< Zaburi 33 >

1 Mwimbieni Bwana kwa furaha, enyi wenye haki; kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.
Rejoice in the LORD, O ye righteous: [for] praise is comely for the upright.
2 Msifuni Bwana kwa kinubi, mwimbieni sifa kwa zeze la nyuzi kumi.
Praise the LORD with harp: sing to him with the psaltery [and] an instrument of ten strings.
3 Mwimbieni wimbo mpya; pigeni kwa ustadi, na mpaze sauti za shangwe.
Sing to him a new song; play skillfully with a loud noise.
4 Maana neno la Bwana ni haki na kweli, ni mwaminifu kwa yote atendayo.
For the word of the LORD [is] right; and all his works [are done] in truth.
5 Bwana hupenda uadilifu na haki; dunia imejaa upendo wake usiokoma.
He loveth righteousness and judgment: the earth is full of the goodness of the LORD.
6 Kwa neno la Bwana mbingu ziliumbwa, jeshi lao la angani kwa pumzi ya kinywa chake.
By the word of the LORD were the heavens made; and all the host of them by the breath of his mouth.
7 Ameyakusanya maji ya bahari kama kwenye chungu; vilindi vya bahari ameviweka katika ghala.
He gathereth the waters of the sea together as a heap: he layeth up the depth in store-houses.
8 Dunia yote na imwogope Bwana, watu wote wa dunia wamche.
Let all the earth fear the LORD: let all the inhabitants of the world stand in awe of him.
9 Kwa maana Mungu alisema, na ikawa, aliamuru na ikasimama imara.
For he spoke, and it was [done]; he commanded, and it stood fast.
10 Bwana huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa.
The LORD bringeth the counsel of the heathen to naught: he maketh the devices of the people of no effect.
11 Lakini mipango ya Bwana inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote.
The counsel of the LORD standeth for ever, the thoughts of his heart to all generations.
12 Heri taifa ambalo Bwana ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake.
Blessed [is] the nation whose God [is] the LORD; [and] the people [whom] he hath chosen for his own inheritance.
13 Kutoka mbinguni Bwana hutazama chini na kuwaona wanadamu wote;
The LORD looketh from heaven; he beholdeth all the sons of men.
14 kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani:
From the place of his habitation he looketh upon all the inhabitants of the earth.
15 yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda.
He fashioneth their hearts alike; he considereth all their works.
16 Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake.
There is no king saved by the multitude of a host: a mighty man is not delivered by much strength.
17 Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa.
A horse [is] a vain thing for safety: neither shall he deliver [any] by his great strength.
18 Lakini macho ya Bwana yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo,
Behold, the eye of the LORD [is] upon them that fear him, upon them that hope in his mercy;
19 ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa.
To deliver their soul from death, and to keep them alive in famine.
20 Sisi tunamngojea Bwana kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu.
Our soul waiteth for the LORD: he [is] our help and our shield.
21 Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu.
For our heart shall rejoice in him, because we have trusted in his holy name.
22 Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee Bwana, tunapoliweka tumaini letu kwako.
Let thy mercy, O LORD, be upon us, according as we hope in thee.

< Zaburi 33 >