< Ruth 1 >

1 Wakati Waamuzi walipotawala Israeli, kulikuwa na njaa katika nchi. Mtu mmoja kutoka nchi ya Bethlehemu ya Yuda, pamoja na mke wake na wanawe wawili, akaenda kuishi katika nchi ya Moabu.
Or il arriva du temps que les Juges jugeaient, qu'il y eut une famine au pays; et un homme de Bethléhem de Juda s'en alla, pour demeurer en quelque [lieu du] pays de Moab, lui et sa femme, et ses deux fils.
2 Mtu huyu aliitwa Elimeleki, mkewe aliitwa Naomi, na hao wanawe wawili waliitwa Maloni na Kilioni. Walikuwa Waefrathi kutoka Bethlehemu ya Yuda. Wakaenda katika nchi ya Moabu, wakaishi huko.
Et le nom de cet homme était Eli-mélec, et le nom de sa femme Nahomi, et les noms de ses deux fils Mahlon et Kiljon, Ephratiens, de Bethléhem de Juda; et ils vinrent au pays de Moab, et y demeurèrent.
3 Elimeleki mumewe Naomi akafa, hivyo Naomi akabaki na wanawe wawili.
Or Eli-mélec, mari de Nahomi, mourut et elle resta avec ses deux fils;
4 Nao wakaoa wanawake Wamoabu, jina la mmoja aliitwa Orpa, na wa pili aliitwa Ruthu. Baada ya kama miaka kumi,
Qui prirent pour eux des femmes Moabites, dont l'une s'appelait Horpa, et l'autre Ruth; et ils demeurèrent là environ dix ans.
5 Maloni na Kilioni pia wakafa. Basi Naomi akabaki hana mume wala wanawe wawili.
Puis ses deux fils Mahlon et Kiljon moururent; ainsi cette femme demeura là, privée de ses deux fils et de son mari.
6 Aliposikia akiwa huko Moabu kwamba Bwana amewasaidia watu wake kwa kuwapa chakula, Naomi na wakweze wakajiandaa kurudi nyumbani.
Depuis elle se leva avec ses belles-filles pour s'en retourner du pays de Moab; car elle apprit au pays de Moab, que l'Eternel avait visité son peuple, en leur donnant du pain.
7 Yeye na wakweze wawili wakaondoka pale walipokuwa wakiishi na kushika njia kurudi nchi ya Yuda.
Ainsi elle partit du lieu où elle avait demeuré, et ses deux belles-filles avec elle, et elles se mirent en chemin pour retourner au pays de Juda.
8 Ndipo Naomi akawaambia wale wakwe zake wawili, “Rudini, kila mmoja wenu nyumbani kwa mama yake. Bwana na awatendee fadhili kama mlivyowatendea hao waliofariki, na pia mimi.
Et Nahomi dit à ses deux belles-filles: Allez, retournez chacune en la maison de sa mère; l'Eternel vous fasse du bien, comme vous en avez fait à ceux qui sont morts, et à moi.
9 Bwana na amjalie kila mmoja wenu maisha mema nyumbani kwa mume mwingine.” Kisha akawabusu, nao wakalia kwa sauti kubwa,
L'Eternel vous fasse trouver du repos à chacune dans la maison de son mari; et elle les baisa; mais elles élevèrent leur voix, et pleurèrent.
10 wakamwambia, “Tutarudi pamoja na wewe nyumbani kwa watu wako.”
Et lui dirent: Mais [plutôt] nous retournerons avec toi vers ton peuple.
11 Lakini Naomi akasema, “Rudini nyumbani, binti zangu. Kwa nini mnifuate? Je, mimi nitaweza tena kuwa na wana wengine ambao wataweza kuwaoa ninyi?
Et Nahomi répondit: Retournez-vous-en, mes filles; pourquoi viendriez-vous avec moi? Ai-je encore des fils en mon ventre, afin que vous les ayez pour maris?
