< 1 Nyakati 2 >

1 Hawa ndio wana wa Israeli: Reubeni, Simioni, Lawi, Yuda, Isakari, Zebuloni,
Ovo su sinovi Izrailjevi: Ruvim, Simeun, Levije i Juda, Isahar i Zavulon,
2 Dani, Yusufu, Benyamini, Naftali, Gadi, na Asheri.
Dan, Josif i Venijamin, Neftalim, Gad i Asir.
3 Wana wa Yuda walikuwa Eri, Onani, na Shela, ambao walizaliwa na binti wa Shua, Wakanaani. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa muovu katika macho ya Yahweh, na Yahweh akamwua.
Sinovi Judini: Ir i Avnan i Sila; ta mu tri rodi kæi Suvina Hananejka; ali Ir prvenac Judin bješe nevaljao pred Gospodom, te ga ubi.
4 Tamari, mkwe wake, alimzalia Peresi na Zera. Yuda alikuwa na wana wa kiume wa tano.
A Tamara snaha njegova rodi mu Faresa i Zaru. Svega pet bješe sinova Judinijeh.
5 Wana wa Peresi walikuwa Hesroni na Hamuli.
Sinovi Faresovi: Esron i Amul.
6 Wana wa Zera walikuwa Zimri, Ethani, Hemani, Kalikoli na Darda, wote kwa jumla ni watano.
A sinovi Zarini: Zimrije i Etan i Eman i Halkol i Dara; svega pet.
7 Mwana wa Karmi alikuwa ni Akani, aliye leta taabu katika Israeli alipo iba kile kilicho hifadhiwa kwa ajili ya Mungu.
I sinovi Harmijini: Ahan, koji smuti Izrailja ogriješiv se o stvari proklete.
8 Mwana wa Ethani alikuwa Azaria.
A sinovi Etanovi: Azarija.
9 Wana wa Hezroni walikuwa ni Yerameeli, Ramu, na Kalebu.
A sinovi Esronovi, što mu se rodiše: Jerameilo i Aram i Halev.
10 Ramu akawa baba wa Aminadabu, na Aminadabu akawa baba wa Nashoni, kiongozi miongoni uzao wa Yuda.
A Aram rodi Aminadava, a Aminadav rodi Nasona, kneza sinova Judinijeh;
11 Nashoni akawa baba wa Salmoni, na Salmon akawa baba wa Boazi.
A Nason rodi Salmona; a Salmon rodi Voza;
12 Boazi akawa baba wa Obedi, na Obedi akawa baba wa Yese.
A Voz rodi Ovida; a Ovid rodi Jeseja;
13 Yese akawa baba wa mzaliwa wake wa kwanza Eliabu, wa pili Abinadabu, wa tatu Shama.
A Jesej rodi prvenca svojega Elijava, i Avinadava drugoga i Samu treæega,
14 Nethaneli wa nne, Radai wa tano.
Natanaila èetvrtoga, Radaja petoga,
15 Ozemu wa sita, na Daudi wa saba.
Osema šestoga, Davida sedmoga,
16 Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa Abishai, Yoabu, na Asaheli, jumla watatu.
I sestre im Seruju i Avigeju. A sinovi Serujini bjehu Avisaj i Joav i Asailo, trojica.
17 Abigali akamzaa Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri Mwishmaeli.
A Avigeja rodi Amasu; a otac Amasin bješe Jeter Ismailjac.
18 Kalebu mwana wa Hesroni akawa baba wa watoto wa Azubu mkewe, na Yeriothi. Wanawe walikuwa Yesheri, Shobabu, na Ardoni.
A Halev sin Esronov rodi s Azuvom ženom svojom i s Jeriotom sinove, i sinovi mu bjehu Jeser i Sovav i Ardon.
19 Azuba akafa, na Kalebu akamuoa Efrathi, aliye mzalia Huri.
A kad umrije Azuva, Halev se oženi Efratom, koja mu rodi Ora;
20 Huri akawa baba wa Uri, na Uri akawa baba wa Besaleli.
A Or rodi Uriju, a Urija rodi Veseleila.
