< 1 Nyakati 2 >

1 Hawa ndio wana wa Israeli: Reubeni, Simioni, Lawi, Yuda, Isakari, Zebuloni,
Filii autem Israel: Ruben, Simeon, Levi, Iuda, Issachar, et Zabulon,
2 Dani, Yusufu, Benyamini, Naftali, Gadi, na Asheri.
Dan, Ioseph, Beniamin, Nephthali, Gad et Aser.
3 Wana wa Yuda walikuwa Eri, Onani, na Shela, ambao walizaliwa na binti wa Shua, Wakanaani. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa muovu katika macho ya Yahweh, na Yahweh akamwua.
Filii Iuda: Her, Onan, et Sela. Hi tres nati sunt ei de filia Sue Chananitide. Fuit autem Her primogenitus Iuda, malus coram Domino, et occidit eum.
4 Tamari, mkwe wake, alimzalia Peresi na Zera. Yuda alikuwa na wana wa kiume wa tano.
Thamar autem nurus eius peperit ei Phares et Zara. Omnes ergo filii Iuda, quinque.
5 Wana wa Peresi walikuwa Hesroni na Hamuli.
Filii autem Phares: Hesron et Hamul.
6 Wana wa Zera walikuwa Zimri, Ethani, Hemani, Kalikoli na Darda, wote kwa jumla ni watano.
Filii quoque Zaræ: Zamri, et Ethan, et Eman, Chalchal quoque, et Dara, simul quinque.
7 Mwana wa Karmi alikuwa ni Akani, aliye leta taabu katika Israeli alipo iba kile kilicho hifadhiwa kwa ajili ya Mungu.
Filii Charmi: Achar, qui turbavit Israel, et peccavit in furto anathematis.
8 Mwana wa Ethani alikuwa Azaria.
Filii Ethan: Azarias.
9 Wana wa Hezroni walikuwa ni Yerameeli, Ramu, na Kalebu.
Filii autem Hesron qui nati sunt ei: Ierameel, et Ram, et Calubi.
10 Ramu akawa baba wa Aminadabu, na Aminadabu akawa baba wa Nashoni, kiongozi miongoni uzao wa Yuda.
Porro Ram genuit Aminadab. Aminadab autem genuit Nahasson, principem filiorum Iuda.
11 Nashoni akawa baba wa Salmoni, na Salmon akawa baba wa Boazi.
Nahasson quoque genuit Salma, de quo ortus est Booz.
12 Boazi akawa baba wa Obedi, na Obedi akawa baba wa Yese.
Booz vero genuit Obed, qui et ipse genuit Isai.
13 Yese akawa baba wa mzaliwa wake wa kwanza Eliabu, wa pili Abinadabu, wa tatu Shama.
Isai autem genuit primogenitum Eliab, secundum Abinadab, tertium Simmaa,
14 Nethaneli wa nne, Radai wa tano.
quartum Nathanael, quintum Raddai,
15 Ozemu wa sita, na Daudi wa saba.
sextum Asom, septimum David.
16 Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa Abishai, Yoabu, na Asaheli, jumla watatu.
Quorum sorores fuerunt Sarvia, et Abigail. Filii Sarviæ: Abisai, Ioab, et Asael, tres.
17 Abigali akamzaa Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri Mwishmaeli.
Abigail autem genuit Amasa, cuius pater fuit Iether Ismahelites.
18 Kalebu mwana wa Hesroni akawa baba wa watoto wa Azubu mkewe, na Yeriothi. Wanawe walikuwa Yesheri, Shobabu, na Ardoni.
Caleb vero filius Hesron accepit uxorem nomine Azuba, de qua genuit Ierioth: fueruntque filii eius Iaser, et Sobab, et Ardon.
19 Azuba akafa, na Kalebu akamuoa Efrathi, aliye mzalia Huri.
Cumque mortua fuisset Azuba, accepit uxorem Caleb, Ephratha: quæ peperit ei Hur.
20 Huri akawa baba wa Uri, na Uri akawa baba wa Besaleli.
Porro Hur genuit Uri: et Uri genuit Bezeleel.
