< Zaburi 22 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
Til sangmesteren; efter "Morgenrødens hind"; en salme av David. Min Gud! Min Gud! Hvorfor har du forlatt mig? Langt borte fra min frelse er min klages ord.
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
Min Gud! Jeg roper om dagen, og du svarer ikke, og om natten, og jeg får ikke tie.
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
Og du er dog hellig, du som troner over Israels lovsanger.
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
Til dig satte våre fedre sin lit; de satte sin lit til dig, og du utfridde dem.
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
Til dig ropte de, og de blev reddet; til dig satte de sin lit, og de blev ikke til skamme.
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
Men jeg er en orm og ikke en mann, menneskers spott og folks forakt.
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
Alle de som ser mig, spotter mig, vrenger munnen, ryster på hodet og sier:
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
Sett din vei i Herrens hånd! Han skal redde ham, han skal utfri ham, siden han har behag i ham.
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
Ja, du er den som drog mig frem av mors liv, som lot mig hvile trygt ved min mors bryst.
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
På dig er jeg kastet fra mors liv; fra min mors skjød er du min Gud.
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
Vær ikke langt borte fra mig! for trengselen er nær, og det er ingen hjelper.
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
Sterke okser omringer mig, Basans okser kringsetter mig.
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
De spiler op sin munn imot mig som en sønderrivende og brølende løve.
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
Jeg er utøst som vann, og alle mine ben skiller sig at; mitt hjerte er som voks, smeltet midt i mitt liv.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
Min kraft er optørket som et potteskår, og min tunge henger fast ved mine gommer, og i dødens støv legger du mig.
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
For hunder omringer mig, de ondes hop kringsetter mig; de har gjennemboret mine hender og mine føtter.
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
Jeg kan telle alle mine ben; de ser til, de ser på mig med lyst.
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
De deler mine klær mellem sig og kaster lodd om min kjortel.
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
Men du? Herre, vær ikke langt borte, du min styrke, skynd dig å hjelpe mig!
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
Redd min sjel fra sverdet, mitt eneste fra hunders vold!
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Frels mig fra løvens gap, og fra villoksenes horn - du bønnhører mig!
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
Jeg vil kunngjøre ditt navn for mine brødre, midt i menigheten vil jeg love dig.
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
I som frykter Herren, lov ham, all Jakobs ætt, ær ham, og frykt for ham, all Israels ætt!
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
For han har ikke foraktet og ikke avskydd den elendiges elendighet og ikke skjult sitt åsyn for ham; men da han ropte til ham, hørte han.
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
Fra dig utgår min pris i en stor forsamling; mine løfter vil jeg holde for deres øine som frykter ham.
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
De saktmodige skal ete og bli mette; de som søker Herren, skal love ham; eders hjerte leve til evig tid!
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
Alle jordens ender skal komme det i hu og vende om til Herren, og alle folkenes slekter skal tilbede for ditt åsyn.
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
For riket hører Herren til, og han hersker over folkene.
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
Alle jordens rikmenn skal ete og tilbede; for hans åsyn skal alle de bøie sig som stiger ned i støvet, og den som ikke kan holde sin sjel i live.
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
Efterkommerne skal tjene ham, der skal fortelles om Herren til efterslekten.
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
De skal komme og kunngjøre hans rettferdighet for det folk som blir født, at han har gjort det.

< Zaburi 22 >