< 1 Nyakati 2 >

1 Hawa ndio wana wa Israeli: Reubeni, Simioni, Lawi, Yuda, Isakari, Zebuloni,
Voici les enfants d’Israël: Ruben, Siméon, Lévi, Juda, Issachar et Zabulon,
2 Dani, Yusufu, Benyamini, Naftali, Gadi, na Asheri.
Dan, Joseph et Benjamin, Nephtali, Gad et Aser.
3 Wana wa Yuda walikuwa Eri, Onani, na Shela, ambao walizaliwa na binti wa Shua, Wakanaani. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa muovu katika macho ya Yahweh, na Yahweh akamwua.
Enfants de Juda: Er, Onân et Chêla; ces trois lui naquirent de la fille de Choua, la Cananéenne. Er, le premier-né de Juda, ayant déplu au Seigneur, le Seigneur le fit mourir.
4 Tamari, mkwe wake, alimzalia Peresi na Zera. Yuda alikuwa na wana wa kiume wa tano.
Tamar, sa bru, lui enfanta Péreç et Zérah. Total des fils de Juda: cinq.
5 Wana wa Peresi walikuwa Hesroni na Hamuli.
Les fils de Péreç furent Heçrôn et Hamoul.
6 Wana wa Zera walikuwa Zimri, Ethani, Hemani, Kalikoli na Darda, wote kwa jumla ni watano.
Fils de Zérah: Zimri, Ethân, Hêmân, Kalkol, Dara, en tout cinq.
7 Mwana wa Karmi alikuwa ni Akani, aliye leta taabu katika Israeli alipo iba kile kilicho hifadhiwa kwa ajili ya Mungu.
Fils de Carmi: Akhar, qui affligea Israël en violant l’anathème.
8 Mwana wa Ethani alikuwa Azaria.
Fils d’Ethân: Azaria.
9 Wana wa Hezroni walikuwa ni Yerameeli, Ramu, na Kalebu.
Fils de Heçrôn, qui lui naquirent: Yerahmeêl, Râm et Keloubaï.
10 Ramu akawa baba wa Aminadabu, na Aminadabu akawa baba wa Nashoni, kiongozi miongoni uzao wa Yuda.
Râm engendra Amminadab, et Amminadab Nahchôn, prince des enfants de Juda.
11 Nashoni akawa baba wa Salmoni, na Salmon akawa baba wa Boazi.
Nahchôn engendra Salmâ, et Salmâ Booz.
12 Boazi akawa baba wa Obedi, na Obedi akawa baba wa Yese.
Booz engendra Obed, et Obed Jessé.
13 Yese akawa baba wa mzaliwa wake wa kwanza Eliabu, wa pili Abinadabu, wa tatu Shama.
Jessé engendra comme premier-né Elïab, Abinadab deuxième, Chimea troisième,
14 Nethaneli wa nne, Radai wa tano.
Nethanel quatrième, Raddaï cinquième,
15 Ozemu wa sita, na Daudi wa saba.
Ocem sixième, David septième.
16 Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa Abishai, Yoabu, na Asaheli, jumla watatu.
Leurs sœurs étaient Cerouya et Abigaïl; les fils de Cerouya: Abchaï, Joab, Assahel, en tout trois.
17 Abigali akamzaa Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri Mwishmaeli.
Abigaïl enfanta Amassa. Amassa avait pour père Yéter, l’Ismaélite.
18 Kalebu mwana wa Hesroni akawa baba wa watoto wa Azubu mkewe, na Yeriothi. Wanawe walikuwa Yesheri, Shobabu, na Ardoni.
Caleb, fils de Heçrôn, eut des enfants d’Azouba, sa femme, et de Yerioth. Les enfants de la première furent: Yêcher, Chobab et Ardôn.
19 Azuba akafa, na Kalebu akamuoa Efrathi, aliye mzalia Huri.
Azouba étant morte, Caleb épousa Efrath, et celle-ci lui enfanta Hour.
20 Huri akawa baba wa Uri, na Uri akawa baba wa Besaleli.
Hour engendra Ouri, et Ouri Beçalêl.