21 Baadae Hesroni (alipo kuwa na miaka sitini) akamuoa binti wa Makiri, baba wa Gileadi. Akamzalia Segubu.
Post hæc ingressus est Hesron ad filiam Machir patris Galaad, et accepit eam cum esset annorum sexaginta: quæ peperit ei Segub.
22 Segubu akawa baba wa Yairi, aliye miliki miji ishirini na mitatu katika nchi ya Gileadi.
Sed et Segub genuit Iair, et possedit viginti tres civitates in Terra Galaad.
23 Geshuri na Aramu wakawapokonya miji ya Yairi na Kenathi, pamoja na miji sitini iliyo zunguka. Hawa wakazi wote walikuwa ni uzao wa Makiri, baba wa Gileadi.
Cepitque Gessur, et Aram oppida Iair, et Canath, et viculos eius sexaginta civitatum. Omnes isti, filii Machir patris Galaad.
24 Baada ya kifo cha Hesroni, Kalebu akalala na Efrata, mke wa baba yake Hesroni. Akamzalia Ashuri, baba wa Tekoa.
Cum autem mortuus esset Hesron, ingressus est Caleb ad Ephratha. Habuit quoque Hesron uxorem Abia, quæ peperit ei Assur patrem Thecuæ.
25 Wana wa Yerameeli, mzaliwa wa kwanza wa Hesroni, walikuwa ni Ramu mzaliwa wa kwanza, Buna, Oreni, Ozemu, na Ahiya.
Nati sunt autem filii Ierameel primogeniti Hesron, Ram primogenitus eius, et Buna, et Aram, et Asom, et Achia.
26 Yerameeli alikuwa na mke mwingine, Jina lake lilikuwa Atara. Yeye alikuwa mama wa Onamu.
Duxit quoque uxorem alteram Ierameel, nomine Atara, quæ fuit mater Onam.
27 Wana wa Ramu, mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli, walikuwa Maasi, Yamini, na Ekeri.
Sed et filii Ram primogeniti Ierameel, fuerunt Moos, Iamin, et Achar.
28 Wana wa Onamu walikuwa ni Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa ni Nadabu na Abishuri.
Onam autem habuit filios Semei, et Iada. Filii autem Semei: Nadab, et Abisur.
29 Jina la mke wa Abishuri lilikuwa Abihaili, na akamzalia Abani na Molidi.
Nomen vero uxoris Abisur, Abihail, quæ peperit ei Ahobban, et Molid.
30 Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa pasipo watoto.
Filii autem Nadab fuerunt Saled, et Apphaim. Mortuus est autem Saled absque liberis.
31 Mwana wa Apaimu alikuwa Ishi. Mwana wa Ishi alikuwa Sheshani. Mwana wa Sheshani alikuwa Alai.
Filius vero Apphaim, Iesi: qui Iesi genuit Sesan. Porro Sesan genuit Oholai.
32 Wana wa Yada, kaka yake Shamai, walikuwa Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa pasipo mtoto.
Filii autem Iada fratris Semei: Iether, et Ionathan. Sed et Iether mortuus est absque liberis.
33 Wana wa Yonathani walikuwa Pelethi na Zaza. Hawa ndio uzao wa Yerameeli.
Porro Ionathan genuit Phaleth, et Ziza. Isti fuerunt filii Ierameel.
34 Sasa Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, bali wa kike pekee. Sheshani alikuwa na mtumishi, wa Kimisri, ambaye jina lake lilikuwa Yariha.
Sesan autem non habuit filios, sed filias: et servum Ægyptium nomine Ieraa.
35 Sheshani alimkabidhi binti yake kwa Yariha mtumishi wake kama mke wake. Akamzalia Atai.
Deditque ei filiam suam uxorem: quæ peperit ei Ethei.
36 Atai akawa baba wa Nathani, na Nathani akawa baba wa Zabadi.
Ethei autem genuit Nathan, et Nathan genuit Zabad.
37 Zabadi akawa baba wa Efalali, na Afalali akawa baba wa Obedi.
Zabad quoque genuit Ophlal, et Ophlal genuit Obed.
