< Zaburi 19 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu, anga zahubiri kazi ya mikono yake.
[For the Chief Musician. A Psalm by David.] The heavens declare the glory of God. The expanse shows his handiwork.
2 Siku baada ya siku zinatoa habari, usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
Day after day they pour forth speech, and night after night they display knowledge.
3 Hakuna msemo wala lugha, ambapo sauti zao hazisikiki.
There is no speech nor language, where their voice is not heard.
4 Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu. Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
Their voice has gone out to all the earth, their words to the farthest part of the world. In them he has set a tent for the sun,
5 linafanana na bwana arusi akitoka chumbani mwake, kama shujaa afurahiavyo kukamilisha kushindana kwake.
which is as a bridegroom coming out of his chamber, like a strong man rejoicing to run his course.
6 Huchomoza upande mmoja wa mbingu, na kufanya mzunguko wake hadi upande mwingine. Hakuna kilichojificha joto lake.
His going forth is from the end of the heavens, his circuit to its ends; There is nothing hidden from its heat.
7 Sheria ya Bwana ni kamilifu, ikihuisha nafsi. Shuhuda za Bwana ni za kuaminika, zikimpa mjinga hekima.
Jehovah's Law is perfect, restoring the soul. Jehovah's testimony is sure, making wise the simple.
8 Maagizo ya Bwana ni kamili, nayo hufurahisha moyo. Amri za Bwana huangaza, zatia nuru machoni.
Jehovah's precepts are right, rejoicing the heart. Jehovah's commandment is pure, enlightening the eyes.
9 Kumcha Bwana ni utakatifu, nako kwadumu milele. Amri za Bwana ni za hakika, nazo zina haki.
The fear of Jehovah is clean, enduring forever. Jehovah's ordinances are true, and righteous altogether.
10 Ni za thamani kuliko dhahabu, kuliko dhahabu iliyo safi sana, ni tamu kuliko asali, kuliko asali kutoka kwenye sega.
More to be desired are they than gold, yes, than much fine gold; sweeter also than honey and the extract of the honeycomb.
11 Kwa hizo mtumishi wako anaonywa, katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
Moreover by them is your servant warned. In keeping them there is great reward.
12 Ni nani awezaye kutambua makosa yake? Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
Who can discern his errors? Forgive me from hidden errors.
13 Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi, nazo zisinitawale. Ndipo nitakapokuwa sina lawama, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.
Keep back your servant also from presumptuous sins. Let them not have dominion over me. Then I will be upright. I will be blameless and innocent of great transgression.
14 Maneno ya kinywa changu na mawazo ya moyo wangu, yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu na Mkombozi wangu.
Let the words of my mouth and the meditation of my heart be acceptable in your sight always, Jehovah, my rock and my redeemer.

< Zaburi 19 >