21 Baadae Hesroni (alipo kuwa na miaka sitini) akamuoa binti wa Makiri, baba wa Gileadi. Akamzalia Segubu.
Ensuite Heçrôn eut commerce avec une fille de Makhir, père de Ghilad, qu’il avait épousée à l’âge de soixante ans. Elle lui enfanta Segoub.
22 Segubu akawa baba wa Yairi, aliye miliki miji ishirini na mitatu katika nchi ya Gileadi.
Segoub engendra Yaïr, qui posséda vingt-trois villes dans le pays de Galaad.
23 Geshuri na Aramu wakawapokonya miji ya Yairi na Kenathi, pamoja na miji sitini iliyo zunguka. Hawa wakazi wote walikuwa ni uzao wa Makiri, baba wa Gileadi.
Ghechour et Aram leur enlevèrent les bourgs de Yaïr, avec Kenath et ses bourgs, en tout soixante villes. Tous ceux-là étaient fils de Makhir, père de Ghilad.
24 Baada ya kifo cha Hesroni, Kalebu akalala na Efrata, mke wa baba yake Hesroni. Akamzalia Ashuri, baba wa Tekoa.
Après la mort de Heçrôn à Caleb d’Efrath, la femme de Heçron, Abiyya, lui enfanta Achhour, le père de Tekoa.
25 Wana wa Yerameeli, mzaliwa wa kwanza wa Hesroni, walikuwa ni Ramu mzaliwa wa kwanza, Buna, Oreni, Ozemu, na Ahiya.
Les fils de Yerahmeêl, le premier-né de Heçron, furent Râm, l’aîné, Bouna, Orén, Ocem, nés d’ Ahiyya.
26 Yerameeli alikuwa na mke mwingine, Jina lake lilikuwa Atara. Yeye alikuwa mama wa Onamu.
Yerahmeêl eut une autre femme, du nom d’Atara. Ce fut la mère d’Onam.
27 Wana wa Ramu, mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli, walikuwa Maasi, Yamini, na Ekeri.
Les fils de Râm, le premier-né de Yerahmeêl, furent: Maaç, Yamîn et Eker.
28 Wana wa Onamu walikuwa ni Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa ni Nadabu na Abishuri.
Les fils d’Onam furent Chammaï et Yada, ceux de Chammaï: Nadab et Abichour.
29 Jina la mke wa Abishuri lilikuwa Abihaili, na akamzalia Abani na Molidi.
La femme d’Abichour, qui s’appelait Abihaïl, lui enfanta Ahbân et Molid.
30 Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa pasipo watoto.
Les fils de Nadab furent Séled et Appaïm. Séled mourut sans enfants.
31 Mwana wa Apaimu alikuwa Ishi. Mwana wa Ishi alikuwa Sheshani. Mwana wa Sheshani alikuwa Alai.
Les enfants d’Appaïm furent Yicheï, de celui-ci Chêchân, de celui-ci Ahlaï.
32 Wana wa Yada, kaka yake Shamai, walikuwa Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa pasipo mtoto.
Les fils de Yada, frère de Chammaï, furent Yéter et Jonathan. Yéter mourut sans enfants.
33 Wana wa Yonathani walikuwa Pelethi na Zaza. Hawa ndio uzao wa Yerameeli.
Les fils de Jonathan furent: Péleth et Zaza. Tels furent les descendants de Yerahmeêl.
34 Sasa Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, bali wa kike pekee. Sheshani alikuwa na mtumishi, wa Kimisri, ambaye jina lake lilikuwa Yariha.
Chêchân n’avait pas de fils, mais seulement des filles. Ayant un esclave égyptien du nom de Yarha,
35 Sheshani alimkabidhi binti yake kwa Yariha mtumishi wake kama mke wake. Akamzalia Atai.
Chêchân donna en mariage sa fille à ce Yarha, son esclave, et elle lui enfanta Attaï.
36 Atai akawa baba wa Nathani, na Nathani akawa baba wa Zabadi.
Attaï engendra Nathan, et celui-ci Zabad.
37 Zabadi akawa baba wa Efalali, na Afalali akawa baba wa Obedi.
Zabad engendra Eflâl, et celui-ci Obed.
38 Obedi akawa baba wa Yehu, na Yehu akawa baba wa Azaria.
Obed engendra Jéhu et celui-ci Azaria.
