai, a descendant of Zerah from Netophath [town].
14 Mkuu kwa mwezi wa kumi na moja alikuwa Benaia kutoka mji wa Pirathoni, kutoka kabila la Efraimu. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The commander for the following/eleventh month was Benaiah from Pirathon [town] in the tribe of Ephraim.
15 Mkuu kwa mwezi wa kumi na mbili alikuwa Helidai kutoka mji wa Netopafa, kutoka ukoo uliotoka kwa Othinieli. Katika kikosi chake walikuwa wanaume elfu ishirini na nne.
The commander for the last month [of each year] was Heldai, a descendant of Othniel from Netophath [town].
16 Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli: Kwa kabila la Rubeni, Eliezeri mwana wa Zikri alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Simeoni, Shefatia mwana wa Maka alikuwa kiongozi.
This is a list of the administrators of the [twelve] tribes [DOU] of Israel: Eliezer, the son of Zicri, was the administrator of the tribe of Reuben. Shephatiah, the son of Maacah, was the administrator of the tribe of Simeon.
17 Kwa kabila la Lawi, Hashinia mwana wa Kemueli alikuwa kiongozi, na Zadoki aliongoza uzao wa Aruni.
Hashabiah, the son of Kemuel, was the administrator of the tribe of Levi. Zadok was the administrator of the tribe of Aaron.
18 Kwa kabila la Yuda, Elihu, mmoja wa kaka zake Daudi, alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Isakari, Omri mwana wa Mikaeli alikuwa kiongozi.
Elihu, David’s [older] brother, was the administrator of the tribe of Judah. Omri, the son of Michael, was the administrator of the tribe of Issachar.
19 Kwa kabila la Zebuluni, Ishimaia mwana wa Obadia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Naftali, Yeremothi mwana wa Azirieli alikuwa kiongozi.
Ishmaiah, the son of Obadiah, was the administrator of the tribe of Zebulun. Jerimoth, the son of Azriel, was the administrator of the tribe of Naphtali.
20 Kwa kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Azazia alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Manase, Yoeli mwana wa Pedaia alikuwa kiongozi.
Hoshea, the son of Azaziah, was the administrator of the tribe of Ephraim. Joel, the son of Pedaiah, was the administrator of the tribe of the [western] half of the tribe of Manasseh.
21 Kwa nusu kabila la Manase lililo Gileadi, Ido mwana wa Zekaria alikuwa kiongozi. Kwa kabila la Benjamini, Yaasieli mwana wa Abneri alikuwa kiongozi.
Iddo, the son of Zechariah, was the administrator of the [eastern] half of the tribe of Manasseh, in [the] Gilead [region]. Jaasiel, the son of Abner, was the administrator of the tribe of Benjamin.
22 Kwa kabila la Dani, Azareli mwana wa Yerohamu alikuwa kiongozi. Hawa walikuwa viongozi wa makabila ya Israeli.
Azarel, the son of Jeroham, was the administrator of the tribe of Dan. Those were the leaders over the tribes of Israel.
23 Daudi hakuwa hesabu wenye umri wa miaka ishirini au chini zaidi, kwasababu Yahweh alihaidi kuongeza Israeli kama nyota za mbinguni.
[When] David [told Joab to count the men of Israel, he] did not [tell him to] count the men who were less then 20 years old, because Yahweh had promised [many years previously] that there would be as many [people] in Israel as there are stars in the sky.
24 Yoabu mwana wa Zeruia alianza kuhesabu wanaume, lakini hakumaliza. Gadhabu iliangukia Israeli kwa hili. Hii idadi haikuandikwa kwenye nyakati za mfalme Daudi.
Joab [and his helpers] started to count the men of Israel, but they did not finish counting them [because Joab knew that Yahweh was angry about their being counted]. Yahweh punished [MTY] the people of Israel because of this counting, and as a result the total number of Israeli men [able to serve in the army] was not written on the scroll about King David’s [rule].
25 Azimavethi mwana wa Adieli alikuwa mhusika wa hazina za mfalme. Yonathani mwana wa Uzia alikuwa juu ya nyumba za ghala katika mashamba, kwenye miji, na vijijini, na kwenye minara iliyo imarishwa.
Azmaveth, the son of Adiel, was in charge of the king’s storehouses. Jonathan, the son of Uzziah, was is charge of the storehouses in various towns and villages in Israel, and also in charge of the watchtowers.
26 Ezri mwana wa Kelubi alikuwa juu ya mashamba, hao walio lima ardhi.
Ezri the son of Kelub was in charge of the workers who farmed the land [that belonged to the king].
27 Shimei kutoka Rama alikuwa juu ya mashamba ya mizabibu, na Zabdi kutoka Shefamu alikuwa juu ya mizabibu na mhifadhi wa mvinyo.
Shimei from Ramath [town] was in charge of the king’s vineyards. Zabdi from Shepham [town] was in charge of storing the wine from the [grapes produced in] vineyards.
28 Mwangalizi wa miti mizeituni na miti ya mikuyu iliyo kuwa bondeni alikuwa Baali Hanani kutoka Gederi, na juu ya nyumba za ghala za mafuta alikuwa Yoashi.
Baal-Hanan from Geder [city] was in charge of storing the olive oil.
29 Juu ya mifugo iliyo kuwa inalishwa huko Sharoni alikuwa Shitrai kutoka Sharoni, na juu ya mifugo iliyo kuwa mabondeni alikuwa Shafati mwana wa Adlai.
Shitrai from the Sharon Plain was in charge of the herds of cattle that (grazed/ate grass) there. Shaphat the son of Adlai was in charge of the cattle in the valleys.
30 Msimamizi wa ngamia alikuwa Obili Mishimaeli, na juu ya punda wakike alikuwa Yehideia kutoka Meronothi. Juu ya mifugo alikuwa Yazizi Mhagri.
Obil, a descendant of Ishmael, was in charge of the camels. Jehdeiah from Meronoth [town] was in charge of the donkeys.
31 Hawa wote walikuwa wasimamizi wa mali za Mfalme Daudi.
Jaziz, a descendant of Hagar, was in charge of the [king’s] flocks of sheep. All of those officials were in charge of the things that belonged to King David.
32 Yonathani, mjomba wake Daudi alikuwa mshauri, sababu alikuwa na busara na mwandishi. Yehieli mwana wa Hakimoni aliwajali watoto wa mfalme.
David’s uncle Jonathan was a wise counselor for him. Jehiel, the son of Hacmoni, taught the king’s sons.
33 Ahithofeli alikuwa mshauri wa mfalme, na Hushai kutoka watu wa Waariki alikuwa mshauri wake wa siri.
Ahithophel was the king’s official counselor.
34 Nafasi ya Ahithofeli ilichukuliwa na Yehoiada mwana wa Benaia, na Abiathari. Yoabu alikuwa mkuu wa jeshi la mfalme.
Hushai from the Ark people-group was the king’s special friend. Benaiah’s son Jehoiada became the king’s advisor after Ahithophel died, and later Abiathar became his advisor. Joab was the chief commander of the army.

< 1 Nyakati 27 >