< Zekaria 1 >

1 Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:
Le huitième mois de la seconde année de Darius, la parole de l'Eternel fut [adressée] à Zacharie, fils de Barachie, fils d'Hiddo, le Prophète, en disant:
2 “Bwana aliwakasirikia sana baba zako wa zamani.
L'Eternel a été extrêmement indigné contre vos pères.
3 Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
C'est pourquoi tu leur diras: Ainsi a dit l'Eternel des armées: Retournez-vous vers moi, dit l'Eternel des armées; et je me retournerai vers vous, dit l'Eternel des armées.
4 Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema Bwana.
Ne soyez point comme vos pères, auxquels les Prophètes qui ont été ci-devant criaient, en disant: Ainsi a dit l'Eternel des armées: Détournez-vous maintenant de votre mauvais train, et de vos mauvaises actions; mais ils n'ont pas écouté, et n'ont pas été attentifs à ce que je leur disais, dit l'Eternel.
5 Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele?
Vos pères où sont-ils? Et ces Prophètes-là devaient-ils vivre à toujours?
6 Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?” “Kisha walitubu na kusema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’”
Cependant mes paroles et mes ordonnances que j'avais enjointes aux Prophètes mes serviteurs, n'ont-elles pas atteint vos pères? De sorte que, s'étant convertis, ils ont dit: Comme l'Eternel des armées avait pensé de nous faire selon notre train, et selon nos actions, ainsi nous a-t-il fait.
7 Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.
Le vingt-quatrième jour du onzième mois, qui est le mois de Sébat, en la seconde année de Darius, la parole de l'Eternel fut [adressée] à Zacharie, fils de Barachie, fils d'Hiddo, le Prophète, comme s'ensuit.
8 Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.
J'eus de nuit une vision: et voici, un homme était monté sur un cheval roux, et il se tenait entre des myrtes qui étaient en un lieu profond; et après lui il y avait des chevaux roux, des chevaux pommelés et des blancs.
9 Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?” Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”
Et je dis: Mon Seigneur! Que [signifient] ces choses? Et l’Ange qui parlait avec moi me dit: Je te montrerai ce que ces choses [signifient].
10 Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambao Bwana amewatuma waende duniani kote.”
Et l'homme qui se tenait entre les myrtes, répondit, et dit: Ce sont ici ceux que l'Eternel a envoyés pour parcourir la terre.
11 Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika wa Bwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”
Et ils répondirent à l'Ange de l'Eternel qui se tenait entre les myrtes, et dirent: Nous avons parcouru la terre; et voici, toute la terre est habitée, et est en repos.
12 Kisha malaika wa Bwana akasema, “Bwana Mwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?”
Alors l'Ange de l'Eternel répondit, et dit: Eternel des armées, jusqu'à quand n'auras-tu point compassion de Jérusalem et des villes de Juda, contre lesquelles tu as été indigné pendant ces soixante et dix années?
13 Kwa hiyo Bwana akazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.
Et l'Eternel répondit à l'Ange qui parlait avec moi, de bonnes paroles, des paroles de consolation.
14 Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni,
Puis l'Ange qui parlait avec moi, me dit: Crie, en disant: Ainsi a dit l'Eternel des armées: Je suis ému d'une grande jalousie pour Jérusalem et pour Sion.
15 lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’
Et je suis extrêmement indigné contre les nations qui sont à leur aise; car j'étais indigné pour un peu [de temps], et ils ont aidé au mal.
16 “Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
C'est pourquoi ainsi a dit l'Eternel: Je me suis retourné vers Jérusalem par compassion, et ma maison sera rebâtie dans elle, dit l'Eternel des armées; et le niveau sera étendu sur Jérusalem.
17 “Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi na Bwana atamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’”
Crie encore, en disant: Ainsi a dit l'Eternel des armées: Mes villes regorgeront encore de biens, et l'Eternel consolera encore Sion, et élira encore Jérusalem.
18 Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne!
Puis j'élevai mes yeux, et regardai; et voici quatre cornes.
19 Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?” Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”
Alors je dis à l'Ange qui parlait avec moi: Que veulent dire ces choses? Et il me répondit: Ce sont les cornes qui ont dissipé Juda, Israël et Jérusalem.
20 Kisha Bwana akanionyesha mafundi wanne.
Puis l'Eternel me montra quatre forgerons.
21 Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?” Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”
Et je dis: Que viennent faire ceux-ci? Et il répondit, et dit: Ce sont là les cornes qui ont dissipé Juda, tellement que personne ne levait la tête; mais ceux-ci sont venus pour les effrayer, et pour abattre les cornes des nations qui ont élevé la corne contre le pays de Juda, pour le dissiper.

< Zekaria 1 >