< Zaburi 3 >

1 Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
Éternel, que mes ennemis sont nombreux! Combien de gens se lèvent contre moi!
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
Combien, qui disent de mon âme: Point de salut pour lui auprès de Dieu! (Sélah, pause)
3 Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
Mais toi, Éternel, tu es mon bouclier, ma gloire, et celui qui me fait lever la tête.
4 Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
Je crie de ma voix à l'Éternel, et il me répond de sa montagne sainte. (Sélah)
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.
Je me couche, je m'endors, et je me réveille; car l'Éternel me soutient.
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
Je ne crains point les milliers d'hommes qui se rangent de toute part contre moi.
7 Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
Lève-toi, Éternel, sauve-moi, mon Dieu! Car tu as frappé à la joue tous mes ennemis, tu as brisé les dents des méchants.
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
Le salut vient de l'Éternel; ta bénédiction est sur ton peuple! (Sélah)

< Zaburi 3 >