< Zaburi 50 >

1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
Un Salmo de Asaf. ¡El Señor, el Dios todopoderoso, habla! Él convoca a todos en la tierra, desde el este hasta el oeste.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
Dios brilla desde el monte de Sión, perfecto en belleza.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
Nuestro Dios llegará, y no se quedará quieto. Llamas de fuego vienen detrás de él, quemando todo a su alrededor; una feroz tormenta se mueve alrededor de él.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
Invoca a los cielos sobre la tierra para que presencien el juicio de su pueblo.
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
“Tráiganme a los que confían en mí, aquellos que cumplieron mi pacto conmigo como sacrificio”.
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
Los cielos declaran que sus decisiones están bien, porque Dios mismo es el juez. (Selah)
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
“Mi pueblo, escuchen lo que tengo para decir. Traigo cargos en su contra, Israel. ¡Yo soy Dios, su Dios!
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
No estoy hablando de sacrificios ni de ofrendas quemadas que me ofrecen todo el tiempo.
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
No necesito toros de sus graneros ni cabras de sus corrales,
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
porque míos son todos los animales del bosque, y el ganado de miles de cerros me pertenece.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
Conozco a cada pájaro de la montaña; todas las cosas vivientes en los campos son mías.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
Si estuviera hambriento, no te lo diría, porque la tierra y todo lo que hay en ella es mío.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
¿Me como yo la carne de los toros y bebo la sangre de las cabras?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
Den ofrendas de agradecimiento a Dios; mantengan las promesas que le hicieron al Altísimo,
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
y llámenme cuando estén en problemas. Los rescataré, y me agradecerán”.
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
Pero a los malvados Dios les dice, “¿Cuál es el objetivo de repetir mi ley y hacer promesas vacías sobre obedecer mi pacto?
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
Odias mi disciplina, y desechas mis palabras.
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
Cuando ves a la gente robando los admiras y te asocias con adúlteros.
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
Con tu boca dices cosas malas; usas tu lengua para esparcir mentiras.
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
Te sientas y comienzas a hablar en contra de tu hermano, calumniando al hijo de tu propia madre.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
Yo me quedo callado cuando haces esas cosas. Tú pensaste que yo era alguien como tú. Pero ahora te confronto, y traigo mis cargos en contra tuya.
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
Piensen otra vez, ustedes que menosprecian a Dios, o los haré trizas, y nadie podrá salvarlos.
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
Pero aquellos que dan ofrendas de agradecimiento me honran, y a aquellos que siguen el bien les mostraré mi salvación”.

< Zaburi 50 >