< Zaburi 41 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
[For the Chief Musician. A Psalm by David.] Blessed is he who considers the poor and needy. Jehovah will deliver him in the day of evil.
2 Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
Jehovah will protect him, and keep him alive. He shall be blessed on the earth, and he will not surrender him to the will of his enemies.
3 Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
Jehovah will sustain him on his sickbed, and restore him from his bed of illness.
4 Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
I said, "Jehovah, have mercy on me. Heal me, for I have sinned against you."
5 Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
My enemies speak evil against me: "When will he die, and his name perish?"
6 Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
If he comes to see me, he speaks falsehood. His heart gathers iniquity to itself. When he goes abroad, he tells it.
7 Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
All who hate me whisper together against me. They imagine the worst for me.
8 “Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
"A wicked thing is poured out on him; and he who lies down will not rise again."
9 Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
Even my own close friend, in whom I trusted, who ate my bread, has lifted up his heel against me.
10 Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
But you, Jehovah, have mercy on me, and raise me up, that I may repay them.
11 Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
By this I know that you delight in me, because my enemy doesn't triumph over me.
12 Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
As for me, you uphold me in my integrity, and set me in your presence forever.
13 Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.
Blessed be Jehovah, the God of Israel, from everlasting and to everlasting. Amen and amen.

< Zaburi 41 >