< 1 Nyakati 24 >

1 Makundi vya kazi kulingana na uzao wa Aroni yalikuwa haya: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
The work groups based on Aaron's descendants were these: Nadab, Abihu, Eleazar and Ithamar.
2 Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao kufa. Walikuwa hawana watoto, kwahiyo Eleazari na Ithamari walitumika kama makuhani.
Nadab and Abihu died before their father died. They had no children, so Eleazar and Ithamar served as priests.
3 Daudi pamoja na Zadoki, uzao wa Eleazari, na Ahimeleki, uzao wa Ithamari, waliwagawanya katika makundi yao ya kazi kama makuhani.
David, together with Zadok, a descendant of Eleazar, and Ahimelech, a descendant of Ithamar, divided them into groups for their work as priests.
4 Kulikuwa na wanaume viongozi zaidi kati ya uzao wa Eleazari kuliko kati ya uzao wa Ithamari, kwahiyo waligawanya uzao wa Eleazari katika makundi kumi na sita. Walifanya hivyo na viongozi wa ukoo na uzao wa Ithamari. Magawanyo haya yalikuwa nane kwa idadi, sambamba na koo zao.
There were more leading men among Eleazar's descendants than among Ithamar's descendants, so they divided Eleazar's descendants into sixteen groups. They did this by heads of clans and by Ithamar's descendants. These divisions were eight in number, corresponding to their clans.
5 Waliwagawanya bila upendeleo kwa kura, kwa kuwa walikuwa waamuzi watakatifu na waamuzi wa Mungu, kutoka pande zote uzao wa Eleazari na uzao wa Ithamari.
They divided them impartially by lot, for there were holy officials and officials of God, from both Eleazar's descendants and Ithamar's descendants.
6 Shemaia mwana wa Nethaneli mwandishi, Mlawi, aliandika majina yao mbele ya mfalme, muamuzi, kuhani Zadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa makuhani na familia za Walawi. Ukoo mmoja ulichaguliwa kwa kura kutoka uzao wa Eleazari, na kisha uliofata utachaguliwa kutoka uzao wa Ithhamari.
Shemaiah son of Nethanel the scribe, a Levite, wrote down their names in the presence of the king, the officials, Zadok the priest, Ahimelech son of Abiathar, and the leaders of the priestly and Levite families. One clan was drawn by lot from Eleazar's descendants, and then the next would be drawn from Ithamar's descendants.
7 Kura ya kwanza ilienda kwa Yehoiaribu, ya pili kwa Yedaia,
The first lot went to Jehoiarib, the second to Jedaiah,
8 ya tatu kwa Harimu, ya nne kwa Seorimu,
the third to Harim, the fourth to Seorim,
9 ya tano kwa Malikija, ya sita kwa Mijamini,
the fifth to Malchijah, the sixth to Mijamin,
10 ya saba kwa Hakozi, ya nane kwa Abija,
the seventh to Hakkoz, the eighth to Abijah,
11 ya tisa kwa Yeshua, ya kumi kwa Shekania,
the ninth to Jeshua, the tenth to Shecaniah,
12 ya kumi na moja kwa Eliashibu, ya kumi na mbili kwa Yakimu,
the eleventh to Eliashib, the twelfth to Jakim,
13 ya kumi na tatu kwa Hupa, ya kumi na nne kwa Yesheheabu,
the thirteenth to Huppah, the fourteenth to Jeshebeab,
14 ya kumi na tano kwa Biliga, ya kumi na sita kwa Imma,
the fifteenth to Bilgah, the sixteenth to Immer,
15 ya kumi na saba kwa Heziri, ya kumi na nane kwa Hapizezi,
the seventeenth to Hezir, the eighteenth to Happizzez,
16 ya kumi na tisa kwa Pethaia, ya ishirini kwa Yehezikeli,
the nineteenth to Pethahiah, the twentieth to Jehezkel,
17 ya ishirini na moja kwa Yakini, ya ishirini na mbili kwa Gamuli,
the twenty-first to Jakin, the twenty-second to Gamul,
18 ya ishirini na tatu kwa Delaia, na ya ishirini na nne kwa Maazia.
the twenty-third to Delaiah, and the twenty-fourth to Maaziah.
19 Hii ilikuwa taratibu ya utumishi wao, walipo kuja kwenye nyumba ya Yahweh, wakifuata utaratibu waliopewa na Aruni babu yao, kama Yahweh, Mungu wa Israeli, alivyo waagiza.
This was the order of their service, when they came into Yahweh's house, following the procedure given to them by Aaron their ancestor, as Yahweh, the God of Israel, had instructed him.
20 Hawa walikuwa Walawi waliobakia: Wana wa Amiramu, Shebueli; wana wa Shebaeli, Yedeia.
These were the rest of the descendants of Levi: Of the sons of Amram, Shubael; of the sons of Shubael, Jehdeiah.
21 Wana wa Rehabia: wana wa Rehabia, Ishia kiongozi.
As for Rehabiah, the sons of Rehabiah: Ishijah the leader.
22 Wa Waizari, Shelomothi; mwana wa Shelomothi, Yahathi.
From the Izharites: Shelomoth; from the sons of Shelomoth: Jahath.
23 Wana wa Hebroni: Yeria kiongozi, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
The sons of Hebron: Jeriah the leader, Amariah the second, Jahaziel the third, and Jekameam the fourth.
24 Wana wa uzao wa Uzieli ulimjumuisha Mika. Uzao wa Mika ulimjumuisha Shamiri.
The son of Uzziel: Micah; from the sons of Micah: Shamir.
25 Kaka wa Mika alikuwa Ishia. Wana wa Ishia akijumuishwa Zakaria.
The brother of Micah: Ishijah. From the sons of Ishijah: Zechariah.
26 Wana na Merari: Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia, Beno.
The sons of Merari: Mahli and Mushi; from the son of Jaaziah: Beno.
27 Wana wa Merari: Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri, na Ibrri.
The sons of Merari from Jaaziah: Beno, Shoham, Zaccur, and Ibri.
28 Wana wa Mahili: eleazari, ambaye alikuwa hana wana.
From Mahli: Eleazar, who had no sons.
29 Wana wa Kishi: Yerameli
From Kish: The son of Kish: Jerahmeel.
30 wana wa Mushi: Mahli, Eda, na yerimothi. Walikuwa walawi, walio orodheshwa na familia zao.
The sons of Mushi: Mahli, Eder, and Jerimoth. These were the Levites, listed by their families.
31 Wanaume hawa ambao walikuwa vichwa katika nyumba za baba zao na kila wadogo zao, walipiga kura katika uwepo wa Mfalme Daudi, na Zadoki na Ahimeleki, pamoja na viongozi wa familia wa makuhani na Walawi. Walirusha kura kama uzao wa Aroni walivyofanya.
These men who were the head of each father's house and each of their younger brothers, cast lots in the presence of King David, and Zadok and Ahimelech, along with the leaders of the families of the priests and Levites. They cast lots just as Aaron's descendants had done.

< 1 Nyakati 24 >