< Zaburi 17 >

1 Sala ya Daudi. Sikia, Ee Bwana, kusihi kwangu kwa haki, sikiliza kilio changu. Tega sikio kwa ombi langu, halitoki kwenye midomo ya udanganyifu.
[A Prayer by David.] Hear, Jehovah, my righteous plea; Give ear to my prayer, that doesn't go out of deceitful lips.
2 Hukumu yangu na itoke kwako, macho yako na yaone yale yaliyo haki.
Let my sentence come forth from your presence. Let your eyes look on equity.
3 Ingawa unauchunguza moyo wangu na kunikagua usiku, ingawa umenijaribu, hutaona chochote. Nimeamua kwamba kinywa changu hakitatenda dhambi.
You have proved my heart. You have visited me in the night. You have tried me, and found nothing. I have resolved that my mouth shall not disobey.
4 Kuhusu matendo ya wanadamu: kwa neno la midomo yako, nimejiepusha na njia za wenye jeuri.
As for the works of men, by the word of your lips, I have kept myself from the ways of the violent.
5 Hatua zangu zimeshikamana na njia zako; nyayo zangu hazikuteleza.
My steps have held fast to your paths. My feet have not slipped.
6 Ee Mungu, ninakuita, kwa kuwa utanijibu, nitegee sikio lako na usikie ombi langu.
I have called on you, for you will answer me, God. Turn your ear to me. Hear my speech.
7 Uonyeshe ajabu ya upendo wako mkuu, wewe uokoaye kwa mkono wako wa kuume wale wanaokukimbilia kutokana na adui zao.
Show your marvelous loving kindness, you who save those who take refuge by your right hand from their enemies.
8 Nilinde kama mboni ya jicho lako, unifiche chini ya kivuli cha mbawa zako
Keep me as the apple of your eye. Hide me under the shadow of your wings,
9 kutokana na waovu wanaonishambulia, kutokana na adui wauaji wanaonizunguka.
from the wicked who oppress me, my deadly enemies, who surround me.
10 Huifunga mioyo yao iliyo migumu, vinywa vyao hunena kwa majivuno.
They close up their callous hearts. With their mouth they speak proudly.
11 Wamenifuatia nyayo zangu, sasa wamenizingira, wakiwa macho, waniangushe chini.
They have tracked me down; suddenly they surround me. They watch closely, crouching down to the ground.
12 Wamefanana na simba mwenye njaa awindaye, kama simba mkubwa anyemeleaye mafichoni.
He is like a lion that is greedy of his prey, as it were a young lion lurking in secret places.
13 Inuka, Ee Bwana, pambana nao, uwaangushe, niokoe kutokana na waovu kwa upanga wako.
Arise, Jehovah, confront him. Cast him down. Deliver my soul from the wicked by your sword;
14 Ee Bwana, mkono wako uniokoe na watu wa jinsi hii, kutokana na watu wa ulimwengu huu ambao fungu lao liko katika maisha haya. Na wapate adhabu ya kuwatosha. Watoto wao na wapate zaidi ya hayo, hukumu na iendelee kwa watoto wa watoto wao.
from men with your hand, Jehovah, from men of the world, whose portion is in this life. You fill their womb with treasure. They are satisfied with children, and they leave their wealth to their little ones.
15 Na mimi katika haki nitauona uso wako, niamkapo, nitaridhika kwa kuona sura yako.
As for me, I shall see your face in righteousness. I shall be satisfied, when I awake, with seeing your form.

< Zaburi 17 >