< Zaburi 34 >

1 Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
[By David; when he pretended to be insane before Abimelech, who drove him away, and he departed.] I will bless Jehovah at all times. His praise will always be in my mouth.
2 Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
My soul shall boast in Jehovah. The humble shall hear of it, and be glad.
3 Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
Oh magnify Jehovah with me. Let us exalt his name together.
4 Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
I sought Jehovah, and he answered me, and delivered me from all my fears.
5 Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
They looked to him and were radiant, and their faces are not ashamed.
6 Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
This poor man cried, and Jehovah heard him, and saved him out of all his troubles.
7 Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
The angel of Jehovah encamps around those who fear him, and delivers them.
8 Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
Oh taste and see that Jehovah is good. Blessed is the man who takes refuge in him.
9 Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
Oh fear Jehovah, you his holy ones, for there is no lack with those who fear him.
10 Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
The young lions do lack, and suffer hunger, but those who seek Jehovah shall not lack any good thing.
11 Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
Come, you children, listen to me. I will teach you the fear of Jehovah.
12 Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
Who is someone who desires life, and loves many days, that he may see good?
13 basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
Keep your tongue from evil, and your lips from speaking lies.
14 Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
Turn away from evil, and do good. Seek peace, and pursue it.
15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
The eyes of Jehovah are toward the righteous. His ears listen to their cry.
16 Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
Jehovah's face is against those who do evil, to cut off the memory of them from the earth.
17 Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
The righteous cry out, and Jehovah hears, and delivers them out of all their troubles.
18 Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
Jehovah is near to those who have a broken heart, and saves those who have a crushed spirit.
19 Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
Many are the afflictions of the righteous, but Jehovah delivers him out of them all.
20 huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
He protects all of his bones. Not one of them is broken.
21 Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
Evil shall kill the wicked. Those who hate the righteous shall be condemned.
22 Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.
Jehovah redeems the soul of his servants. None of those who take refuge in him shall be condemned.

< Zaburi 34 >