< Zaburi 71 >

1 Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
Éternel, je me suis retiré vers toi; que je ne sois jamais confus!
2 Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
Délivre-moi par ta justice et me fais échapper; incline ton oreille vers moi et sauve-moi!
3 Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
Sois pour moi un rocher de retraite, où je puisse toujours me retirer; tu as ordonné que je sois sauvé; car tu es mon rocher et ma forteresse.
4 Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
Mon Dieu, délivre-moi de la main du méchant, de la main du pervers et de l'oppresseur.
5 Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
Car tu es mon attente, Seigneur Éternel, ma confiance dès ma jeunesse.
6 Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
Je me suis appuyé sur toi dès ma naissance; c'est toi qui m'as tiré du sein de ma mère; tu es ma louange en tout temps.
7 Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
J'ai été comme un monstre aux yeux de plusieurs; mais toi, tu es ma forte retraite.
8 Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
Que ma bouche soit pleine de ta louange et de ta gloire chaque jour!
9 Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
Ne me rejette pas au temps de la vieillesse; quand ma force s'en va, ne m'abandonne pas!
10 Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
Car mes ennemis parlent de moi; ceux qui guettent mon âme tiennent conseil ensemble,
11 Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
Disant: Dieu l'a abandonné; poursuivez-le et le saisissez, car il n'y a personne qui le délivre.
12 Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
O Dieu! ne t'éloigne pas de moi; mon Dieu, accours à mon aide!
13 Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
Que les ennemis de mon âme soient couverts d'opprobre et de honte; que ceux qui cherchent ma perte soient confus, et qu'ils périssent!
14 Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
Mais moi, j'espérerai toujours, et je te louerai de plus en plus.
15 Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
Ma bouche racontera chaque jour ta justice et tes délivrances; car je n'en sais pas le nombre.
16 Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
J'irai louant tes grandes œuvres, Seigneur Éternel; je célébrerai ta seule justice.
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
O Dieu! tu m'as instruit dès ma jeunesse, et jusqu'ici j'ai annoncé tes merveilles.
18 Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
Et même jusqu'à la vieillesse, jusqu'à la blanche vieillesse, ô Dieu, ne m'abandonne pas; jusqu'à ce que j'aie annoncé la force de ton bras à cette génération, ta puissance à tous ceux qui naîtront,
19 Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
Et ta justice, ô Dieu, qui est haut élevée. Tu fais de grandes choses. O Dieu! qui est semblable à toi?
20 Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
Toi qui, m'ayant fait voir plusieurs détresses et plusieurs maux, reviens me rendre la vie, et qui me fais remonter hors des abîmes de la terre.
21 Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
Tu accroîtras ma grandeur, et tu me consoleras encore.
22 Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
Aussi je te louerai sur l'instrument du luth, pour ta fidélité, ô mon Dieu! Je te psalmodierai sur la harpe, ô Saint d'Israël!
23 Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
Mes lèvres, et mon âme que tu as rachetée, chanteront de joie quand je te psalmodierai.
24 Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.
Ma langue aussi chaque jour redira ta justice; car ceux qui cherchent mon mal seront honteux et rougiront.

< Zaburi 71 >