21 Baadae Hesroni (alipo kuwa na miaka sitini) akamuoa binti wa Makiri, baba wa Gileadi. Akamzalia Segubu.
Potom otide Esron ka kæeri Mahira oca Galadova, i oženi se njom kad mu bijaše šezdeset godina, i ona mu rodi Seguva.
22 Segubu akawa baba wa Yairi, aliye miliki miji ishirini na mitatu katika nchi ya Gileadi.
A Seguv rodi Jaira, koji imaše dvadeset i tri grada u zemlji Galadskoj.
23 Geshuri na Aramu wakawapokonya miji ya Yairi na Kenathi, pamoja na miji sitini iliyo zunguka. Hawa wakazi wote walikuwa ni uzao wa Makiri, baba wa Gileadi.
Jer uze Gesurejima i Sircima sela Jairova i Kenat sa selima njegovijem, šezdeset gradova. To sve uzeše sinovi Mahira oca Galadova.
24 Baada ya kifo cha Hesroni, Kalebu akalala na Efrata, mke wa baba yake Hesroni. Akamzalia Ashuri, baba wa Tekoa.
I kad umrije Esron u Halev-Efrati, žena Esronova Avija rodi mu Ashora oca Tekojanima.
25 Wana wa Yerameeli, mzaliwa wa kwanza wa Hesroni, walikuwa ni Ramu mzaliwa wa kwanza, Buna, Oreni, Ozemu, na Ahiya.
A sinovi Jerameila prvenca Esronova bjehu: prvenac Aram, pa Vuna i Oren i Osem i Ahija.
26 Yerameeli alikuwa na mke mwingine, Jina lake lilikuwa Atara. Yeye alikuwa mama wa Onamu.
Imaše i drugu ženu Jerameilo, po imenu Ataru, ona je mati Onamova.
27 Wana wa Ramu, mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli, walikuwa Maasi, Yamini, na Ekeri.
A sinovi Arama prvenca Jerameilova bjehu: Mas i Jamin i Eker.
28 Wana wa Onamu walikuwa ni Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa ni Nadabu na Abishuri.
I sinovi Onamovi bjehu: Samaj i Jadaj; a sinovi Samajevi: Nadav i Avisur.
29 Jina la mke wa Abishuri lilikuwa Abihaili, na akamzalia Abani na Molidi.
I ime ženi Avisurovoj bješe Avihaila, koja mu rodi Avana i Molida.
30 Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa pasipo watoto.
A sinovi Nadavovi: Seled i Apaim; ali Seled umrije bez djece.
31 Mwana wa Apaimu alikuwa Ishi. Mwana wa Ishi alikuwa Sheshani. Mwana wa Sheshani alikuwa Alai.
A sinovi Apailovi: Jesej; a sinovi Jesejevi: Sisan, i kæi Sisanova Alaja.
32 Wana wa Yada, kaka yake Shamai, walikuwa Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa pasipo mtoto.
A sinovi Jadaja brata Samajeva: Jeter i Jonatan; ali Jeter umrije bez djece.
33 Wana wa Yonathani walikuwa Pelethi na Zaza. Hawa ndio uzao wa Yerameeli.
A sinovi Jonatanovi: Falet i Zaza. Ti bijahu sinovi Jerameilovi.
34 Sasa Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, bali wa kike pekee. Sheshani alikuwa na mtumishi, wa Kimisri, ambaye jina lake lilikuwa Yariha.
A Sisan ne imaše sinova nego kæeri; i imaše Sisan slugu Misirca po imenu Jaraju.
35 Sheshani alimkabidhi binti yake kwa Yariha mtumishi wake kama mke wake. Akamzalia Atai.
Zato Sisan dade kæer svoju Jaraji sluzi svojemu za ženu; a ona mu rodi Ataja.
