< Zaburi 89 >

1 Utenzi wa Ethani Mwezrahi. Nitaimba juu ya upendo mkuu wa Bwana milele; kwa kinywa changu nitajulisha uaminifu wako ujulikane kwa vizazi vyote.
以斯拉人以探的訓誨詩。 我要歌唱耶和華的慈愛,直到永遠; 我要用口將你的信實傳與萬代。
2 Nitatangaza kuwa upendo wako unasimama imara milele na uaminifu wako umeuthibitisha mbinguni.
因我曾說:你的慈悲必建立到永遠; 你的信實必堅立在天上。
3 Ulisema, “Nimefanya agano na mteule wangu, nimemwapia mtumishi wangu Daudi,
我與我所揀選的人立了約, 向我的僕人大衛起了誓:
4 ‘Nitaimarisha uzao wako milele na kudumisha ufalme wako kwa vizazi vyote.’”
我要建立你的後裔,直到永遠; 要建立你的寶座,直到萬代。 (細拉)
5 Ee Bwana, mbingu zinayasifu maajabu yako, uaminifu wako pia katika kusanyiko la watakatifu.
耶和華啊,諸天要稱讚你的奇事; 在聖者的會中,要稱讚你的信實。
6 Kwa kuwa ni nani katika mbingu anayeweza kulinganishwa na Bwana? Ni nani miongoni mwa viumbe vya mbinguni aliye kama Bwana?
在天空誰能比耶和華呢? 神的眾子中,誰能像耶和華呢?
7 Katika kusanyiko la watakatifu, Mungu huogopwa sana, anahofiwa kuliko wote wanaomzunguka.
他在聖者的會中,是大有威嚴的上帝, 比一切在他四圍的更可畏懼。
8 Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, ni nani aliye kama wewe? Ee Bwana, wewe ni mwenye nguvu, na uaminifu wako unakuzunguka.
耶和華-萬軍之上帝啊, 哪一個大能者像你耶和華? 你的信實是在你的四圍。
9 Wewe unatawala bahari yenye msukosuko; wakati mawimbi yake yanapoinuka, wewe unayatuliza.
你管轄海的狂傲; 波浪翻騰,你就使它平靜了。
10 Wewe ulimponda Rahabu kama mmojawapo wa waliochinjwa; kwa mkono wako wenye nguvu, uliwatawanya adui zako.
你打碎了拉哈伯,似乎是已殺的人; 你用有能的膀臂打散了你的仇敵。
11 Mbingu ni zako, nayo nchi pia ni yako, uliuwekea ulimwengu msingi pamoja na vyote vilivyomo.
天屬你,地也屬你; 世界和其中所充滿的都為你所建立。
12 Uliumba kaskazini na kusini; Tabori na Hermoni wanaliimbia jina lako kwa furaha.
南北為你所創造; 他泊和黑門都因你的名歡呼。
13 Mkono wako umejaa uwezo; mkono wako una nguvu, mkono wako wa kuume umetukuzwa.
你有大能的膀臂; 你的手有力,你的右手也高舉。
14 Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako cha enzi; upendo na uaminifu vinakutangulia.
公義和公平是你寶座的根基; 慈愛和誠實行在你前面。
15 Heri ni wale ambao wamejifunza kukusifu kwa shangwe, wanaotembea katika mwanga wa uwepo wako, Ee Bwana.
知道向你歡呼的,那民是有福的! 耶和華啊,他們在你臉上的光裏行走。
16 Wanashangilia katika jina lako mchana kutwa, wanafurahi katika haki yako.
他們因你的名終日歡樂, 因你的公義得以高舉。
17 Kwa kuwa wewe ni utukufu na nguvu yao, kwa wema wako unatukuza pembe yetu.
你是他們力量的榮耀; 因為你喜悅我們,我們的角必被高舉。
18 Naam, ngao yetu ni mali ya Bwana, na mfalme wetu mali ya Aliye Mtakatifu wa Israeli.
我們的盾牌屬耶和華; 我們的王屬以色列的聖者。
19 Ulizungumza wakati fulani katika maono, kwa watu wako waaminifu, ukasema: “Nimeweka nguvu kwa shujaa, nimemwinua kijana miongoni mwa watu.
