< Zaburi 29 >

1 Zaburi ya Daudi. Mpeni Bwana, enyi mashujaa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
[A Psalm by David.] Ascribe to Jehovah, you sons of the mighty, ascribe to Jehovah glory and strength.
2 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
Ascribe to Jehovah the glory due to his name. Worship Jehovah in holy array.
3 Sauti ya Bwana iko juu ya maji; Mungu wa utukufu hupiga radi, Bwana hupiga radi juu ya maji makuu.
The voice of Jehovah is on the waters. The God of glory thunders, even Jehovah on many waters.
4 Sauti ya Bwana ina nguvu; sauti ya Bwana ni tukufu.
The voice of Jehovah is powerful. The voice of Jehovah is full of majesty.
5 Sauti ya Bwana huvunja mierezi; Bwana huvunja vipande vipande mierezi ya Lebanoni.
The voice of Jehovah breaks the cedars. Yes, Jehovah breaks in pieces the cedars of Lebanon.
6 Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama, Sirioni urukaruke kama mwana nyati.
He makes them also to skip like a calf; Lebanon and Sirion like a young, wild ox.
7 Sauti ya Bwana hupiga kwa miali ya umeme wa radi.
The voice of Jehovah strikes with flashes of lightning.
8 Sauti ya Bwana hutikisa jangwa; Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi.
The voice of Jehovah shakes the wilderness. Jehovah shakes the wilderness of Kadesh.
9 Sauti ya Bwana huzalisha ayala, na huuacha msitu wazi. Hekaluni mwake wote wasema, “Utukufu!”
The voice of Jehovah makes the large trees tremble, and strips the forests bare. In his temple everything says, "Glory."
10 Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika; Bwana ametawazwa kuwa Mfalme milele.
Jehovah sat enthroned at the Flood. Yes, Jehovah sits as King forever.
11 Bwana huwapa watu wake nguvu; Bwana huwabariki watu wake kwa kuwapa amani.
Jehovah will give strength to his people. Jehovah will bless his people with peace.

< Zaburi 29 >