< Zaburi 22 >

1 Kwa mwimbishaji. Mtindo wa utenzi wa “Kulungu wa Alfajiri.” Zaburi ya Daudi. Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu?
For the leader; set to “Deer of the Dawn”. A psalm of David. My God, my God, why have you left me, my rescue so far from the words of my roaring?
2 Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, hata usiku, sinyamazi.
I cry in the day, you do not answer, I cry in the night but find no rest.
3 Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; wewe ni sifa ya Israeli.
You are the Holy One, throned on the praises of Israel.
4 Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, walikutumaini nawe ukawaokoa.
In you our ancestors trusted, they trusted and you delivered them.
5 Walikulilia wewe na ukawaokoa, walikutegemea wewe nao hawakuaibika.
They cried to you, and found safety, in you did they trust and were not put to shame.
6 Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau.
But I am a worm, not a person; insulted by others, despised by the people.
7 Wote wanionao hunidhihaki, hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao:
All who see me mock me, with mouths wide open and wagging heads:
8 Husema, “Anamtegemea Bwana, basi Bwana na amwokoe. Amkomboe basi, kwa maana anapendezwa naye.”
‘He relies on the Lord; let him save him. Let him rescue the one he holds dear!’
9 Hata hivyo ulinitoa tumboni, ukanifanya nikutegemee, hata nilipokuwa ninanyonya matiti ya mama yangu.
But you drew me from the womb, laid me safely on my mother’s breasts.
10 Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, toka tumboni mwa mama yangu umekuwa Mungu wangu.
On your care was I cast from my very birth, you are my God from my mother’s womb.
11 Usiwe mbali nami, kwa maana shida iko karibu na hakuna wa kunisaidia.
Be not far from me, for trouble is nigh, and there is none to help.
12 Mafahali wengi wamenizunguka, mafahali wa Bashani wenye nguvu wamenizingira.
I am circled by many bulls, beset by the mighty of Bashan,
13 Simba wangurumao wanaorarua mawindo yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu.
who face me with gaping jaws, like ravening roaring lions.
14 Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.
Poured out am I like water, and all my bones are loosened. My heart is become like wax, melted within me.
15 Nguvu zangu zimekauka kama kigae, ulimi wangu umegandamana na kaakaa la kinywa changu, kwa sababu umenilaza katika mavumbi ya kifo.
My palate is dry as a sherd, my tongue sticks to my jaws; in the dust of death you lay me.
16 Mbwa wamenizunguka, kundi la watu waovu limenizingira, wametoboa mikono yangu na miguu yangu.
For dogs are round about me, a band of knaves encircles me, gnawing my hands and my feet.
17 Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, watu wananikodolea macho na kunisimanga.
I can count my bones, every one. As for them, they feast their eyes on me.
18 Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, na vazi langu wanalipigia kura.
They divide my garments among them, and over my raiment cast lots.
19 Lakini wewe, Ee Bwana, usiwe mbali. Ee Nguvu yangu, uje haraka unisaidie.
But you, O Lord, be not far, O my strength, hasten to help me.
20 Okoa maisha yangu na upanga, uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa.
Deliver my life from the sword my life from the power of the dogs.
21 Niokoe kutoka kinywani mwa simba, niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu.
Save me from the jaws of the lion, from the horns of the wild oxen help me.
22 Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, katika kusanyiko nitakusifu wewe.
I will tell of your fame to my kindred, and in the assembly will praise you.
23 Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli!
Praise the Lord, you who fear him. All Jacob’s seed, give him glory. All Israel’s seed, stand in awe of him.
24 Kwa maana hakupuuza wala kudharau mateso ya aliyeonewa; hakumficha uso wake bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie.
For he has not despised nor abhorred the sorrow of the sorrowful. He hid not his face from me, but he listened to my cry for help.
25 Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe.
Of you is my praise in the great congregation; my vows I will pay before those who fear him.
26 Maskini watakula na kushiba, wale wamtafutao Bwana watamsifu: mioyo yenu na iishi milele!
The afflicted will eat to their heart’s desire, and those who seek after the Lord will praise him. Lift up your hearts forever.
27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Bwana, nazo jamaa zote za mataifa watasujudu mbele zake,
All will call it to mind, to the ends of the earth, and turn to the Lord; and all tribes of the nations will bow down before you.
28 kwa maana ufalme ni wa Bwana naye hutawala juu ya mataifa.
For the kingdom belongs to the Lord: he is the Lord of the nations.
29 Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. Wote waendao mavumbini watapiga magoti mbele yake, wote ambao hawawezi kudumisha uhai wao.
To him will bow down all who sleep in the earth, and before him bend all who go down to the dust, and those who could not preserve their lives.
30 Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana.
My descendants will tell of the Lord to the next generation;
31 Watatangaza haki yake kwa watu ambao hawajazaliwa bado, kwa maana yeye ametenda hili.
they will declare his righteousness to people yet to be born: He has done it.

< Zaburi 22 >