當時,你在異象中曉諭你的聖民,說: 我已把救助之力加在那有能者的身上; 我高舉那從民中所揀選的。
20 Nimemwona Daudi, mtumishi wangu, na nimemtia mafuta yangu matakatifu.
我尋得我的僕人大衛, 用我的聖膏膏他。
21 Kitanga changu kitamtegemeza, hakika mkono wangu utamtia nguvu.
我的手必使他堅立; 我的膀臂也必堅固他。
22 Hakuna adui atakayemtoza ushuru, hakuna mtu mwovu atakayemwonea.
仇敵必不勒索他; 凶惡之子也不苦害他。
23 Nitawaponda adui zake mbele zake na kuwaangamiza watesi wake.
我要在他面前打碎他的敵人, 擊殺那恨他的人。
24 Upendo wangu mkamilifu utakuwa pamoja naye, kwa Jina langu pembe yake itatukuzwa.
只是我的信實和我的慈愛要與他同在; 因我的名,他的角必被高舉。
25 Nitauweka mkono wake juu ya bahari, mkono wake wa kuume juu ya mito.
我要使他的左手伸到海上, 右手伸到河上。
26 Naye ataniita kwa sauti, ‘Wewe ni Baba yangu, Mungu wangu, Mwamba na Mwokozi wangu.’
他要稱呼我說:你是我的父, 是我的上帝,是拯救我的磐石。
27 Nitamteua pia awe mzaliwa wangu wa kwanza, aliyetukuka kuliko wafalme wote wa dunia.
我也要立他為長子, 為世上最高的君王。
28 Nitadumisha upendo wangu kwake milele, na agano langu naye litakuwa imara.
我要為他存留我的慈愛,直到永遠; 我與他立的約必要堅定。
29 Nitaudumisha uzao wake milele, kiti chake cha enzi kama mbingu zinavyodumu.
我也要使他的後裔存到永遠, 使他的寶座如天之久。
30 “Kama wanae wataacha amri yangu na wasifuate sheria zangu,
倘若他的子孫離棄我的律法, 不照我的典章行,
31 kama wakihalifu maagizo yangu na kutoshika amri zangu,
背棄我的律例, 不遵守我的誡命,
32 nitaadhibu dhambi yao kwa fimbo, uovu wao kwa kuwapiga,
我就要用杖責罰他們的過犯, 用鞭責罰他們的罪孽。
33 lakini sitauondoa upendo wangu kwake, wala sitausaliti uaminifu wangu kamwe.
只是我必不將我的慈愛全然收回, 也必不叫我的信實廢棄。
34 Mimi sitavunja agano langu wala sitabadili lile ambalo midomo yangu imelitamka.
我必不背棄我的約, 也不改變我口中所出的。
35 Mara moja na kwa milele, nimeapa kwa utakatifu wangu, nami sitamdanganya Daudi:
我一次指着自己的聖潔起誓: 我決不向大衛說謊!
36 kwamba uzao wake utaendelea milele, na kiti chake cha enzi kitadumu mbele zangu kama jua;
他的後裔要存到永遠; 他的寶座在我面前如日之恆一般,
37 kitaimarishwa milele kama mwezi, shahidi mwaminifu angani.”
又如月亮永遠堅立, 如天上確實的見證。 (細拉)
38 Lakini wewe umemkataa, umemdharau, umemkasirikia sana mpakwa mafuta wako.
但你惱怒你的受膏者, 就丟掉棄絕他。
39 Umelikana agano lako na mtumishi wako, na umeinajisi taji yake mavumbini.
你厭惡了與僕人所立的約, 將他的冠冕踐踏於地。
40 Umebomoa kuta zake zote, na ngome zake zote umezifanya kuwa magofu.
你拆毀了他一切的籬笆, 使他的保障變為荒場。
41 Wote wapitao karibu wamemnyangʼanya mali zake; amekuwa dharau kwa jirani zake.
凡過路的人都搶奪他; 他成為鄰邦的羞辱。
42 Umeutukuza mkono wa kuume wa adui zake, umewafanya watesi wake wote washangilie.
你高舉了他敵人的右手; 你叫他一切的仇敵歡喜。
43 Umegeuza makali ya upanga wake, na hukumpa msaada katika vita.
你叫他的刀劍捲刃, 叫他在爭戰之中站立不住。
44 Umeikomesha fahari yake, na kukiangusha kiti chake cha enzi.
你使他的光輝止息, 將他的寶座推倒於地。
45 Umezifupisha siku za ujana wake, umemfunika kwa vazi la aibu.
你減少他青年的日子, 又使他蒙羞。 (細拉)
46 Hata lini, Ee Bwana? Utajificha milele? Ghadhabu yako itawaka kama moto hata lini?
耶和華啊,這要到幾時呢? 你要將自己隱藏到永遠嗎? 你的忿怒如火焚燒要到幾時呢?
47 Kumbuka jinsi maisha yangu yanavyopita haraka. Ni kwa ubatili kiasi gani umemuumba mwanadamu!
求你想念我的時候是何等的短少; 你創造世人,要使他們歸何等的虛空呢?
48 Ni mtu gani awezaye kuishi na asione kifo, au kujiokoa mwenyewe kutoka nguvu za kaburi? (Sheol h7585)
誰能常活免死、 救他的靈魂脫離陰間的權柄呢? (細拉) (Sheol h7585)
49 Ee Bwana, uko wapi upendo wako mkuu wa mwanzoni, ambao katika uaminifu wako ulimwapia Daudi?
主啊,你從前憑你的信實 向大衛立誓要施行的慈愛在哪裏呢?
50 Bwana kumbuka jinsi mtumishi wako amesimangwa, jinsi ninavyovumilia moyoni mwangu dhihaka za mataifa yote,
主啊,求你記念僕人們所受的羞辱, 記念我怎樣將一切強盛民的羞辱存在我懷裏。
51 dhihaka ambazo kwazo adui zako wamenisimanga, Ee Bwana, ambazo kwazo wamesimanga kila hatua ya mpakwa mafuta wako.
耶和華啊,你的仇敵用這羞辱羞辱了你的僕人, 羞辱了你受膏者的腳蹤。
52 Msifuni Bwana milele!
耶和華是應當稱頌的,直到永遠。 阿們!阿們!

< Zaburi 89 >