< Zekaria 3 >

1 Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, akiwa amesimama mbele ya malaika wa Bwana, naye Shetani amesimama upande wake wa kuume ili amshtaki.
And the Lord showed me Jesus the high priest standing before the angel of the Lord, and the Devil stood on his right hand to resist him.
2 Bwana akamwambia Shetani, “Bwana akukemee Shetani! Bwana, ambaye ameichagua Yerusalemu, akukemee! Je, mtu huyu siyo kijinga kinachowaka kilichonyakuliwa kwenye moto?”
And the Lords said to the Devil, The Lord rebuke you, O Devil, even the Lord that has chosen Jerusalem rebuke you: behold! is not this as a brand plucked from the fire?
3 Wakati huu, Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu alipokuwa amesimama mbele ya malaika.
Now Jesus was clothed in filthy raiment, and stood before the angel.
4 Malaika akawaambia wale waliokuwa wamesimama mbele yake, “Mvueni hizo nguo zake chafu.” Kisha akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeiondoa dhambi yako, nami nitakuvika mavazi ya kitajiri.”
And [the Lord] answered and spoke to those who stood before him, saying, Take away the filthy raiment from him: and he said to him, Behold, I have taken away your iniquities: and clothe you him with a long robe,
5 Kisha nikasema, “Mvike kilemba kilicho safi kichwani mwake.” Kwa hiyo wakamvika kilemba safi kichwani na kumvika yale mavazi mengine, wakati malaika wa Bwana akiwa amesimama karibu.
and place a pure mitre upon his head. So they placed a pure mitre upon his head, and clothed him with garments: and the angel of the Lord stood [by].
6 Malaika wa Bwana akamwamuru Yoshua:
And the angel of the Lord testified to Jesus, saying,
7 “Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Ikiwa utakwenda katika njia zangu na kushika masharti yangu, basi utaitawala nyumba yangu na kuwa na amri juu ya nyua zangu, nami nitakupa nafasi miongoni mwa hawa wasimamao hapa.
Thus says the Lord Almighty; If you will walk in my ways, and take heed to my charges, then shall you judge my house: and if you will diligently keep my court, then will I give you men to walk in the midst of these that stand [here].
8 “‘Sikiliza, ee Yoshua kuhani mkuu, pamoja na wenzako walioketi mbele yako, ambao ni watu walio ishara ya mambo yatakayokuja: Ninakwenda kumleta mtumishi wangu, Tawi.
Hear now, Jesus the high priest, you, and your neighbors that are sitting before [you]: for they are diviners, for, behold, I bring forth my servant The Branch.
9 Tazama, jiwe nililoliweka mbele ya Yoshua! Kuna macho saba juu ya jiwe lile moja, nami nitachora maandishi juu yake,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitaiondoa dhambi ya nchi hii kwa siku moja.
For [as for] the stone which I have set before the face of Jesus, on the one stone are seven eyes: behold, I am digging a trench, says the Lord Almighty, and I will search out all the iniquity of that land in one day.
10 “‘Katika siku hiyo kila mmoja wenu atamwalika jirani yake akae chini ya mzabibu wake na mtini wake,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”
In that day, says the Lord Almighty, you shall call together every man his neighbor under the vine and under the fig tree.

< Zekaria 3 >