< Zaburi 22 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
For the chief musician; set to “The rhythm of the deer.” A psalm of David. My God, my God, why have you abandoned me? Why are you so far from saving me and far from the words of my anguish?
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
My God, I cry out in the daytime, but you do not answer, and at night I am not silent!
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
Yet you are holy; you sit as king with the praises of Israel.
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
Our ancestors trusted in you; they trusted in you, and you rescued them.
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
They cried to you and they were rescued. They trusted in you and were not disappointed.
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
But I am a worm and not a man, a disgrace to humanity and despised by the people.
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
All those who see me taunt me; they mock me; they shake their heads at me.
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
They say, “He trusts in Yahweh; let Yahweh rescue him. Let him rescue him, for he delights in him.”
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
For you brought me from the womb; you made me trust you when I was on my mother's breasts.
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
I have been thrown on you from the womb; you are my God since I was in my mother's womb!
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
Do not be far away from me, for trouble is near; there is no one to help.
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
Many bulls surround me; strong bulls of Bashan surround me.
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
They open their mouths wide against me like a roaring lion ripping its victim.
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
I am being poured out like water, and all my bones are dislocated. My heart is like wax; it melts away within my inner parts.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
My strength has dried up like a piece of pottery; my tongue sticks to the roof of my mouth. You have laid me in the dust of death.
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
For dogs have surrounded me; a company of evildoers has encircled me; they have pierced my hands and my feet.
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
I can count all my bones. They look and stare at me.
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
They divide my garments among themselves, they cast lots for my clothes.
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
Do not be far away, Yahweh; please hurry to help me, my strength!
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
Rescue my soul from the sword, my only life from the claws of wild dogs.
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Save me from the lion's mouth; rescue me from the horns of the wild oxen.
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
I will declare your name to my brothers; in the midst of the assembly I will praise you.
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
You who fear Yahweh, praise him! All you descendants of Jacob, honor him! Stand in awe of him, all you descendants of Israel!
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
For he has not despised or abhorred the suffering of the afflicted one; Yahweh has not hidden his face from him; when the afflicted one cried to him, he heard.
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
My praise will be because of you in the great assembly; I will fulfill my vows before those who fear him.
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
The oppressed will eat and be satisfied; those who seek Yahweh will praise him. May your hearts live forever.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
All the peoples of the earth will remember and turn to Yahweh; all the families of the nations will bow down before you.
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
For the kingdom is Yahweh's; he is the ruler over the nations.
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
All the prosperous people of the earth will feast and will worship; all those who are descending into the dust will bow before him, those who cannot preserve their own lives.
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
A generation to come will serve him; they will tell the next generation of the Lord.
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
They will come and tell of his righteousness; they will tell to a people not yet born what he has done!

< Zaburi 22 >