38 Obedi akawa baba wa Yehu, na Yehu akawa baba wa Azaria.
Obed genuit Iehu, Iehu genuit Azariam.
39 Azaria akawa baba wa Helesi, na Helesi akawa baba wa Eleasa.
Azarias genuit Helles, et Helles genuit Elasa.
40 Eleasa akawa baba wa Sismai, na Sismai akawa baba wa Shalumu.
Elasa genuit Sisamoi, Sisamoi genuit Sellum.
41 Shalumu akawa baba wa Yekamia, na Yekamia akawa baba wa Elishama.
Sellum genuit Icamiam, Icamia autem genuit Elisama.
42 Wana wa Kalebu, kaka yake Yerameeli, walikuwa ni Mesha mzaliwa wake wa kwanza, aliye kuwa baba wa Zifu. Mwanae wa pili, Maresha, allikuwa baba wa Hebroni.
Filii autem Caleb fratris Ierameel: Mesa primogenitus eius, ipse est pater Ziph: et filii Maresa patris Hebron.
43 Wana wa Hebroni walikuwa Kora, Tapua, Rekemu, na Shema.
Porro filii Hebron, Core, et Taphua, et Recem, et Samma.
44 Shema akawa baba wa Rahamu, baba wa Yorkeamu. Rekemu akawa baba wa Shamai.
Samma autem genuit Raham, patrem Iercaam, et Recem genuit Sammai.
45 Mwana wa Shamai alikuwa Maoni, na Maoni alikuwa baba wa Bethsuri.
Filius Sammai, Maon: et Maon pater Bethsur.
46 Efa, suria wa Kalebu, alimza Harani, Mosa, na Gazezi. Harani akawa baba wa Gazezi.
Epha autem concubina Caleb peperit Haran, et Mosa, et Gezez. Porro Haran genuit Gezez.
47 Wana wa Yadai walikuwa Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa, na Shaafa.
Filii autem Iahaddai, Regom, et Ioathan, et Gesan, et Phalet, et Epha, et Saaph.
48 Maaka, suria wa Kalebu, alimza Sheberi na Tirhana.
Concubina Caleb Maacha, peperit Saber, et Tharana.
49 Pia akamza Shaafu baba wa Madmana, Sheva baba wa Makbena na baba wa Gibea. Binti wa Kalebu alikuwa Aksa. Hawa walikuwa uzao wa Kalebu.
Genuit autem Saaph pater Madmena, Sue patrem Machbena, et patrem Gabaa. Filia vero Caleb, fuit Achsa.
50 Hawa walikuwa wana wa Huri, mzaliwa wake wa kwanza kwa Efratha: Shobali baba wa Kiriath-Yearimu.
Hi erant filii Caleb, filii Hur primogeniti Ephratha, Sobal pater Cariathiarim.
51 Salma baba wa Bethlehemu, na Harefu baba wa Beth-gaderi.
Salma pater Bethlehem, Hariph pater Bethgader.
52 Shobali baba wa kiriath-Yearimu alikuwa na uzao: Haroe, nusu ya watu Wamenuthite,
Fuerunt autem filii Sobal patris Cariathiarim, qui videbat dimidium requietionum.
53 na ukoo wa Kiriath-Yearimu: Waithri, Waputhi, Washumathi, na Wamishrai. Wasorathi na Waeshtaoli walitoka huku.
Et de cognatione Cariathiarim, Iethrei, et Aphuthei, et Semathei, et Maserei. Ex his egressi sunt Saraitæ, et Esthaolitæ.
54 Ukoo wa Salma ulikuwa kama ufatao: Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, na nusu ya Wamenuhothi na Wazori,
Filii Salma, Bethlehem, et Netophathi, Coronæ domus Ioab, et dimidium requietionis Sarai,
55 ukoo wa waandishi walio ishi Yabesi: Watirathi, Washimeathi, na Wasukathi. Hawa walikuwa Wakeni walio toka katika uzao wa Hamathi, babu wa Warekabu.
cognationes quoque scribarum habitantium in Iabes, canentes atque resonantes, et in tabernaculis commorantes. Hi sunt Cinæi, qui venerunt de Calore patris domus Rechab.

< 1 Nyakati 2 >