12 Rudini nyumbani, binti zangu; mimi ni mzee kiasi kwamba siwezi kumpata mume mwingine. Hata kama ningefikiria kuwa bado kuna tumaini kwangu, hata kama ningekuwa na mume usiku huu na kuwazaa wana,
Retournez-vous-en, mes filles, allez-vous-en; car je suis trop âgée pour être remariée; et quand je dirais que j'en aurais quelque espérance, quand même dès cette nuit je serais avec un mari, et quand même j'aurais enfanté des fils;
13 je, mngesubiri mpaka wakue? Mngebakia bila kuolewa mkiwasubiri? La, hasha, binti zangu. Nimepata uchungu kuliko ninyi, kwa sababu mkono wa Bwana umekuwa kinyume nami!”
Les attendriez-vous jusqu'à ce qu'ils fussent grands? Différeriez-vous pour eux d'être remariées? Non, mes filles; certes je suis dans une plus grande amertume que vous, parce que la main de l'Eternel s'est déployée contre moi.
14 Kisha wakalia tena kwa sauti. Orpa akambusu mama mkwe wake, akaenda zake, lakini Ruthu akaambatana naye.
Alors elles élevèrent leur voix, et pleurèrent encore; et Horpa baisa sa belle-mère; mais Ruth resta avec elle.
15 Naomi akamwambia, “Tazama, mwenzako anarejea kwa watu wake na kwa miungu yake. Rudi pamoja naye.”
Et [Nahomi lui] dit: Voici, ta belle-sœur s'en est retournée à son peuple et à ses dieux; retourne-t'en après ta belle-sœur.
16 Lakini Ruthu akajibu, “Usinisihi nikuache au niache kukufuata. Utakakokwenda nami nitakwenda, na wewe utakapoishi nitaishi. Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako atakuwa Mungu wangu.
Mais Ruth répondit: Ne me prie point de te laisser, pour m'éloigner de toi; car où tu iras, j'irai; et où tu demeureras, je demeurerai; ton peuple sera mon peuple, et ton Dieu sera mon Dieu.
17 Pale utakapofia nami nitafia hapo, na papo hapo nitazikwa. Bwana na aniadhibu vikali, kama kitu kingine chochote kitanitenga nawe isipokuwa kifo.”
Là où tu mourras, je mourrai, et j'y serai ensevelie. Ainsi me fasse l'Eternel et ainsi y ajoute, qu'il n'y aura que la mort qui me sépare de toi.
18 Naomi alipotambua kwamba Ruthu amenuia kufuatana naye, hakuendelea kumsihi tena.
[Nahomi] donc voyant qu'elle était résolue d'aller avec elle, cessa de lui en parler.
19 Kwa hiyo hao wanawake wawili wakaondoka, wakafika Bethlehemu. Walipofika Bethlehemu, mji mzima ulitaharuki, wanawake wakashangaa, wakasema, “Huyu aweza kuwa ni Naomi?”
Et elles marchèrent toutes deux jusqu'à ce qu'elles vinrent à Bethléhem; et comme elles furent entrées dans Bethléhem, toute la ville se mit à parler sur son sujet; [et les femmes] dirent: N'est-ce pas ici Nahomi?
20 Akawaambia, “Msiniite tena Naomi, niiteni Mara, kwa sababu Mwenyezi amenitendea mambo machungu sana.
Et elle leur répondit: Ne m'appelez point Nahomi, appelez-moi Mara. Car le Tout-Puissant m'a remplie d'amertume.
21 Mimi niliondoka hali nimejaa, lakini Bwana amenirudisha mtupu. Kwa nini kuniita Naomi? Bwana amenitendea mambo machungu; Mwenyezi ameniletea msiba.”
Je m'en allai pleine de biens, et l'Eternel me ramène vide. Pourquoi m'appelleriez-vous Nahomi, puisque l'Eternel m'a abattue, et que le Tout-Puissant m'a affligée?
22 Kwa hiyo Naomi alirudi pamoja na Ruthu Mmoabu mkwe wake, nao wakafika Bethlehemu mwanzoni mwa kuvuna shayiri.
C'est ainsi que s'en retourna Nahomi, et avec elle Ruth la Moabite, sa belle-fille, qui était venue du pays de Moab; et elles entrèrent dans Bethléhem au commencement de la moisson des orges.

< Ruth 1 >