< Zaburi 37 >

1 Zaburi ya Daudi. Usisumbuke kwa ajili ya watendao maovu, wala usiwaonee wivu watendao mabaya,
לדוד אל-תתחר במרעים אל-תקנא בעשי עולה
2 kwa maana kama majani watanyauka mara, kama mimea ya kijani watakufa mara.
כי כחציר מהרה ימלו וכירק דשא יבולון
3 Mtumaini Bwana na utende yaliyo mema; Kaa katika nchi ukafurahie malisho salama.
בטח ביהוה ועשה-טוב שכן-ארץ ורעה אמונה
4 Jifurahishe katika Bwana naye atakupa haja za moyo wako.
והתענג על-יהוה ויתן-לך משאלת לבך
5 Mkabidhi Bwana njia yako, mtumaini yeye, naye atatenda hili:
גול על-יהוה דרכך ובטח עליו והוא יעשה
6 Yeye atafanya haki yako ingʼae kama mapambazuko, na hukumu ya shauri lako kama jua la adhuhuri.
והוציא כאור צדקך ומשפטך כצהרים
7 Tulia mbele za Bwana na umngojee kwa uvumilivu; usisumbuke watu wanapofanikiwa katika njia zao, wanapotekeleza mipango yao miovu.
דום ליהוה-- והתחולל-לו אל-תתחר במצליח דרכו באיש עשה מזמות
8 Epuka hasira na uache ghadhabu, usihangaike: itakuongoza tu kutenda uovu.
הרף מאף ועזב חמה אל-תתחר אך-להרע
9 Kwa maana waovu watakatiliwa mbali, bali wale wanaomtumaini Bwana watairithi nchi.
כי-מרעים יכרתון וקוי יהוה המה יירשו-ארץ
10 Bado kitambo kidogo, nao waovu hawataonekana, ingawa utawatafuta, hawataonekana.
ועוד מעט ואין רשע והתבוננת על-מקומו ואיננו
11 Bali wanyenyekevu watairithi nchi na wafurahie amani tele.
וענוים יירשו-ארץ והתענגו על-רב שלום
12 Waovu hula njama dhidi ya wenye haki na kuwasagia meno,
זמם רשע לצדיק וחרק עליו שניו
13 bali Bwana huwacheka waovu, kwa sababu anajua siku yao inakuja.
אדני ישחק-לו כי-ראה כי-יבא יומו
14 Waovu huchomoa upanga na kupinda upinde, ili wawaangushe maskini na wahitaji, kuwachinja wale ambao njia zao ni nyofu.
חרב פתחו רשעים-- ודרכו קשתם להפיל עני ואביון לטבוח ישרי-דרך
15 Lakini panga zao zitachoma mioyo yao wenyewe, na pinde zao zitavunjwa.
חרבם תבוא בלבם וקשתותם תשברנה
16 Bora kidogo walicho nacho wenye haki kuliko wingi wa mali wa waovu wengi;
טוב-מעט לצדיק-- מהמון רשעים רבים
17 kwa maana nguvu za waovu zitavunjwa, lakini Bwana humtegemeza mwenye haki.
כי זרועות רשעים תשברנה וסומך צדיקים יהוה
18 Bwana anazifahamu siku za wanyofu, na urithi wao utadumu milele.
יודע יהוה ימי תמימם ונחלתם לעולם תהיה
19 Siku za maafa hawatanyauka, siku za njaa watafurahia wingi wa vitu.
לא-יבשו בעת רעה ובימי רעבון ישבעו
20 Lakini waovu wataangamia: Adui za Bwana watakuwa kama uzuri wa mashamba, watatoweka, watatoweka kama moshi.
כי רשעים יאבדו ואיבי יהוה כיקר כרים כלו בעשן כלו
21 Waovu hukopa na hawalipi, bali wenye haki hutoa kwa ukarimu.
לוה רשע ולא ישלם וצדיק חונן ונותן
22 Wale wanaobarikiwa na Bwana watairithi nchi, bali wale anaowalaani watakatiliwa mbali.
כי מברכיו יירשו ארץ ומקלליו יכרתו
23 Kama Bwana akipendezwa na njia ya mtu, yeye huimarisha hatua zake,
מיהוה מצעדי-גבר כוננו ודרכו יחפץ
24 ajapojikwaa, hataanguka, kwa maana Bwana humtegemeza kwa mkono wake.
כי-יפל לא-יוטל כי-יהוה סומך ידו
25 Nilikuwa kijana na sasa ni mzee, lakini sijaona kamwe wenye haki wameachwa au watoto wao wakiombaomba chakula.
נער הייתי-- גם-זקנתי ולא-ראיתי צדיק נעזב וזרעו מבקש-לחם
26 Wakati wote ni wakarimu na hukopesha bila masharti. Watoto wao watabarikiwa.
כל-היום חונן ומלוה וזרעו לברכה
27 Acha ubaya na utende wema, nawe utaishi katika nchi milele.
סור מרע ועשה-טוב ושכן לעולם
28 Kwa kuwa Bwana huwapenda wenye haki naye hatawaacha waaminifu wake. Watalindwa milele, lakini uzao wa waovu utakatiliwa mbali.
כי יהוה אהב משפט ולא-יעזב את-חסידיו לעולם נשמרו וזרע רשעים נכרת
29 Wenye haki watairithi nchi, na kuishi humo milele.
צדיקים יירשו-ארץ וישכנו לעד עליה
30 Kinywa cha mwenye haki hutamka hekima, nao ulimi wake huzungumza lililo haki.
פי-צדיק יהגה חכמה ולשונו תדבר משפט
31 Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake; nyayo zake hazitelezi.
תורת אלהיו בלבו לא תמעד אשריו
32 Watu waovu huvizia wenye haki, wakitafuta kuwaua;
צופה רשע לצדיק ומבקש להמיתו
33 lakini Bwana hatawaacha mikononi mwao wala hatawaacha wahukumiwe kuwa wakosa wanaposhtakiwa.
יהוה לא-יעזבנו בידו ולא ירשיענו בהשפטו
34 Mngojee Bwana, na uishike njia yake. Naye atakutukuza uirithi nchi, waovu watakapokatiliwa mbali, utaliona hilo.
קוה אל-יהוה ושמר דרכו וירוממך לרשת ארץ בהכרת רשעים תראה
35 Nimemwona mtu mwovu na mkatili akistawi kama mwerezi wa Lebanoni,
ראיתי רשע עריץ ומתערה כאזרח רענן
36 lakini alitoweka mara na hakuonekana, ingawa nilimtafuta, hakupatikana.
ויעבר והנה איננו ואבקשהו ולא נמצא
37 Watafakari watu wasio na hatia, wachunguze watu wakamilifu, kuna mafanikio kwa mtu apendaye amani.
שמר-תם וראה ישר כי-אחרית לאיש שלום
38 Lakini watenda dhambi wote wataangamizwa, mafanikio yao yatakatiliwa mbali.
ופשעים נשמדו יחדו אחרית רשעים נכרתה
39 Wokovu wa wenye haki hutoka kwa Bwana, yeye ni ngome yao wakati wa shida.
ותשועת צדיקים מיהוה מעוזם בעת צרה
40 Bwana huwasaidia na kuwaokoa, huwaokoa kutoka kwa waovu na kuwahifadhi, kwa maana wanamkimbilia.
ויעזרם יהוה ויפלטם יפלטם מרשעים ויושיעם--כי-חסו בו

< Zaburi 37 >