< Zaburi 76 >

1 Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
For the end, among the Hymns, a Psalm for Asaph; a Song for the Assyrian. God is known in Judea: his name is great in Israel.
2 Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
And his place has been in peace, and his dwelling-place in Sion.
3 Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
There he broke the power of the bows, the shield, and the sword, and the battle. (Pause)
4 Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
You do wonderfully shine forth from the everlasting mountains.
5 Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
All the simple ones in heart were troubled; all the men of wealth have slept their sleep, and have found nothing in their hands.
6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
At your rebuke, O God of Jacob, the riders on horses slumbered.
7 Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
You are terrible; and who shall withstand you, because of your anger?
8 Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
You did cause judgment to be heard from heaven; the earth feared, and was still,
9 wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
when God arose to judgment, to save all the meek in heart. (Pause)
10 Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
For the inward thought of man shall give thanks to you: and the memorial of his inward thought shall keep a feast to you.
11 Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
Vow, and pay [your vows] to the Lord our God; all that are round about him shall bring gifts, [even] to him that is terrible,
12 Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.
and that takes away the spirits of princes; to him that is terrible among the kings of the earth.

< Zaburi 76 >