39 Azaria akawa baba wa Helesi, na Helesi akawa baba wa Eleasa.
Azaria engendra Héleç, et celui-ci Elassa.
40 Eleasa akawa baba wa Sismai, na Sismai akawa baba wa Shalumu.
Elassa engendra Sismaï et celui-ci Challoum.
41 Shalumu akawa baba wa Yekamia, na Yekamia akawa baba wa Elishama.
Challoum engendra Yekamia, et celui-ci Elichama.
42 Wana wa Kalebu, kaka yake Yerameeli, walikuwa ni Mesha mzaliwa wake wa kwanza, aliye kuwa baba wa Zifu. Mwanae wa pili, Maresha, allikuwa baba wa Hebroni.
Les fils de Caleb, frère de Yerahmeêl, furent: Mêcha, son premier-né, le père de Zif, et Marêcha, son autre fils, le père de Hébron.
43 Wana wa Hebroni walikuwa Kora, Tapua, Rekemu, na Shema.
Les fils de Hébron furent: Korah, Tappouah, Rékem et Chéma.
44 Shema akawa baba wa Rahamu, baba wa Yorkeamu. Rekemu akawa baba wa Shamai.
Chéma engendra Raham, le père de Yorkeam, et Rékem engendra Chammaï.
45 Mwana wa Shamai alikuwa Maoni, na Maoni alikuwa baba wa Bethsuri.
Le fils de Chammaï fut Maôn, et Maôn fut le père de Bêth-Çour.
46 Efa, suria wa Kalebu, alimza Harani, Mosa, na Gazezi. Harani akawa baba wa Gazezi.
Efa, concubine de Caleb, enfanta Harân et Moça (et Gazêz). Harân enfanta Gazêz.
47 Wana wa Yadai walikuwa Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa, na Shaafa.
Les enfants de Yéhdaï furent: Réghem, Jotham, Ghêchân, Pélét, Efa et Chaaf.
48 Maaka, suria wa Kalebu, alimza Sheberi na Tirhana.
Une autre concubine de Caleb, nommée Maakha, enfanta Chéber et Tirhana.
49 Pia akamza Shaafu baba wa Madmana, Sheva baba wa Makbena na baba wa Gibea. Binti wa Kalebu alikuwa Aksa. Hawa walikuwa uzao wa Kalebu.
Elle enfanta Chaaf, le père de Madmanna, Cheva, le père de Makhbèna et le père de Ghibea. La fille de Caleb était Akhsa.
50 Hawa walikuwa wana wa Huri, mzaliwa wake wa kwanza kwa Efratha: Shobali baba wa Kiriath-Yearimu.
Caleb, fils de Hour, premier-né d’Efrata, eut pour fils: Chobal, le père de Kiryat-Yearim,
51 Salma baba wa Bethlehemu, na Harefu baba wa Beth-gaderi.
Salma, le père de Bethléem, Harêf, le père de Bêth-Ghédêr.
52 Shobali baba wa kiriath-Yearimu alikuwa na uzao: Haroe, nusu ya watu Wamenuthite,
Chobal, le père de Kiryat-Yearim, eut des enfants: Haroé, Haci-Hammenouhoth.
53 na ukoo wa Kiriath-Yearimu: Waithri, Waputhi, Washumathi, na Wamishrai. Wasorathi na Waeshtaoli walitoka huku.
Les familles de Kiryat-Yearim furent: le Yitrien, le Poutien, le Choumatien et le Michraïen. D’Eux essaimèrent le Çoratien et l’Echtaoulien.
54 Ukoo wa Salma ulikuwa kama ufatao: Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, na nusu ya Wamenuhothi na Wazori,
Les enfants de Salma furent Bethléem, le Netofatien, Atroth, Bêth-Yoab, le Haci-Hammanahtien, le Çorien.
55 ukoo wa waandishi walio ishi Yabesi: Watirathi, Washimeathi, na Wasukathi. Hawa walikuwa Wakeni walio toka katika uzao wa Hamathi, babu wa Warekabu.
Les familles des scribes qui demeuraient à Yabêç étaient les Tiratiens, les Chimatiens et les Soukatiens. C’Étaient les Kéniens, issus de Hamath, le père de Bêth-Rêkhab.

< 1 Nyakati 2 >