< Zaburi 71 >

1 Ee Bwana, nimekukimbilia wewe, usiache nikaaibika kamwe.
耶和華啊,我投靠你; 求你叫我永不羞愧!
2 Kwa haki yako uniponye na kuniokoa, unitegee sikio lako uniokoe.
求你憑你的公義搭救我,救拔我; 側耳聽我,拯救我!
3 Uwe kwangu mwamba wa kimbilio, mahali nitakapokimbilia kila wakati; toa amri ya kuniokoa, kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu.
求你作我常住的磐石; 你已經命定要救我, 因為你是我的巖石,我的山寨。
4 Ee Mungu wangu uniokoe kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye makucha ya watu wabaya na wakatili.
我的上帝啊,求你救我脫離惡人的手, 脫離不義和殘暴之人的手。
5 Kwa kuwa umekuwa tumaini langu, Ee Bwana Mwenyezi, tegemeo langu tangu ujana wangu.
主-耶和華啊,你是我所盼望的; 從我年幼,你是我所倚靠的。
6 Tangu kuzaliwa nimekutegemea wewe, ulinitoa tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu wewe daima.
我從出母胎被你扶持; 使我出母腹的是你。 我必常常讚美你!
7 Nimekuwa kama kioja kwa wengi, lakini wewe ni kimbilio langu imara.
許多人以我為怪, 但你是我堅固的避難所。
8 Kinywa changu kimejazwa sifa zako, nikitangaza utukufu wako mchana kutwa.
你的讚美,你的榮耀 終日必滿了我的口。
9 Usinitupe wakati wa uzee, wala usiniache nguvu zangu zinapopungua.
我年老的時候,求你不要丟棄我! 我力氣衰弱的時候,求你不要離棄我!
10 Kwa maana adui zangu wananisengenya, wale wanaonivizia kuniua wafanya hila.
我的仇敵議論我; 那些窺探要害我命的彼此商議,
11 Wanasema, “Mungu amemwacha, mkimbilieni mkamkamate, kwani hakuna wa kumwokoa.”
說:上帝已經離棄他; 我們追趕他,捉拿他吧! 因為沒有人搭救。
12 Ee Mungu, usiwe mbali nami, njoo haraka kunisaidia, Ee Mungu wangu.
上帝啊,求你不要遠離我! 我的上帝啊,求你速速幫助我!
13 Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.
願那與我性命為敵的,羞愧被滅; 願那謀害我的,受辱蒙羞。
14 Lakini mimi, nitatumaini siku zote, nitakusifu zaidi na zaidi.
我卻要常常盼望, 並要越發讚美你。
15 Kinywa changu kitasimulia haki yako, wokovu wako mchana kutwa, ingawa sifahamu kipimo chake.
我的口終日要述說你的公義和你的救恩, 因我不計其數。
16 Ee Bwana Mwenyezi, nitakuja na kutangaza matendo yako makuu, nitatangaza haki yako, yako peke yako.
我要來說主-耶和華大能的事; 我單要提說你的公義。
17 Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, hadi leo ninatangaza matendo yako ya ajabu.
上帝啊,自我年幼時,你就教訓我; 直到如今,我傳揚你奇妙的作為。
18 Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.
上帝啊,我到年老髮白的時候, 求你不要離棄我! 等我將你的能力指示下代, 將你的大能指示後世的人。
19 Ee Mungu, haki yako imefika juu katika mbingu, wewe ambaye umefanya mambo makuu. Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
上帝啊,你的公義甚高; 行過大事的上帝啊,誰能像你!
20 Ingawa umenifanya nipate taabu, nyingi na chungu, utanihuisha tena, kutoka vilindi vya dunia utaniinua tena.
你是叫我們多經歷重大急難的, 必使我們復活, 從地的深處救上來。
21 Utaongeza heshima yangu na kunifariji tena.
求你使我越發昌大, 又轉來安慰我。
22 Ee Mungu wangu, nitakusifu kwa kinubi kwa ajili ya uaminifu wako; Ee Uliye Mtakatifu wa Israeli, nitakuimbia sifa kwa zeze.
我的上帝啊,我要鼓瑟稱讚你, 稱讚你的誠實! 以色列的聖者啊,我要彈琴歌頌你!
23 Midomo yangu itapaza sauti kwa furaha ninapokuimbia sifa, mimi, ambaye umenikomboa.
我歌頌你的時候, 我的嘴唇和你所贖我的靈魂都必歡呼;
24 Ulimi wangu utasimulia matendo yako ya haki mchana kutwa, kwa maana wale waliotaka kunidhuru, wameaibishwa na kufadhaishwa.
並且我的舌頭必終日講論你的公義, 因為那些謀害我的人已經蒙羞受辱了。

< Zaburi 71 >