36 Atai akawa baba wa Nathani, na Nathani akawa baba wa Zabadi.
A Ataj rodi Natana; a Natan rodi Zavada;
37 Zabadi akawa baba wa Efalali, na Afalali akawa baba wa Obedi.
A Zavad rodi Eflala; a Eflal rodi Ovida;
38 Obedi akawa baba wa Yehu, na Yehu akawa baba wa Azaria.
A Ovid rodi Juja; a Juj rodi Azariju;
39 Azaria akawa baba wa Helesi, na Helesi akawa baba wa Eleasa.
A Azarija rodi Helisa; a Helis rodi Eleasu;
40 Eleasa akawa baba wa Sismai, na Sismai akawa baba wa Shalumu.
A Eleasa rodi Sisamaja; a Sisamaj rodi Saluma;
41 Shalumu akawa baba wa Yekamia, na Yekamia akawa baba wa Elishama.
A Salum rodi Jekamiju; a Jekamija rodi Elisama.
42 Wana wa Kalebu, kaka yake Yerameeli, walikuwa ni Mesha mzaliwa wake wa kwanza, aliye kuwa baba wa Zifu. Mwanae wa pili, Maresha, allikuwa baba wa Hebroni.
A sinovi Haleva brata Jerameilova bjehu: Misa prvenac njegov, otac Zifejima; pa sinovi Marise oca Hevronova.
43 Wana wa Hebroni walikuwa Kora, Tapua, Rekemu, na Shema.
A sinovi Hevronovi: Korej i Tafuja i Rekem i Sema.
44 Shema akawa baba wa Rahamu, baba wa Yorkeamu. Rekemu akawa baba wa Shamai.
A Sema rodi Rama oca Jorkoamova; a Rekem rodi Samaja.
45 Mwana wa Shamai alikuwa Maoni, na Maoni alikuwa baba wa Bethsuri.
A sin Samajev bješe Maon, a taj Maon bi otac Vet-Suru.
46 Efa, suria wa Kalebu, alimza Harani, Mosa, na Gazezi. Harani akawa baba wa Gazezi.
I Gefa inoèa Halevova rodi Harana i Mosu i Gazesa.
47 Wana wa Yadai walikuwa Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa, na Shaafa.
A sinovi Jadajevi: Regem i Jotam i Gisan i Felet i Gefa i Sagaf.
48 Maaka, suria wa Kalebu, alimza Sheberi na Tirhana.
Maha inoèa Halevova rodi Severa i Tirhanu.
49 Pia akamza Shaafu baba wa Madmana, Sheva baba wa Makbena na baba wa Gibea. Binti wa Kalebu alikuwa Aksa. Hawa walikuwa uzao wa Kalebu.
Rodi i Sagafa oca Madmancima i Sevu oca Mahvincima i Gavajanima; a kæi Halevova bijaše Ahsa.
50 Hawa walikuwa wana wa Huri, mzaliwa wake wa kwanza kwa Efratha: Shobali baba wa Kiriath-Yearimu.
Ovo bijahu sinovi Haleva sina Ora prvenca Efratina; Soval otac Kirijat-Jarimu,
51 Salma baba wa Bethlehemu, na Harefu baba wa Beth-gaderi.
Salma otac Vitlejemu, Aref otac Vet-Gaderu.
52 Shobali baba wa kiriath-Yearimu alikuwa na uzao: Haroe, nusu ya watu Wamenuthite,
A imaše sinove Soval otac Kirijat-Jarimu: Aroja i Asi-Amenuhota.
53 na ukoo wa Kiriath-Yearimu: Waithri, Waputhi, Washumathi, na Wamishrai. Wasorathi na Waeshtaoli walitoka huku.
A porodice Kirijat-jarimske bjehu: Jetrani i Fuæani i Sumaæani i Misrajani. Od njih izidoše Saraæani i Estaoljani.
54 Ukoo wa Salma ulikuwa kama ufatao: Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, na nusu ya Wamenuhothi na Wazori,
Sinovi Salmini: Vitlejemci i Netofaæani, Ataroæani od doma Joavova, i Zorani, polovina Manahaæana,
55 ukoo wa waandishi walio ishi Yabesi: Watirathi, Washimeathi, na Wasukathi. Hawa walikuwa Wakeni walio toka katika uzao wa Hamathi, babu wa Warekabu.
I porodice pisarske u Javisu, Tiraæani, Simeaæani, Suhaæani; to su Keneji, koji se narodiše od Emata, oca doma Rihavova.

< 1 Nyakati 2 >