< Zaburi 56 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Njiwa mkimya wa mbali.” Utenzi wa Daudi. Baada ya kukamatwa na Wafilisti huko Gathi. Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao.
[For the Chief Musician. To the tune of "Silent Dove in Distant Lands." A poem by David, when the Philistines seized him in Gath.] Be merciful to me, God, for man wants to swallow me up. All day long, he attacks and oppresses me.
2 Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, wengi wananishambulia kwa kiburi chao.
My enemies want to swallow me up all day long, for they are many who fight proudly against me.
3 Wakati ninapoogopa, nitakutumaini wewe.
When I am afraid, I will put my trust in you.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. Mwanadamu apatikanaye na kufa, atanitenda nini?
In God, I praise his word. In God, I put my trust. I will not be afraid. What can flesh do to me?
5 Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, siku zote wanapanga shauri la kunidhuru.
All day long they twist my words. All their thoughts are against me for evil.
6 Wananifanyia hila, wanajificha, wanatazama hatua zangu, wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu.
They conspire and lurk, watching my steps, they are eager to take my life.
7 Wasiepuke kwa vyovyote, Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa.
Shall they escape by iniquity? In anger cast down the peoples, God.
8 Andika maombolezo yangu, orodhesha machozi yangu katika gombo lako: je, haya hayapo katika kumbukumbu zako?
You number my wanderings. You put my tears into your bottle. Aren't they in your book?
9 Ndipo adui zangu watarudi nyuma ninapoita msaada. Kwa hili nitajua kwamba Mungu yuko upande wangu.
Then my enemies shall turn back in the day that I call. I know this, that God is for me.
10 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,
In God, I will praise his word. In the LORD, I will praise his word.
11 katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?
I have put my trust in God. I will not be afraid. What can man do to me?
12 Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.
Your vows are on me, God. I will give thank offerings to you.
13 Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti na miguu yangu kwenye kujikwaa, ili niweze kuenenda mbele za Mungu katika nuru ya uzima.
For you have delivered my soul from death, and prevented my feet from falling, that I may walk before God in the light of the living.

< Zaburi 56 >