< Sefania 1 >

1 Neno la Bwana lililomjia Sefania mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria, mwana wa Hezekia, wakati wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda:
La parole de l'Éternel, qui fut adressée à Sophonie, fils de Cushi, fils de Guédalia, fils d'Amaria, fils d'Ézéchias, aux jours de Josias, fils d'Amon, roi de Juda.
2 Bwana asema, “Nitafagia kila kitu kutoka kwenye uso wa dunia.”
Je ferai périr entièrement toutes choses sur la face de la terre, dit l'Éternel.
3 “Nitafagilia mbali watu na wanyama; nitafagilia mbali ndege wa angani na samaki wa baharini. Wafanyao maovu watapata tu kokoto, nami nitamkatilia mbali mwanadamu atoke katika dunia,” asema Bwana.
Je ferai périr les hommes et les bêtes; je ferai périr les oiseaux du ciel et les poissons de la mer; j'enlèverai les scandales avec les méchants, et je retrancherai les hommes de la face de la terre, dit l'Éternel.
4 “Nitaiadhibu Yuda na wote wakaao Yerusalemu. Kutoka mahali hapa nitakatilia mbali kila mabaki ya Baali, majina ya wapagani na makuhani waabuduo sanamu:
J'étendrai ma main sur Juda et sur tous les habitants de Jérusalem; et je retrancherai de ce lieu le reste de Baal, et le nom de ses prêtres avec les sacrificateurs,
5 wale ambao husujudu juu ya mapaa kuabudu jeshi la vitu vya angani, wale ambao husujudu na kuapa kwa Bwana na ambao pia huapa kwa Malkamu,
Et ceux qui se prosternent sur les toits devant l'armée des cieux, et ceux qui se prosternent en jurant par l'Éternel, et qui jurent aussi par leur roi,
6 wale wanaoacha kumfuata Bwana, wala hawamtafuti Bwana wala kutaka shauri lake.
Et ceux qui se détournent de l'Éternel, et ceux qui ne cherchent pas l'Éternel et ne s'enquièrent pas de lui.
7 Nyamazeni mbele za Bwana Mwenyezi, kwa maana siku ya Bwana iko karibu. Bwana ameandaa dhabihu, amewaweka wakfu wale aliowaalika.
Tais-toi devant le Seigneur, l'Éternel! Car le jour de l'Éternel est proche; l'Éternel a préparé un sacrifice, il a sanctifié ses conviés.
8 Katika siku ya dhabihu ya Bwana nitawaadhibu wakuu na wana wa mfalme na wale wote wanaovaa nguo za kigeni.
Et au jour du sacrifice de l'Éternel, je châtierai les princes, et les fils du roi, et tous ceux qui revêtent des vêtements étrangers.
9 Katika siku hiyo nitaadhibu wote ambao hukwepa kukanyaga kizingiti, ambao hujaza hekalu la miungu yao kwa dhuluma na udanganyifu.”
Et je châtierai, en ce jour-là, tous ceux qui sautent par-dessus le seuil, ceux qui remplissent la maison de leur Seigneur de violence et de fraude.
10 Bwana asema, “Katika siku hiyo kilio kitapanda juu kutoka lango la Samaki, maombolezo kutoka mtaa wa pili, na mshindo mkubwa kutoka vilimani.
En ce jour-là, dit l'Éternel, on entendra des cris à la porte des Poissons, des hurlements dans la seconde partie de la ville, et un grand désastre sur les collines.
11 Ombolezeni, ninyi mnaoishi katika eneo la sokoni; wafanyabiashara wenu wote wameangamizwa, wote ambao wanafanya biashara ya fedha wataangamizwa.
Lamentez-vous, habitants de Macthesh! Car tous ceux qui trafiquent sont détruits, tous ces gens chargés d'argent sont exterminés!
12 Wakati huo nitasaka mji wa Yerusalemu kwa taa, na kuwaadhibu wale ambao wanakaa katika hali ya kuridhika, ambao ni kama divai iliyobaki kwenye machicha, ambao hudhani, ‘Bwana hatafanya lolote, jema au baya.’
Et il arrivera, en ce temps-là, que je fouillerai Jérusalem avec des lampes, et que je châtierai ces hommes qui se figent sur leurs lies, et qui disent dans leur cœur: L'Éternel ne fera ni bien ni mal.
13 Utajiri wao utatekwa nyara, nyumba zao zitabomolewa. Watajenga nyumba, lakini hawataishi ndani yake; watapanda mizabibu lakini hawatakunywa divai yake.
Leurs biens seront au pillage, et leurs maisons en désolation; ils auront bâti des maisons, mais ils n'y habiteront point; ils auront planté des vignes, mais ils n'en boiront pas le vin.
14 “Siku kubwa ya Bwana iko karibu: iko karibu na inakuja haraka. Sikilizeni! Kilio katika siku ya Bwana kitakuwa kichungu, hata shujaa atapiga kelele.
Le grand jour de l'Éternel est proche; il est proche, et vient en toute hâte. La voix du jour de l'Éternel retentit; là l'homme vaillant lui-même pousse des cris amers.
15 Siku ile ni siku ya ghadhabu, siku ya fadhaa na dhiki, siku ya uharibifu na ukiwa, siku ya giza na utusitusi, siku ya mawingu na giza nene,
C'est un jour de colère que ce jour-là; un jour de détresse et d'angoisse, un jour de ruine et de désolation, un jour de ténèbres et d'obscurité, un jour de nuées et de brouillards,
16 siku ya tarumbeta na mlio wa vita dhidi ya miji yenye ngome na dhidi ya minara mirefu.
Un jour de trompettes et d'alarmes contre les villes fortes et contre les hautes tours.
17 Nitawaletea watu dhiki, nao watatembea kama vipofu, kwa sababu wametenda dhambi dhidi ya Bwana. Damu yao itamwagwa kama vumbi na matumbo yao kama taka.
Je mettrai les hommes dans la détresse, et ils marcheront comme des aveugles, parce qu'ils ont péché contre l'Éternel. Leur sang sera répandu comme de la poussière, et leur chair comme de l'ordure.
18 Fedha yao wala dhahabu yao hazitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya ghadhabu ya Bwana. Katika moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa, kwa maana ataleta mwisho wa wote wanaoishi katika dunia ghafula.”
Ni leur argent, ni leur or ne pourront les délivrer au jour de la colère de l'Éternel; et par le feu de sa jalousie tout le pays sera consumé; car c'est d'une entière destruction, c'est d'une ruine soudaine qu'il frappera tous les habitants de la terre.

< Sefania 1 >