< Zaburi 18 >

1 Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi mtumishi wa Bwana aliyomwimbia Bwana wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli. Alisema hivi: Nakupenda wewe, Ee Bwana, nguvu yangu.
Il dit donc: Je t'aimerai, ô Éternel, qui es ma force!
2 Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu, Mungu wangu ni mwamba, ambaye kwake ninakimbilia. Yeye ni ngao yangu na pembe ya wokovu wangu, ngome yangu.
Éternel, mon rocher, ma forteresse et mon libérateur! Mon Dieu, mon rocher où je me réfugie! Mon bouclier, la force qui me délivre, ma haute retraite!
3 Ninamwita Bwana anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
Je m'écrie: Loué soit l'Éternel! et je suis délivré de mes ennemis.
4 Kamba za mauti zilinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Les liens de la mort m'avaient enveloppé, et les torrents de la destruction m'avaient épouvanté;
5 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
Les liens du Sépulcre m'entouraient, les pièges de la mort m'avaient surpris; (Sheol h7585)
6 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu anisaidie. Kutoka hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika mbele zake, masikioni mwake.
Dans ma détresse, j'invoquai l'Éternel, et je criai à mon Dieu. De son palais, il entendit ma voix, et les cris que je poussais vers lui parvinrent à ses oreilles.
7 Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Alors la terre fut ébranlée et trembla; les fondements des montagnes s'agitèrent et s'ébranlèrent, parce qu'il était courroucé.
8 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
Une fumée montait de ses narines, et de sa bouche un feu dévorant; il en jaillissait des charbons embrasés.
9 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Il abaissa les cieux et descendit, ayant l'obscurité sous ses pieds.
10 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
Il était monté sur un chérubin, et il volait; il était porté sur les ailes du vent.
11 Alifanya giza kuwa kitu chake cha kujifunika, hema lake kumzunguka, mawingu meusi ya mvua ya angani.
Il fit des ténèbres sa retraite; il mit autour de lui, comme une tente, des eaux ténébreuses, de noirs nuages.
12 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
De la splendeur qui était devant lui, s'échappaient des nuées, avec de la grêle et des charbons de feu.
13 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Et l'Éternel tonna dans les cieux, le Très-Haut fit retentir sa voix, avec de la grêle et des charbons de feu.
14 Aliipiga mishale yake na kutawanya adui, naam, umeme mwingi wa radi na kuwafukuza.
Il lança ses flèches, et dispersa mes ennemis; il lança des éclairs nombreux, et les mit en déroute.
15 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwako, Ee Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwako.
Alors le fond des eaux apparut, et les fondements du monde furent mis à découvert, au bruit de ta menace, ô Éternel, au souffle du vent de ta colère.
16 Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Il étendit sa main d'en haut, et me prit; il me tira des grosses eaux.
17 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Il me délivra de mon ennemi puissant, et de mes adversaires qui étaient plus forts que moi.
18 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Ils m'avaient surpris au jour de ma calamité; mais l'Éternel fut mon appui.
19 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Il m'a mis au large, il m'a délivré, parce qu'il a pris son plaisir en moi.
20 Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
L'Éternel m'a traité selon ma justice; il m'a rendu selon la pureté de mes mains.
21 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Car j'ai gardé les voies de l'Éternel, et je n'ai point été infidèle à mon Dieu.
22 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
Car toutes ses ordonnances sont devant moi, et je ne m'écarte point de ses statuts.
23 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
J'ai été intègre avec lui, et je me suis gardé de mon péché.
24 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu machoni pake.
Aussi l'Éternel m'a rendu selon ma justice, selon la pureté de mes mains devant ses yeux.
25 Kwa yeye aliye mwaminifu, unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia, unajionyesha kutokuwa na hatia.
Avec celui qui est bon, tu es bon; avec l'homme intègre, tu es intègre.
26 Kwa aliye mtakatifu, unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka, unajionyesha kuwa mkaidi.
Avec celui qui est pur, tu te montres pur; mais avec le pervers, tu agis selon sa perversité.
27 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini huwashusha wenye kiburi.
Car c'est toi qui sauves le peuple affligé, et qui abaisses les yeux des superbes.
28 Wewe, Ee Bwana, unaifanya taa yangu iendelee kuwaka; Mungu wangu hulifanya giza langu kuwa mwanga.
C'est toi qui fais luire ma lampe; c'est l'Éternel mon Dieu qui éclaire mes ténèbres.
29 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
Car avec toi je fonds sur une troupe; avec mon Dieu je franchis la muraille.
30 Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu, neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
La voie de Dieu est parfaite; la parole de l'Éternel est éprouvée; il est un bouclier pour tous ceux qui se retirent vers lui.
31 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Car qui est Dieu, sinon l'Éternel? Et qui est un rocher, sinon notre Dieu?
32 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Le Dieu qui me ceint de force, et qui a rendu mon chemin sûr;
33 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Qui rend mes pieds semblables à ceux des biches, et me fait tenir sur mes hauteurs;
34 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Qui forme mes mains au combat, et mes bras bandent un arc d'airain.
35 Hunipa ngao yako ya ushindi, nao mkono wako wa kuume hunitegemeza, unajishusha chini ili kuniinua.
Tu m'as donné le bouclier de ton salut; ta droite me soutient, et ta bonté me rend puissant.
36 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Tu élargis le chemin sous mes pas, et mes talons ne chancellent point.
37 Niliwafuatia adui zangu na nikawapata, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
Je poursuis mes ennemis; je les atteins, et je ne reviens qu'après les avoir exterminés.
38 Niliwaseta hata hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Je les frappe, et ils ne peuvent se relever; ils tombent sous mes pieds.
39 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Car tu m'as ceint de force pour le combat, tu fais plier sous moi mes adversaires.
40 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Tu fais tourner le dos à mes ennemis devant moi; ceux qui me haïssaient, je les détruis.
41 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Ils crient, mais il n'y a point de libérateur; ils crient à l'Éternel, mais il ne leur répond pas.
42 Niliwaponda kama mavumbi yanayopeperushwa na upepo; niliwamwaga nje kama tope barabarani.
Je les broie comme la poussière livrée au vent, je les jette au loin comme la boue des rues.
43 Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu; umenifanya kuwa kiongozi wa mataifa, watu ambao sikuwajua wananitumikia.
Tu me sauves des dissensions du peuple; tu me mets à la tête des nations; le peuple que je ne connaissais pas m'est assujetti.
44 Mara wanisikiapo hunitii, wageni hunyenyekea mbele yangu.
Au bruit de mon nom, ils m'obéissent; les fils de l'étranger viennent me flatter.
45 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Les fils de l'étranger défaillent, et sortent tremblants de leur retraite.
46 Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu Mwokozi wangu!
L'Éternel est vivant! Et béni soit mon rocher! Que le Dieu de mon salut soit exalté,
47 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, awatiishaye mataifa chini yangu,
Le Dieu qui me donne la vengeance, et qui range les peuples sous moi!
48 aniokoaye na adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
Toi qui me délivres de mes ennemis, qui m'élèves au-dessus de mes adversaires, qui me délivres de l'homme violent!
49 Kwa hiyo nitakusifu katikati ya mataifa, Ee Bwana; nitaliimbia sifa jina lako.
C'est pourquoi je te louerai, ô Éternel, parmi les nations, et je chanterai à ton nom.
50 Humpa mfalme wake ushindi mkuu, huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.
C'est lui qui délivre magnifiquement son roi, qui fait miséricorde à son Oint, à David et à sa postérité à jamais.

< Zaburi 18 >