< Zaburi 146 >

1 Msifuni Bwana! Ee nafsi yangu, umsifu Bwana,
Praise JAH. Praise Jehovah, my soul.
2 Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo.
While I live, I will praise Jehovah. I will sing praises to my God as long as I exist.
3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa.
Do not put your trust in princes, each a son of man in whom there is no help.
4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
His spirit departs, and he returns to the earth. In that very day, his thoughts perish.
5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake,
Blessed is the one who has the God of Jacob for his help, whose hope is in Jehovah his God,
6 Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: Bwana anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele.
who made heaven and earth, the sea, and all that is in them; who keeps truth forever;
7 Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. Bwana huwaweka wafungwa huru,
who executes justice for the oppressed; who gives food to the hungry. Jehovah frees the prisoners.
8 Bwana huwafumbua vipofu macho, Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, Bwana huwapenda wenye haki.
Jehovah opens the eyes of the blind. Jehovah raises up those who are bowed down. Jehovah loves the righteous.
9 Bwana huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu.
Jehovah preserves the foreigners. He upholds the fatherless and widow, but the way of the wicked he turns upside down.
10 Bwana atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Bwana.
Jehovah will reign forever; your God, O Zion, to all generations. Praise JAH.

< Zaburi 146 >