< Zaburi 3 >

1 Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
Psalmus David, Cum fugeret a facie Absalom filii sui. Domine quid multiplicati sunt qui tribulant me? multi insurgunt adversum me.
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
Multi dicunt animae meae: Non est salus ipsi in Deo eius.
3 Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
Tu autem Domine susceptor meus es, gloria mea, et exaltans caput meum.
4 Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
Voce mea ad Dominum clamavi: et exaudivit me de monte sancto suo.
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
Ego dormivi, et soporatus sum: et exurrexi, quia Dominus suscepit me.
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
Non timebo millia populi circumdantis me: exurge Domine: salvum me fac Deus meus.
7 Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
Quoniam tu percussisti omnes adversantes mihi sine causa: dentes peccatorum contrivisti.
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
Domini est salus: et super populum tuum benedictio tua.

< Zaburi 3 >