< Zekaria 2 >

1 Kisha nikatazama juu: pale mbele yangu alikuwepo mtu mwenye kamba ya kupimia mkononi mwake!
I lifted up my eyes, and saw, and look, a man with a measuring line in his hand.
2 Nikamuuliza, “Unakwenda wapi?” Akanijibu, “Kupima Yerusalemu, kupata urefu na upana wake.”
Then I asked, "Where are you going?" He said to me, "To measure Jerusalem, to see what is its breadth and what is its length."
3 Kisha malaika aliyekuwa akizungumza nami akaondoka, malaika mwingine akaja kukutana naye
Look, the angel who talked with me went forth, and another angel went out to meet him,
4 na kumwambia: “Kimbia, umwambie yule kijana, ‘Yerusalemu utakuwa mji usio na kuta kwa sababu ya wingi wa watu na mifugo iliyomo.
and said to him, "Run, speak to this young man, saying, 'Jerusalem will be inhabited as villages without walls, because of the multitude of men and livestock in it.
5 Mimi mwenyewe nitakuwa ukuta wa moto kuuzunguka,’ asema Bwana, ‘nami nitakuwa utukufu wake ndani yake.’
For I,' says Jehovah, 'will be to her a wall of fire around it, and I will be the glory in the midst of her.
6 “Njooni! Njooni! Kimbieni mtoke katika nchi ya kaskazini,” asema Bwana, “Kwa kuwa nimewatawanya kwenye pande nne za mbingu,” asema Bwana.
Come. Come. Flee from the land of the north,' says Jehovah; 'for I have spread you abroad as the four winds of the sky,' says Jehovah.
7 “Njoo, ee Sayuni! Kimbia, wewe ukaaye ndani ya Binti Babeli!”
'Come, Zion. Escape, you who dwell with the daughter of Babylon.'
8 Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Baada ya yeye kuniheshimu na kunituma mimi dhidi ya mataifa yaliyokuteka nyara, kwa kuwa yeyote awagusaye ninyi, anaigusa mboni ya jicho lake,
For thus says Jehovah of hosts: 'For honor he has sent me to the nations which plundered you; for he who touches you touches the apple of my eye.
9 hakika nitauinua mkono wangu dhidi yao ili watumwa wao wawateke nyara. Ndipo mtakapojua ya kwamba Bwana Mwenye Nguvu Zote amenituma.
For, look, I will shake my hand over them, and they will be a spoil to those who served them; and you will know that Jehovah of hosts has sent me.
10 “Piga kelele na ufurahie, ee Binti Sayuni, kwa maana ninakuja, nami nitaishi miongoni mwenu,” asema Bwana.
Sing and rejoice, daughter of Zion; for, look, I come, and I will dwell in the midst of you,' says Jehovah.
11 “Mataifa mengi yataunganishwa na Bwana siku hiyo, nao watakuwa watu wangu. Nitaishi miongoni mwenu nanyi mtajua kwamba Bwana Mwenye Nguvu Zote amenituma kwenu.
Many nations shall join themselves to Jehovah in that day, and shall be my people; and I will dwell in the midst of you, and you shall know that Jehovah of hosts has sent me to you.
12 Bwana atairithi Yuda kama fungu lake katika nchi takatifu na atachagua tena Yerusalemu.
Jehovah will inherit Judah as his portion in the holy land, and will again choose Jerusalem.
13 Tulieni mbele za Bwana, enyi watu wote, kwa sababu ameinuka kutoka makao yake matakatifu.”
Be silent, all flesh, before Jehovah; for he has roused himself from his holy habitation."

< Zekaria 2 >