< Zaburi 48 >

1 Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.
[A Song. A Psalm by the sons of Korah.] Great is Jehovah, and greatly to be praised, in the city of our God, in his holy mountain.
2 Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, furaha ya dunia yote. Kama vilele vya juu sana vya Safoni ni Mlima Sayuni, mji wa Mfalme Mkuu.
Beautiful in elevation, the joy of the whole earth, is Mount Zion, in the far north, the city of the great King.
3 Mungu yuko katika ngome zake; amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake.
God has shown himself in her citadels as a refuge.
4 Wakati wafalme walipounganisha nguvu, waliposonga mbele pamoja,
For, look, the kings assembled themselves, they passed by together.
5 walimwona nao wakashangaa, wakakimbia kwa hofu.
They saw it, then they were amazed. They were dismayed. They hurried away.
6 Kutetemeka kuliwashika huko, maumivu kama ya mwanamke mwenye utungu wa kuzaa.
Trembling took hold of them there, pain, as of a woman in travail.
7 Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi zilizovunjwa na upepo wa mashariki.
With the east wind, you break the ships of Tarshish.
8 Kama tulivyokuwa tumesikia, ndivyo tulivyoona katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, katika mji wa Mungu wetu: Mungu ataufanya uwe salama milele.
As we have heard, so we have seen, in the city of Jehovah of hosts, in the city of our God. God will establish it forever. (Selah)
9 Ee Mungu, hekaluni mwako tunatafakari upendo wako usiokoma.
We have thought about your loving kindness, God, in the midst of your temple.
10 Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, mkono wako wa kuume umejazwa na haki.
As is your name, God, so is your praise to the farthest parts of the earth. Your right hand is full of righteousness.
11 Mlima Sayuni unashangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako.
Let Mount Zion be glad. Let the daughters of Judah rejoice, Because of your judgments.
12 Tembeeni katika Sayuni, uzungukeni mji, hesabuni minara yake;
Walk about Zion, and go around her. Number its towers.
13 yatafakarini vyema maboma yake, angalieni ngome zake, ili mpate kusimulia habari zake kwa kizazi kijacho.
Consider her defenses. Consider her palaces, that you may tell it to the next generation.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.
For this God is our God forever and ever. He will guide us forever.

< Zaburi 48 >