< Zaburi 50 >

1 Zaburi ya Asafu. Mwenye Nguvu, Mungu, Bwana, asema na kuiita dunia, tangu mawio ya jua hadi mahali pake liendapo kutua.
Ein Psalm Asaphs. Gott, Gott Jahwe, redet und ruft der Erde vom Aufgang der Sonne bis zu ihrem Untergang.
2 Kutoka Sayuni, penye uzuri mkamilifu, Mungu anaangaza.
Aus Zion, der Krone der Schönheit, strahlt Gott auf.
3 Mungu wetu anakuja na hatakaa kimya, moto uteketezao unamtangulia, akiwa amezungukwa na tufani kali.
Unser Gott kommt und schweigt nicht. Verzehrendes Feuer geht vor ihm her, und rings um ihn stürmt es gewaltig.
4 Anaziita mbingu zilizo juu, na nchi, ili aweze kuwahukumu watu wake:
Er ruft dem Himmel droben zu und der Erde, damit er sein Volk richte:
5 “Nikusanyieni watu wangu waliowekwa wakfu, waliofanya agano nami kwa dhabihu.”
“Versammelt mir meine Frommen, die den Bund mit mir beim Opfer schlossen!”
6 Nazo mbingu zinatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ni hakimu.
Da verkündigte der Himmel seine Gerechtigkeit; denn Gott ist Richter. (Sela)
7 “Sikieni, enyi watu wangu, nami nitasema, ee Israeli, nami nitashuhudia dhidi yenu: Mimi ndimi Mungu, Mungu wenu.
“Höre, mein Volk, laß mich reden; Israel, laß mich wider dich zeugen: Gott, dein Gott, bin ich!
8 Sikukemei kwa sababu ya dhabihu zako, au sadaka zako za kuteketezwa, ambazo daima ziko mbele zangu.
“Nicht wegen deiner Opfer will ich dich zur Rede setzen - sind doch deine Brandopfer beständig vor mir!
9 Sina haja ya fahali wa banda lako, au mbuzi wa zizi lako.
“Ich mag nicht Farren aus deinem Hause nehmen, noch Böcke aus deinen Hürden.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, na pia makundi ya mifugo juu ya vilima elfu.
“Denn mein sind alle Tiere des Waldes, das Vieh auf den Bergen mit ihren Tausenden.
11 Ninamjua kila ndege mlimani, nao viumbe wa kondeni ni wangu.
“Ich kenne alle Vögel auf den Bergen, und was sich im Gefilde regt, ist mir bewußt.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi, kwa maana ulimwengu ni wangu, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake.
“Wenn mich hungerte, würde ich dir's nicht sagen; denn mein ist der Erdkreis und was ihn füllt.
13 Je, mimi hula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?
“Esse ich etwa das Fleisch von Stieren oder trinke ich das Blut von Böcken?
14 Toa sadaka za shukrani kwa Mungu, timiza nadhiri zako kwake Yeye Aliye Juu Sana,
“Opfere Gott Dank, so wirst du dem Höchsten deine Gelübde bezahlen!
15 na uniite siku ya taabu; nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”
“Und rufe mich an am Tage der Not: ich will dich erretten und du sollst mich preisen!”
16 Lakini kwake mtu mwovu, Mungu asema: “Una haki gani kunena sheria zangu au kuchukua agano langu midomoni mwako?
Zum Gottlosen aber spricht Gott: “Was hast du meine Satzungen herzuzählen und nimmst meinen Bund in deinen Mund,
17 Unachukia mafundisho yangu na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
“während du doch Zucht hassest und meine Worte hinter dich wirfst?
18 Unapomwona mwizi, unaungana naye, unapiga kura yako pamoja na wazinzi.
“Wenn du einen Dieb sahst, so liefst du mit ihm und mit Ehebrechern hattest du Gemeinschaft.
19 Unakitumia kinywa chako kwa mabaya na kuuongoza ulimi wako kwa hila.
“Du lässest deinen Mund sich frei in Bosheit ergehen, und deine Zunge flicht Betrug.
20 Wanena daima dhidi ya ndugu yako na kumsingizia mwana wa mama yako.
“Du sitzest da, redest wider deinen Bruder, bringst Beschimpfung auf den Sohn deiner Mutter.
21 Mambo haya unayafanya, nami nimekaa kimya, ukafikiri Mimi nami ni kama wewe. Lakini nitakukemea na kuweka mashtaka mbele yako.
“Solches thatest du, und ich schwieg. Da meintest du, ich sei ganz wie du. “Aber ich will dich zur Rechenschaft ziehn und dir's vor Augen stellen!
22 “Yatafakarini haya, ninyi mnaomsahau Mungu, ama sivyo nitawararua vipande vipande, wala hapatakuwepo na yeyote wa kuwaokoa:
“Merkt doch dies, die ihr Gottes vergeßt, daß ich nicht hinwegraffe, ohne daß jemand zu retten vermag.
23 Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”
“Wer Dank opfert, ehrt mich, und wer unsträflich wandelt, den will ich seine Lust sehen lassen an Gottes Heil!”

< Zaburi 50 >